Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 1/05 uku. 1
  • ‘Tunalishwa Maneno ya Imani’

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • ‘Tunalishwa Maneno ya Imani’
  • Huduma ya Ufalme—2005
  • Habari Zinazolingana
  • ‘Walioandaliwa Vifaa Kikamili kwa Ajili ya Kila Kazi Njema’
    Huduma Yetu ya Ufalme—1998
  • Mikutano Hunufaisha Vijana
    Huduma Yetu ya Ufalme—2000
  • Je, Wewe Hula Vyema Kiroho?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1997
  • “Anampa Nguvu Mtu Aliyechoka”
    Huduma ya Ufalme—2007
Pata Habari Zaidi
Huduma ya Ufalme—2005
km 1/05 uku. 1

‘Tunalishwa Maneno ya Imani’

1 Kuishi maisha ya ujitoaji-kimungu hutaka jitihada nyingi. (1 Tim. 4:7-10) Hatuwezi kufanya hivyo kwa nguvu zetu wenyewe, kwa kuwa tutachoka upesi na kujikwaa. (Isa. 40:29-31) Njia moja tunayoweza kupata nguvu kutoka kwa Yehova ni kwa “kulishwa maneno ya imani.”—1 Tim. 4:6.

2 Chakula Kingi cha Kiroho: Kupitia Neno lake na pia “mtumwa mwaminifu na mwenye busara,” Yehova huandaa chakula kingi cha kiroho. (Mt. 24:45) Je, sisi hujitahidi kunufaika na chakula hicho? Je, tunasoma Biblia kila siku? Je, tumetenga wakati wa kujifunza na kutafakari? (Zab. 1:2, 3) Chakula hicho cha kiroho chenye kujenga hututia nguvu na hutulinda na mambo yenye kudhoofisha imani yanayotokana na ulimwengu wa Shetani. (1 Yoh. 5:19) Yehova atakuwa nasi tukijaza akili zetu mambo yenye kujenga na kuyafuata maishani.—Flp. 4:8, 9.

3 Yehova pia hututia nguvu kupitia mikutano ya kutaniko. (Ebr. 10:24, 25) Mafundisho ya kiroho na ushirika wenye kujenga kwenye mikutano hiyo hutuimarisha ili kusimama imara wakati wa majaribu. (1 Pet. 5:9, 10) Kijana mmoja Mkristo alisema: “Ninakuwa shuleni mchana kutwa, na jambo hilo hunivunja moyo sana. Lakini mikutano ni kama sehemu yenye maji jangwani, ambako ninapata nguvu za kuvumilia shuleni siku inayofuata.” Tunabarikiwa sana tunapojitahidi kuhudhuria mikutano.

4 Kuhubiri Kweli: Kuwahubiria wengine kulikuwa kama chakula kwa Yesu. Kulimtia nguvu. (Yoh. 4:32-34) Vivyo hivyo, sisi hutiwa nguvu tunapozungumza na wengine kuhusu ahadi nzuri za Mungu. Pia, kuwa na mengi ya kufanya katika huduma hutusaidia kukazia akilini na moyoni mwetu Ufalme na baraka ambazo zitakuja hivi karibuni. Jambo hilo hutuburudisha kwelikweli.—Mt. 11:28-30.

5 Tuna pendeleo kubwa la kupata na kunufaika na chakula kingi cha kiroho ambacho Yehova anawaandalia watu wake leo. Na tuendelee kumsifu kwa vigelegele na shangwe.—Isa. 65:13, 14.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki