Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 6/05 uku. 1
  • Kuhubiri Hutusaidia Kuvumilia

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kuhubiri Hutusaidia Kuvumilia
  • Huduma ya Ufalme—2005
  • Habari Zinazolingana
  • Shikamana na Tengenezo la Yehova
    Tengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova
  • “Acheni Uvumilivu Ukamilishe Kazi Yake”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2016
  • Uvumilivu—Muhimu kwa Wakristo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1993
  • Uvumilivu Unaopata Ushindi
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
Pata Habari Zaidi
Huduma ya Ufalme—2005
km 6/05 uku. 1

Kuhubiri Hutusaidia Kuvumilia

1 Neno la Mungu linatuhimiza “tukimbie kwa uvumilivu shindano la mbio lililowekwa mbele yetu.” (Ebr. 12:1) Kama mkimbiaji anavyohitaji kuvumilia ili amalize mbio, ndivyo tunavyohitaji kuvumilia ili tupate zawadi ya uzima wa milele. (Ebr. 10:36) Huduma ya Kikristo inaweza kutusaidiaje kuvumilia kwa uaminifu mpaka mwisho?—Mt. 24:13.

2 Tunaimarishwa Kiroho: Kutangaza ahadi nzuri ya Biblia kuhusu ulimwengu mpya wenye uadilifu hutusaidia kudumisha uhakika wa tumaini letu wenyewe. (1 The. 5:8) Tunapohubiri kwa ukawaida, tunakuwa na fursa ya kuwajulisha wengine kweli ambazo tumejifunza kutoka katika Biblia. Tunapata fursa ya kuitetea imani yetu, na kufanya hivyo hutuimarisha kiroho.

3 Ni lazima tuelewe waziwazi kweli za Biblia ili tuweze kuwafundisha wengine vizuri. Tunahitaji kufanya utafiti na kutafakari kuhusu habari hiyo. Tunapojitahidi kufanya hivyo, ujuzi wetu unaongezeka, imani yetu inaimarika, na tunapata nguvu mpya ya kiroho. (Met. 2:3-5) Kwa hiyo, tunapojitahidi kuwasaidia wengine, tunajiimarisha sisi wenyewe.—1 Tim. 4:15, 16.

4 Kuhubiri kwa bidii ni sehemu muhimu ya “mavazi kamili ya silaha kutoka kwa Mungu,” ambayo tunahitaji ili kusimama imara dhidi ya Ibilisi na roho wake waovu. (Efe. 6:10-13, 15) Kujishughulisha sana na utumishi mtakatifu hutusaidia kukazia akilini mwetu mambo yanayojenga na kuepuka kuchafuliwa na ulimwengu wa Shetani. (Kol. 3:2) Tunapowafundisha wengine njia za Yehova, tunakumbushwa daima kwamba sisi pia tunahitaji kudumisha mwenendo mtakatifu.—1 Pet. 2:12.

5 Mungu Anatutia Nguvu: Hatimaye, kushiriki katika kazi ya kueneza injili hutufundisha kumtegemea Yehova. (2 Kor. 4:1, 7) Ni baraka iliyoje! Kusitawisha sifa hiyo ya kumtegemea Yehova hutusaidia kutimiza huduma yetu na vilevile kukabiliana na hali yoyote maishani. (Flp. 4:11-13) Kwa kweli, kujifunza kumtegemea Yehova kabisa ndio msingi wa kuvumilia. (Zab. 55:22) Kuhubiri hutusaidia katika njia nyingi kuvumilia.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki