Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 9/05 uku. 7
  • Endeleeni Kujengana

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Endeleeni Kujengana
  • Huduma ya Ufalme—2005
  • Habari Zinazolingana
  • Tenda Mema na Uwe Mkarimu
    Huduma ya Ufalme—2005
  • Kujengana Tunapokuwa Katika Huduma
    Huduma Yetu ya Ufalme—2008
  • ‘Endeleeni Kujengana’
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2022
  • Mazungumzo ya Kiroho Hujenga
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2003
Pata Habari Zaidi
Huduma ya Ufalme—2005
km 9/05 uku. 7

Endeleeni Kujengana

1 Mtume Paulo alifanya yote aliyoweza ili awaimarishe waamini wenzake. (Mdo. 14:19-22) Hali kadhalika, tunahangaika wakati ndugu zetu wanapokabili hali ngumu, nasi hutamani kuwasaidia. Biblia inaonyesha kwamba si wazee tu wanaopaswa kuwajali wengine, bali kwamba sisi sote tunapaswa kufanya hivyo. (Rom. 15:1, 2) Fikiria njia mbili za kuonyesha kwamba tunatii himizo hili la upendo: “Endeleeni kufarijiana na kujengana.”—1 The. 5:11.

2 Tambua Mahitaji ya Wengine: Neno la Mungu linasema kwamba Dorkasi “alizidi katika matendo mema na zawadi za rehema.” (Mdo. 9:36, 39) Alitambua wale waliokuwa na uhitaji na akafanya yale aliyoweza ili kuwasaidia. Alituwekea mfano bora sana. Huenda unajua kwamba ndugu au dada fulani aliye mzee anahitaji msaada ili afike mikutanoni. Au huenda painia fulani angetaka mtu wa kuandamana naye kwenye utumishi wa shambani alasiri moja katikati ya juma. Wazia jinsi mtu mwenye uhitaji atakavyotiwa moyo ukitambua uhitaji wake na kumsaidia!

3 Kuzungumzia Mambo ya Kiroho: Tunaweza pia kuwajenga wengine kwa mazungumzo yetu. (Efe. 4:29) Mzee mmoja mwenye ujuzi alisema hivi: “Ukitaka kuwatia wengine moyo, zungumzia mambo ya kiroho. Ili kuanzisha mazungumzo yenye kujenga, unaweza kuuliza swali rahisi kama vile, ‘Ulipataje kweli?’” Wajali sana vijana kutanikoni. Wahangaikie wale waliovunjika moyo na wale walio na haya. (Met. 12:25) Usiruhusu mazungumzo kuhusu burudani za ulimwengu yakuzuie usizungumzie mambo mazuri ya kiroho pamoja na waamini wenzako.—Rom. 1:11, 12.

4 Lakini unaweza kusema nini ili uwajenge wengine? Ulipokuwa ukisoma na kujifunza Biblia kibinafsi hivi karibuni je, ulipata kanuni fulani iliyokufanya umpende Yehova zaidi? Je, ulichochewa na jambo fulani ulilosikia katika hotuba ya watu wote au kwenye Funzo la Mnara wa Mlinzi? Au je, ulivutiwa na jambo fulani lililoonwa lenye kuimarisha imani? Ikiwa unathamini sana mambo hayo ya kiroho yenye thamani, nyakati zote utakuwa na jambo lenye kutia moyo unaloweza kuwaambia wengine.—Met. 2:1; Luka 6:45.

5 Na tuendelee kujengana kwa kusaidiana na kwa kutumia ndimi zetu kwa hekima.—Met. 12:18.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki