Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 9/05 uku. 8
  • Wasaidie Wengine ‘Watii Kutoka Moyoni’

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Wasaidie Wengine ‘Watii Kutoka Moyoni’
  • Huduma ya Ufalme—2005
  • Habari Zinazolingana
  • Je, Una ‘Moyo Mtiifu’?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1998
  • “Kumpenda Mungu Humaanisha Hivi”
    “Jitunzeni Katika Upendo wa Mungu”
  • Yehova Anathamini Utii Wako
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2007
  • Jifunze Utii kwa Kukubali Nidhamu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
Pata Habari Zaidi
Huduma ya Ufalme—2005
km 9/05 uku. 8

Wasaidie Wengine ‘Watii Kutoka Moyoni’

1 Utii ni takwa muhimu la kumwabudu Yehova kwa njia inayokubalika. (Kum. 12:28; 1 Pet. 1:14-16) Hivi karibuni, Mungu atawahukumu “wale wasiomjua Mungu na wale wasiotii habari njema.” (2 The. 1:8) Tunaweza kuwasaidiaje wengine ‘watii kutoka moyoni’ mafundisho ya Neno la Mungu?—Rom. 6:17.

2 Kwa Kuwasaidia Wasitawishe Imani na Upendo: Maandiko huhusianisha sana utii na imani. Mtume Paulo alizungumzia “amri ya Mungu anayedumu milele ili kuendeleza utii kwa njia ya imani.” (Rom. 16:26) Kitabu cha Waebrania sura ya 11 kina mifano chungu nzima ya watu waliokuwa na imani, na mingi kati ya mifano hiyo inahusisha kutenda kupatana na maagizo ya Yehova. (Ebr. 11:7, 8, 17) Kwa upande mwingine, kutotii huhusianishwa na ukosefu wa imani. (Yoh. 3:36; Ebr. 3:18, 19) Tunahitaji kuboresha ustadi wetu wa kutumia Neno la Mungu ili tuweze kuwasaidia wengine wasitawishe imani itakayowafanya wawe watiifu.—2 Tim. 2:15; Yak. 2:14, 17.

3 Utii unahusianishwa pia na upendo. (Kum. 5:10; 11:1, 22; 30:16) Andiko la 1 Yohana 5:3 linasema hivi: “Kwa maana kumpenda Mungu humaanisha hivi, kwamba tuzishike amri zake; na bado amri zake si mzigo mzito.” Unaweza kumsaidiaje mwanafunzi wa Biblia ampende Yehova? Mnapojifunza, tafuta fursa za kumsaidia athamini zaidi sifa za Yehova. Mweleze jinsi unavyompenda Mungu sana. Msaidie mwanafunzi afikirie jinsi anavyoweza kusitawisha uhusiano wa kibinafsi pamoja na Yehova. Upendo ndio muhimu zaidi kati ya mambo yote ambayo hutuchochea na kuwachochea wengine wamtii Yehova.—Mt. 22:37.

4 Kwa Kuweka Mfano: Njia bora zaidi ya kuwachochea wengine waitii habari njema ni kuwawekea mfano. Lakini tunahitaji kujitahidi daima ili tuwe na “moyo mtiifu.” (1 Fal. 3:9; Met. 4:23) Jitihada hizo zinahusisha nini? Lisha moyo wako kwa kujifunza Biblia kwa ukawaida na kuhudhuria mikutano. (Zab. 1:1, 2; Ebr. 10:24, 25) Shirikiana na watu ambao mioyo yao imeungana katika ibada ya kweli. (Met. 13:20) Hubiri kwa ukawaida ukiwa na tamaa ya kuwasaidia watu katika eneo lenu. Mwombe Yehova akusaidie kusitawisha moyo mzuri. (Zab. 86:11) Epuka mambo yanayoweza kufisidi moyo wako kama vile burudani zenye ukosefu wa maadili au zenye jeuri. Fuatia mambo yatakayokusaidia kumkaribia Mungu na kuimarisha uhusiano wako pamoja naye.—Yak. 4:7, 8.

5 Yehova aliwahakikishia watu wake wa kale kwamba baraka zingewafikia ikiwa wangesikiliza sauti yake. (Kum. 28:1, 2) Hali kadhalika leo, Yehova anawabariki sana “wale wanaomtii yeye akiwa mtawala.” (Mdo. 5:32) Hivyo, tuwasaidie wengine watii kutoka moyoni kwa kuwafundisha na kwa mfano wetu.

[Maswali ya Funzo]

1. Yehova anataka waabudu wake wafanye nini?

2. Kwa nini ni muhimu kuwasaidia wengine wasitawishe imani yenye nguvu?

3. (a) Utii unahusianaje na upendo? (b) Unaweza kumsaidiaje mwanafunzi wa Biblia ampende Yehova?

4. (a) Kwa nini mfano wetu ni muhimu? (b) Tunapaswa kufanya nini ili tusitawishe “moyo mtiifu”?

5. Watu watiifu wanabarikiwa kwa njia gani?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki