Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 11/05 uku. 1
  • Tangazeni Utukufu wa Yehova

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Tangazeni Utukufu wa Yehova
  • Huduma ya Ufalme—2005
  • Habari Zinazolingana
  • “Mpeni Yehova utukufu ambao jina lake linastahili.”—Zaburi 96:8.
    “Mpeni Yehova utukufu ambao jina lake linastahili.”—Zaburi 96:8.
  • Mpeni Yehova Utukufu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2025
  • Kujulisha Jina la Mungu
    Huduma Yetu ya Ufalme—2003
  • Kwa Nini Ni Lazima Tujue Jina la Mungu
    Jina la Mungu Litakaloendelea Milele
Pata Habari Zaidi
Huduma ya Ufalme—2005
km 11/05 uku. 1

Tangazeni Utukufu wa Yehova

1 Mtunga-zaburi alitangaza hivi: “Mwimbieni Yehova, enyi watu wote wa dunia. Tangazeni utukufu wake kati ya mataifa, kazi zake za ajabu kati ya vikundi vyote vya watu.” Tunapotafakari mambo ambayo Yehova ametufanyia, anayotufanyia, na atakayotufanyia, mioyo yetu inachochewa kutangaza utukufu wake!—Zab. 96:1, 3.

2 Katika Huduma Yetu: Mashahidi wa Yehova wana pendeleo la kuitwa kwa jina la Mungu na kulitangaza duniani kote. (Mal. 1:11) Wao ni tofauti kabisa na makasisi wa dini zinazodai kuwa za Kikristo, ambao kwa kiburi huliondoa jina la Mungu katika tafsiri zao za Biblia! Kazi ya kulitangaza jina la Mungu ni ya haraka kwa kuwa lazima watu waliitie jina hilo kwa imani ili waokolewe katika dhiki kuu inayokuja. (Rom. 10:13-15) Isitoshe, amani mbinguni na duniani, hutegemea kutakaswa kwa jina la Mungu. Kwa kweli, kazi zote za Mungu zinahusiana na jina lake.

3 “Yehova ni mkuu na wa kusifiwa sana.” Lakini ili watu ‘wamhesabie Yehova utukufu wa jina lake,’ lazima waujue ukweli kumhusu. (Zab. 96:4, 8) Hata hivyo, watu fulani hudai hakuna Mungu. (Zab. 14:1) Wengine humvunjia heshima kwa kusema kwamba yeye hana nguvu, au kwa kudai kwamba yeye hajihusishi na shughuli za wanadamu. Tunapowasaidia watu wenye mioyo minyoofu kupata ujuzi sahihi kumhusu Muumba, makusudi yake, na utu wake wenye kuvutia, tunamtukuza Yehova.

4 Kwa Mwenendo Wetu: Tunamheshimu Yehova kwa kuishi kupatana na kanuni zake za uadilifu. Watu huona mwenendo wetu mzuri. (1 Pet. 2:12) Kwa mfano, sura yetu safi na nadhifu inaweza kuwachochea wengine watupongeze, na hivyo tunapata fursa ya kuzungumza nao kuhusu manufaa ya kuishi kupatana na kanuni za Neno la Mungu. (1 Tim. 2:9, 10) Tunafurahi kama nini wakati watu wengine ‘wanapoona matendo yetu mazuri na kumpa utukufu Baba yetu aliye mbinguni’!—Mt. 5:16.

5 Na tumsifu Mungu wetu mtukufu kwa neno na tendo kila siku, na hivyo kushiriki kutoa mwito huu wa shangwe: “Mwimbieni Yehova, libarikini jina lake. Tangazeni habari njema za wokovu wake siku baada ya siku.”—Zab. 96:2.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki