Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Mei 15
“Je, ungefurahi kuishi katika hali inayofafanuliwa kwenye mstari huu? [Soma 2 Petro 3:13, kisha umruhusu ajibu.] Gazeti hili linaeleza kuhusu mbingu mpya na dunia mpya. Pia linafafanua jinsi maisha yatakavyokuwa Mungu atakapotimiza kusudi lake kwa dunia.”
Amkeni! Mei
“Watu fulani wanaamini kwamba katika ulimwengu wa leo, unahitaji kuwa mjeuri ili ufanikiwe. Tofauti na hilo, ona pendekezo ambalo Yesu alitoa. [Soma Mathayo 5:5, 9.] Je, unakubaliana na hilo? [Mruhusu ajibu.] Gazeti hili linazungumzia faida tatu za kuwa mtu anayefuatia amani.” Mwonyeshe makala inayoanzia kwenye ukurasa wa 28.
Mnara wa Mlinzi Juni 1
“Hapo zamani, wazee walitendewa kwa heshima katika jamii nyingi, kama sheria hii ya kale inavyosema. [Soma Mambo ya Walawi 19:32.] Je, bado watu wengi wanawaheshimu wazee? [Mruhusu ajibu.] Gazeti hili linaonyesha jinsi Mungu anavyowajali wazee na pia jinsi tunavyoweza kufanya hivyo.”
Amkeni! Juni
“Ugaidi si jambo jipya, lakini leo umekuwa tatizo la ulimwenguni pote nao humwathiri kila mtu. Kwa nini hali iko hivyo? [Mruhusu ajibu.] Toleo hili la Amkeni! linazungumzia ahadi ya Biblia kwamba ugaidi utaisha na jinsi Mungu atakavyoleta amani ya kweli duniani.” Soma Mika 4:4.