Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Mei 15
“Ungejibuje swali hili? [Soma swali kwenye jalada, kisha mruhusu ajibu.] Biblia inatupa sababu ya kuwa na tumaini. [Soma Mathayo 6:9, 10.] Gazeti hili linaeleza jinsi ambavyo Ufalme wa Mungu utafanya mapenzi ya Mungu yatendeke hapa duniani.”
Amkeni! Mei
“Je, unafikiri kwamba tayari Mungu ameamua jinsi matendo yetu na wakati wetu ujao utakavyokuwa? [Mruhusu ajibu.] Kulingana na mstari huu wa Biblia, Mungu anawaruhusu watu wajichagulie jinsi wanavyotaka kuishi. [Soma Kumbukumbu la Torati 30:19.] Makala hii inaonyesha kile ambacho Biblia inasema kuhusiana na jambo hilo.” Zungumzia makala inayoanzia ukurasa wa 12.
Mnara wa Mlinzi Juni 1
“Karibu kila siku tunasikia habari kuhusu wale wanaotenda maovu. [Zungumzia jambo la karibuni linalojulikana katika eneo lenu.] Je, umewahi kujiuliza ikiwa kuna mtu fulani mwovu asiyeonekana anayewachochea watu? [Mruhusu ajibu, kisha usome Ufunuo 12:12.] Gazeti hili linaeleza jinsi tunavyoweza kujilinda.”
Amkeni! Juni
“Ningependa kujua maoni yako kuhusu andiko hili. [Soma 1 Timotheo 6:10.] Je, unafikiri kwamba wale wanaopenda pesa na kufuatia mali wanateseka kweli? [Mruhusu ajibu.] Gazeti hili linazungumzia matokeo mabaya ya kufuatia mali.”