Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 10/06 uku. 1
  • Wewe Unatanguliza Nini?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Wewe Unatanguliza Nini?
  • Huduma ya Ufalme—2006
  • Habari Zinazolingana
  • “Je, Unanipenda Kuliko Hawa?”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2017
  • Je, Tafrija Unayochagua Inakujenga?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Elekezea Sana Fikira Mpango wa Kibinafsi
    Huduma Yetu ya Ufalme—1989
  • Usiruhusu Kitu Chochote Kikutenganishe Na Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
Pata Habari Zaidi
Huduma ya Ufalme—2006
km 10/06 uku. 1

Wewe Unatanguliza Nini?

1 Ungejibuje swali hilo? Bila shaka, sisi sote hutamani kutanguliza mambo ya Ufalme. (Mt. 6:33) Lakini huenda tukajiuliza, ‘Je, mambo ninayochagua kufanya yanaonyesha kwamba ninatanguliza Ufalme?’ Biblia inatutia moyo hivi: “Endeleeni kuthibitisha ninyi wenyewe jinsi mlivyo.” (2 Kor. 13:5) Tunaweza kujithibitishiaje kwamba tunatanguliza Ufalme?

2 Jinsi Unavyotumia Wakati: Tunaweza kuanza kwa kuchunguza jinsi tunavyotumia wakati wetu. (Efe. 5:15, 16) Tunatumia wakati mwingi kadiri gani kila juma pamoja na marafiki, kutazama televisheni, kutumia Intaneti, au kufanya jambo fulani tunalopenda? Tukiandika wakati ambao tunatumia kufanya mambo hayo na tuulinganishe na wakati tunaotumia katika utendaji wa kiroho, huenda tukashangaa. Je, tunatumia wakati mwingi sana kazini bila kujali utumishi mtakatifu ili tu tuwe na pesa za kutosha kwa ajili ya vitu vya bei ghali? Ni mara nyingi kadiri gani tunadhabihu mikutano au mahubiri ili tusafiri katika miisho ya juma kwa ajili ya tafrija?

3 Panga Mambo ya Kutanguliza: Wengi kati yetu hawana wakati wa kutosha kufanya kila jambo wanalotaka. Hivyo, ili kutanguliza mambo ya Ufalme, tunahitaji kuchunguza mambo tunayotanguliza kisha tupange wakati kwa ajili ya “mambo yaliyo ya maana zaidi.” (Flp. 1:10) Mambo hayo yanatia ndani kujifunza Neno la Mungu, kushiriki katika huduma, kutunza familia, na kuhudhuria mikutano ya Kikristo. (Zab. 1:1, 2; Rom. 10:13, 14; 1 Tim. 5:8; Ebr. 10:24, 25) Utendaji mwingine, kama vile mazoezi ya kiasi na tafrija zinazofaa ni muhimu. (Marko 6:31; 1 Tim. 4:8) Lakini mambo hayo yasiyo ya maana sana yanapaswa kuwekwa mahali pake.

4 Ndugu mmoja kijana aliamua kutanguliza mambo ya Ufalme kwa kuwa mtumishi wa wakati wote badala ya kufuatia elimu ya juu ili apate kazi ya kimwili. Alijifunza lugha nyingine na kuhamia eneo lenye uhitaji mkubwa. Alisema: “Ninafurahia maisha kabisa huku. Utumishi unaburudisha sana! Laiti vijana wote wangefanya jambo kama hilo na kupata uradhi. Hakuna jambo bora kuliko kumtumikia Yehova kwa nafsi yote.” Naam, kutanguliza Ufalme hutuletea baraka, lakini, la muhimu zaidi, humfurahisha Baba yetu wa mbinguni, Yehova.—Ebr. 6:10.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki