Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 11/06 uku. 1
  • Wajasiri Lakini Wenye Kufanya Amani

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Wajasiri Lakini Wenye Kufanya Amani
  • Huduma ya Ufalme—2006
  • Habari Zinazolingana
  • “Iweni Wenye Kufanya Amani na Watu Wote”
    Huduma Yetu ya Ufalme—2012
  • Je, Inawezekana Kuwa Mwenye Kufanya Amani?
    Amkeni!—2006
  • ‘Tafuteni Sana Amani na Kuifuatia’
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2001
  • Habari Njema Hizi za Ufalme Tuzihubiri
    Mwimbieni Yehova Sifa
Pata Habari Zaidi
Huduma ya Ufalme—2006
km 11/06 uku. 1

Wajasiri Lakini Wenye Kufanya Amani

1 Watu wengi ambao sisi huwahubiria wana imani ambayo haipatani na ukweli wa Biblia. Ingawa tunapaswa kuhubiri kwa ujasiri, tungependa vilevile ‘kuwa wenye kufanya amani na watu wote’ na kuepuka kuwakasirisha bila sababu. (Rom. 12:18; Mdo. 4:29) Ni katika njia gani tunaweza kuwa na ujasiri lakini wenye kufanya amani tunapohubiri habari za Ufalme?

2 Tafuta Mambo Mnayokubaliana: Mtu mwenye kufanya amani huepuka mabishano. Kupinga bila sababu imani ambayo mwenye nyumba ameshikilia kwa nguvu hakuwezi kumfanya apendezwe. Akisema jambo lisilo sahihi, kwa busara tunaweza kutaja jambo fulani tunalokubaliana. Kwa kukazia mambo tunayokubaliana, huenda tukaondoa hisia fulani zisizofaa na kugusa moyo wake.

3 Tukiachilia maoni fulani yasiyo sahihi ya mwenye nyumba, je, tunaridhiana au kupunguza ukweli? La. Mgawo wetu tukiwa wahudumu Wakristo si kupinga kila jambo lisilo la kweli tunalokutana nalo, bali ni kuhubiri habari njema ya Ufalme wa Mungu. (Mt. 24:14) Mwenye nyumba anapotoa maoni yasiyo sahihi, badala ya kuyachambua mara moja, tunaweza kuona jambo hilo kuwa nafasi ya kufahamu jinsi mtu huyo anavyofikiri.—Met. 16:23.

4 Mheshimu Mwenye Nyumba: Kuna wakati ambapo tunapaswa kuwa na ujasiri tunaposahihisha mafundisho ya uwongo. Hata hivyo, kwa kuwa sisi ni watu wenye kufanya amani, tutaepuka kufanya dhihaka au kutumia maneno yenye kuwavunjia heshima watu wanaoamini au kufundisha makosa. Watu hawapendezwi na mtu anayejiona kuwa bora, lakini tukiwa na mwelekeo wa unyenyekevu na fadhili tunaweza kufungua akili za wanaopenda kweli. Tunapowaheshimu wasikilizaji wetu pamoja na imani yao, itakuwa rahisi kwao kukubali ujumbe wetu.

5 Mtume Paulo alifikiria imani ya wale ambao aliwahubiria na akajaribu kupitisha habari njema katika njia ambayo ingegusa mioyo yao. (Mdo. 17:22-31) Kwa hiari alikuwa ‘mambo yote kwa watu wa namna zote, ili kwa vyovyote awaokoe wengine.’ (1 Kor. 9:22) Sisi pia tunaweza kufanya hivyo kwa kufanya amani tunapohubiri habari njema kwa ujasiri.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki