Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 12/12 uku. 1
  • “Iweni Wenye Kufanya Amani na Watu Wote”

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • “Iweni Wenye Kufanya Amani na Watu Wote”
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2012
  • Habari Zinazolingana
  • Kuboresha Ustadi Wetu Katika Huduma—Kushughulika na Mwenye Nyumba Mwenye Hasira
    Huduma Yetu ya Ufalme—2015
  • Wajasiri Lakini Wenye Kufanya Amani
    Huduma ya Ufalme—2006
  • Msaidie Mwenye Nyumba Kufikiri
    Huduma Yetu ya Ufalme—2011
  • Tumia Ile Kanuni Bora Katika Huduma Yako
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2012
km 12/12 uku. 1

“Iweni Wenye Kufanya Amani na Watu Wote”

1. Tunapaswa kutumia shauri gani la Biblia tunapokutana na wenye nyumba ambao wana hasira?

1 Watu wa Yehova hupenda amani, na tunahubiri kuhusu amani. (Isa. 52:7) Hata hivyo, nyakati nyingine tunakutana na watu ambao hukasirika kwa sababu tumewatembelea nyumbani. Ni nini kitakachotusaidia kuwa wenye kufanya amani katika hali kama hizo?—Rom. 12:18.

2. Kwa nini ni muhimu tuwe na ufahamu?

2 Uwe na Ufahamu: Ijapokuwa baadhi ya watu hukasirika kwa sababu wanapinga kweli, wengine hukasirika kwa sababu tofauti. Labda tumewatembelea wakati usiofaa. Huenda mwenye nyumba akakasirika kwa sababu ya matatizo ya kibinafsi. Hata kama mwenye nyumba amekasirishwa na ujumbe wa habari njema, tunapaswa kukumbuka kwamba huenda ni kwa sababu amepotoshwa. (2 Kor. 4:4) Kuwa na ufahamu kutatusaidia kubaki watulivu na hatutavunjika moyo.—Met. 19:11.

3. Tunawezaje kumwonyesha mwenye nyumba heshima?

3 Heshimu Wengine: Watu wengi katika eneo wana imani zilizotia mizizi. (2 Kor. 10:4) Wana haki ya kuamua ikiwa watatusikiliza au la. Hatungependa kamwe kudharau mambo ambayo mwenye nyumba anaamini au kumfanya ahisi kwamba hajui kitu. Ikiwa anataka tuondoke, kwa heshima tutafanya hivyo.

4. Inamaanisha nini kutumia maneno yenye neema?

4 Tumia Maneno Yenye Neema: Hata ikiwa wanatutukana, jibu letu linapaswa kuwa la upole na lenye neema. (Kol. 4:6; 1 Pet. 2:23) Badala ya kuingia katika mabishano, tujaribu kutafuta jambo ambalo sote tutakubaliana. Labda, kwa fadhili tunaweza kumwomba mwenye nyumba atueleze kwa nini anatupinga. Ili kuepuka kumkasirisha zaidi, nyakati nyingine ni bora kukatiza mazungumzo.—Met. 9:7; 17:14.

5. Kuna faida gani tukiwa wenye kufanya amani katika utumishi?

5 Iwapo tutakuwa wenye kufanya amani, huenda mwenye nyumba akakumbuka jinsi tulivyoitikia na labda atasikiliza wakati mwingine atakapohubiriwa. (Rom. 12:20, 21) Hata kama anaonyesha upinzani mkali, siku moja anaweza kuwa ndugu yetu. (Gal. 1:13, 14) Hata iwe mtu huyo atapendezwa na kweli au la, tutamheshimu Yehova na kulipamba fundisho lake ikiwa tutajidhibiti na tutakuwa wenye kufanya amani.—2 Kor. 6:3.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki