Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 3/07 uku. 4
  • “Ungejibuje?”

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • “Ungejibuje?”
  • Huduma ya Ufalme—2007
  • Habari Zinazolingana
  • Kwa Wasomaji Wetu
    Amkeni!—2006
  • (1) Swali, (2) Andiko, na (3) Sura
    Huduma ya Ufalme—2006
  • Maisha na Huduma ya Yesu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
  • Njia Mpya ya Kuanzisha Mazungumzo
    Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo (2016)
Pata Habari Zaidi
Huduma ya Ufalme—2007
km 3/07 uku. 4

“Ungejibuje?”

1 Ingawa unapenda Neno la Mungu, je, wewe huona ni vigumu kukumbuka mambo fulani katika masimulizi ya Biblia au mahali ambapo maneno fulani hususa yanapatikana katika Maandiko? Je, ungependa watoto wako waelewe kwa usahihi mafundisho na mambo ya msingi katika Biblia? Makala yenye kichwa “Ungejibuje?” inayochapishwa kila mwezi katika ukurasa wa 31 wa Amkeni! inaweza kuwasaidia vijana kwa wazee kuelewa Neno la Mungu vizuri zaidi.—Mdo. 17:11.

2 Unaweza kufaidikaje kikamili kutokana na makala hiyo? Toleo la Januari 2006 la Amkeni! lilikuwa na mapendekezo haya: “Hebu tazama ukurasa wa 31 . . . Sehemu fulani za ukurasa huu zitawavutia wasomaji wachanga; nyingine zitachangamsha akili za watu wenye ujuzi zaidi wa Biblia. Sehemu, ‘Ilitukia Lini?’ itakusaidia uwe na chati ya tarehe inayoonyesha kipindi cha wakati ambacho watu wanaotajwa katika Biblia waliishi na mambo muhimu yaliyotukia wakati huo. Ingawa majibu ya sehemu ‘Kutoka Katika Toleo Hili’ yatapatikana katika gazeti lote, majibu ya mengi ya maswali yatachapishwa yakiwa juu-chini katika ukurasa fulani. Mbona usifanye utafiti fulani kabla ya kusoma majibu hayo kisha uwaeleze wengine yale ambayo umejifunza? Unaweza pia kuzungumzia sehemu hii mpya, ‘Ungejibuje?’ ukiwa na familia yako au na kikundi chochote unachoshirikiana nacho.”

3 Naam, familia nyingi hufurahia kutumia makala hiyo katika funzo lao la familia. Mama mmoja anaandika hivi: “Mimi na mume wangu tuliona inafaa kuzungumzia sehemu yenye kichwa, ‘Watoto Watafute Picha’ katika funzo letu la familia ili limchangamshe na kumfurahisha binti yetu mwenye umri wa miaka mitatu. Sisi hufurahia kumwona akichukua Amkeni! kwa uchangamfu na kufungua kila ukurasa mpaka anapopata picha anayotafuta.” Baba mmoja huko Brazili anasema: “Mimi na mwana wangu mwenye umri wa miaka saba tunapenda sana sehemu hiyo ya Amkeni! Imemsaidia Moises kukaza fikira, kufungua Maandiko, na kuelewa picha na tarehe za matukio.” Ashley, mwenye umri wa miaka minane, anaandika hivi: “Asanteni kwa makala ‘Ungejibuje?’ inayopatikana mwishoni mwa Amkeni! Imenifunza mengi kuhusu Biblia.”

4 Kwa nini msitumie makala “Ungejibuje?” mara kwa mara katika funzo lenu la familia? Mnaweza kutumia Fahirisi au Watchtower Library katika CD-ROM, mahali ambapo inapatikana, ili kutafuta majibu ya baadhi ya yale maswali magumu zaidi. Kwa kufanya hivyo, mtawafundisha watoto wenu kufanya utafiti. Ikiwa mna watoto wakubwa, mnaweza kuwapa mgawo wafanye utafiti kuhusu majibu ya sehemu zenye kichwa, “Mimi Ni Nani?” au “Ilitukia Lini?” kabla ya funzo la familia. Kisha wanaweza kutaja matokeo ya utafiti wao wakati wa funzo. Kutumia ukurasa huo vizuri ni njia moja ambayo wazazi wanaweza kukazia Neno la Mungu katika akili za watoto wao na kuwasaidia kuyajua “maandishi matakatifu” tangu wakiwa wachanga.—2 Tim. 3:15; Kum. 6:7.

[Maswali ya Funzo]

1. Wengi wetu huona ni vigumu kufanya nini?

2. Sehemu zilizo katika makala yenye kichwa “Ungejibuje?” zinaweza kutumiwaje?

3. Familia fulani zimefaidikaje kutokana na makala hiyo, na ni sehemu gani zinazokufurahisha zaidi?

4. Familia inaweza kutumiaje makala hiyo katika funzo la Biblia la familia?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki