Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w85 8/1 uku. 19
  • Maisha na Huduma ya Yesu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Maisha na Huduma ya Yesu
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
  • Habari Zinazolingana
  • “Ungejibuje?”
    Huduma ya Ufalme—2007
  • Kwa Wasomaji Wetu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2008
  • Je, Unalitumia Kikamili?
    Huduma Yetu ya Ufalme—2008
  • Njia Mpya ya Kuanzisha Mazungumzo
    Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo (2016)
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
w85 8/1 uku. 19

Maisha na Huduma ya Yesu

Kuanzia na toleo la gazeti hili, makala mpya yenye kichwa kilicho juu itatokea katika Mnara wa Mlinzi.

KWA miaka mitano hivi iliyopita, Mnara wa Mlinzi umekuwa na makala ya kurasa mbili yenye picha inayoitwa “Neno la Mungu Li Hai.” Kwa picha pamoja na maandishi yaliyo rahisi kusoma, mafundisho mengi ya Biblia na masimulizi ya kihistoria yamezungumzwa kwa njia ya waziwazi, iliyo rahisi kueleweka. Sasa makala mpya, yenye kukazia maisha na huduma ya Yesu Kristo, itachukua mahali pa “Neno la Mungu Li Hai.”

Kwenye kurasa mbili zifuatazo utaona sehemu ya kwanza ya makala hiyo mpya. Kwa miezi kadha ijayo, unaweza kutazamia kupokea habari mpya katika kila toleo la Mnara wa Mlinzi. Mfululizo huu mpya wa makala utakuwa kama ule wa “Neno la Mungu Li Hai” wenye kurasa mbili na wenye picha kubwa-kubwa.

Inafaa kwamba Yesu Kristo azungumzwe kwa njia hiyo katika Mnara wa Mlinzi, kwa maana Yesu amekuwa na uvutano mkubwa zaidi juu ya historia ya wanadamu kuliko mwanadamu mwingine ye yote. Na jambo la maana zaidi ni kwamba maisha ya mamilioni ya watu wa rangi zote na mataifa yote yamebadilishwa kwa njia yenye faida wanapokuja kuthamini maisha na mafundisho yake.

Inaelekea tayari unajua mengi juu ya Yesu na huduma yake. Lakini je, umekaza akilini wakati na mahali pa matukio ili uyahusianishe na kuyakumbuka vizuri zaidi? Kwa mfano, Yesu aliwachagua mitume wake 12 wakati gani​—ni mapema wakati wa huduma yake au ni baadaye zaidi? Je! ilikuwa kabla au baada ya yule mwanamke Msamaria kumtambua kuwa Kristo? Naye alikuwa wapi alipowachagua wale 12, au alipolisha kimuujiza wale 5,000, au alipotoa Mahubiri ya Mlimani? Kwa kuwa makala hii mpya itaeleza hadithi ya maisha na huduma ya Yesu kulingana na wakati mambo yalitokea na kwa kuwa itakuwa na picha na masimulizi, itakusaidia ukaze kikiki zaidi akilini mwako matukio hayo ya maana sana.

Makala hii itasaidia wale ambao ni wasomaji wa Biblia kwa muda mrefu na pia wanafunzi wa Biblia walio wapya zaidi, na itasaidia wazazi wanapojifunza pamoja na watoto wao. Maswali yametolewa kwa ajili ya kusudi hilo. Hii ni njia nzuri kama nini ya kuwafahamisha juu ya mwanzilishi wa Ukristo na mafundisho yake! Huenda ukatangulia kuona njia ambazo unaweza kutumia makala hizi katika kuhudumia jamaa yako na wengine. Kumbuka, karibu kila mtu anapenda hadithi, na wengi wanazifurahia zikiwa zinafuatana na kuhadithiwa visehemu-sehemu vyake kwa vipindi vya ukawaida.

Kwa hiyo, kuanzia na sehemu yake ya kwanza, watie moyo wengine wafuatane na hadithi hii yenye kuendelea. Utaona kwamba mitajo ya Biblia imeandikwa kifupi ili ieleweke kwa urahisi zaidi, na chanzo cha Biblia kikiwa kimetolewa mwishoni mwa kila hadithi. Tia moyo usomaji wa masimulizi hayo ya Biblia. Ndiyo, tumia kwa faida makala hii mpya iliyomo katika Mnara wa Mlinzi katika kazi ya kufanya wanafunzi!

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki