Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Juni 15
“Je, umegundua siku hizi watu wengi wanachagua viwango vyao vya mema na mabaya? [Mruhusu ajibu.] Hapa kuna mfano wa mwongozo usiopitwa na wakati unaopatikana katika Biblia. [Soma Andiko linalopatikana kwenye sanduku katika ukurasa wa 6-7.] Gazeti hili linafafanua jinsi tunavyofaidika kwa kufuata viwango vya maadili vya Biblia.”
Amkeni! Juni
“Sisi sote tunahitaji pesa ili tuishi. Je, unafikiri inawezekana tukasongwa sana na mawazo ya jinsi tunavyoweza kutafuta pesa? [Mruhusu ajibu.] Ona kile ambacho Andiko hili linasema kuhusu kufuatia mali. [Soma 1 Timotheo 6:10.] Gazeti hili linatoa mapendekezo ya jinsi mtu anavyoweza kurahisisha maisha yake na kuendelea akiwa na kiasi kidogo cha pesa.”
Mnara wa Mlinzi Julai 1
“Je, wewe hushangaa kwa nini watu fulani hutendewa vibaya kwa sababu ni wa jamii au taifa tofauti au kwa sababu wanazungumza lugha tofauti? [Mruhusu ajibu.] Ona sababu inayotolewa hapa. [Soma 1 Yohana 4:20.] Gazeti hili linajibu swali hili, Je, amani kati ya jamii mbalimbali inaweza kupatikana?”
Amkeni! Julai
“Tofauti na wanyama wanaoongozwa na silika, wanadamu wana uhuru wa kuchagua wataishi kwa kufuata viwango gani. Unafikiri tunaweza kupata wapi mwongozo unaotegemeka? [Mruhusu ajibu. Kisha soma Zaburi 119:105.] Gazeti hili linafafanua jinsi Biblia ilivyo na mwongozo bora.”