Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 2/08 uku. 1
  • Kukumbuka Fidia kwa Uthamini

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kukumbuka Fidia kwa Uthamini
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2008
  • Habari Zinazolingana
  • “Endeleeni Kufanya Hivi”
    Huduma Yetu ya Ufalme—2012
  • Tufanye Yote Tuwezayo Kuonyesha Uthamini Wetu
    Huduma Yetu ya Ufalme—2011
  • “Endeleeni Kufanya Hivi kwa Kunikumbuka Mimi” Ukumbusho wa Kifo cha Yesu Utakuwa Aprili 2
    Huduma ya Ufalme—2007
  • Mialiko ya Ukumbusho Itakayosambazwa Duniani Kote!
    Huduma Yetu ya Ufalme—2010
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2008
km 2/08 uku. 1

Kukumbuka Fidia kwa Uthamini

1, 2. Tuna sababu gani za kukumbuka fidia kwa uthamini?

1 Kwa kutii amri ya Yesu, Wakristo ulimwenguni pote watakutana Jumamosi, Machi 22, 2008 baada ya jua kushuka ili kukumbuka kifo cha Yesu Kristo. (Luka 22:19; 1 Kor. 11:23-26) Tunachochewa kufanya hivyo kwa sababu tunathamini mambo yote yaliyotimizwa siku hiyo miaka 1,975 iliyopita. Kwa kudumisha utimilifu mkamilifu alipokufa kwa uchungu kwenye mti wa mateso, Yesu alitakasa jina la Baba yake na hivyo kutoa jibu bora zaidi kwa dhihaka za Shetani.—Ayu. 1:11; Met. 27:11.

2 Damu ya Yesu iliyomwagwa ilihalalisha agano jipya na hivyo kuwawezesha wanadamu wasio wakamilifu kufanywa kuwa wana wa Mungu wakiwa na taraja la kutawala na Kristo katika Ufalme wake wa kimbingu. (Yer. 31:31-34; Marko 14:24) Isitoshe, kina cha upendo wa Mungu kwa wanadamu kilionekana waziwazi alipomtoa mwana wake mpendwa awe dhabihu, kama Yesu mwenyewe alivyomweleza Nikodemo.—Yoh. 3:16.

3. Wale wanaohudhuria Ukumbusho watanufaikaje?

3 Wakaribishe Wengine: Toleo la Januari la Huduma Yetu ya Ufalme lilipendekeza uandike orodha ya watu ambao ungependa kuwaalika kisha umwalike kibinafsi kila mmoja wao. Je, umeanza kuwakaribisha wale walio katika orodha yako? Je, unafanya mipango kushiriki kikamili katika kampeni ambayo itaanza Machi 1 ya kuwakaribisha watu kwenye Ukumbusho? Wale wanaohudhuria watapata habari ya Kimaandiko itakayojenga imani yao katika fidia, imani inayoongoza kwenye uzima wa milele.—Rom. 10:17.

4. Kwa nini tufike mapema kwa ajili ya Ukumbusho?

4 Wote wanaoweza wanapaswa kupanga wafike mapema ili wawakaribishe kwa uchangamfu wote wanaokubali mwaliko huo wa pekee. Kwa kuwa hudhurio la Ukumbusho huwa kubwa ni muhimu kuwakazia fikira zaidi wapya na wengine wanaohudhuria mikutano mara kwa mara tu.

5. Unaweza kutayarishaje moyo wako kwa ajili ya tukio hilo?

5 Tayarisha Moyo Wako: Kijitabu Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2008 na Kalenda ya 2008 zina ratiba ya pekee ya usomaji wa Biblia wa Ukumbusho kuanzia Machi 17. Kufikiria matukio muhimu ya siku za mwisho za maisha ya kidunia ya Yesu kutakusaidia kutayarisha moyo wako kwa ajili ya maadhimisho ya Ukumbusho. (Ezra 7:10) Kutafakari kuhusu masimulizi hayo na kusali kutaongeza uthamini wako kwa ajili ya upendo wa Yehova na Mwana wake katika kuandaa fidia.—Zab. 143:5.

6. Kusitawisha uthamini kwa ajili ya fidia kunaweza kutunufaishaje?

6 Ukumbusho unapokaribia, na tujitayarishe na kuwatayarisha wengine vizuri kwa ajili ya tukio hilo muhimu. Kukumbuka fidia kwa uthamini kutaimarisha uhusiano wetu na Yehova na Mwana wake. (2 Kor. 5:14, 15) Pia kutatuchochea tuwaige katika kuwaonyesha wengine upendo wa kujidhabihu.—1 Yoh. 4:11.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki