Ratiba ya Mkutano Wa Utumishi
Juma Linaloanza Februari 11
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Ukitumia mapendekezo kwenye ukurasa wa 10 au utoaji mwingine unaofaa eneo lenu, toa maonyesho ya jinsi ya kutoa Mnara wa Mlinzi la Januari 1 na Amkeni! la Januari.
Dak. 15: Je, Unaweza Kutumikia Mahali Penye Uhitaji Mkubwa Zaidi? Hotuba na mazungumzo na wasikilizaji yakitegemea Mnara wa Mlinzi la Julai 15, 2003, ukurasa wa 20. Tia ndani maelezo katika kitabu Tengenezo, ukurasa wa 111, fungu la 1, hadi ukurasa wa 112, fungu la 1. Wahoji kwa ufupi wowote ambao wamehamia mahali penye uhitaji mkubwa zaidi. Walikabili magumu gani, nao walikabilianaje nayo? Walipata baraka gani?
Dak. 20: Wasaidie Wapya Wawe Wahudumu Wenye Maendeleo. Baada ya utangulizi usiozidi dakika moja, zungumzia Mnara wa Mlinzi la Desemba 1, 2005, ukurasa wa 31, kwa maswali na majibu ukitumia maswali ya funzo yaliyoonyeshwa. Baada ya kuzungumzia fungu la 18, panga kuwe na onyesho la mwenye nyumba akimtolea kipingamizi mhubiri mpya ambaye anahubiri na mhubiri mwenye uzoefu. Jibu la mhubiri mpya halina mafanikio naye mwenye nyumba anakatiza mazungumzo hayo. Wanapotoka kwenye nyumba hiyo, mhubiri mwenye uzoefu anampongeza mhubiri mpya kwa uchangamfu kuhusu jitihada zake kisha anamwonyesha jinsi wakati ujao anavyoweza kutumia kitabu Kutoa Sababu kujibu kizuia-mazungumzo hicho.
Juma Linaloanza Februari 18
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyoteuliwa katika Huduma Yetu ya Ufalme.
Dak. 10: “Ripoti ya Ujenzi wa Ofisi ya Tawi ya Tanzania.” Mazungumzo na wasikilizaji.
Dak. 25: “Ushuhuda wa Imani!”a Ishughulikiwe na mwangalizi wa utumishi. Malizia kwa kupitia mambo mazuri ambayo kutaniko lilitimiza katika mwaka wa utumishi uliopita.
Juma Linaloanza Februari 25
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Wakumbushe wahubiri watoe ripoti ya utumishi ya Februari. Soma ripoti ya hesabu na taarifa ya shukrani. Toa onyesho la jinsi ya kutumia mwaliko wa Ukumbusho kumkaribisha mshiriki wa familia au jirani.
Dak. 20: “Kukumbuka Fidia kwa Uthamini”b Kadiri wakati unavyoruhusu, waombe wasikilizaji watoe maelezo kuhusu maandiko yaliyotajwa.
Dak. 15: Jitayarishe Kutoa Magazeti ya Karibuni. Mazungumzo na wasikilizaji. Baada ya kutaja mambo machache katika Mnara wa Mlinzi la Februari 1 na Amkeni! la Februari, waulize wasikilizaji ni makala gani inayoweza kuwavutia watu katika eneo lenu na kwa nini. Waombe wasikilizaji wataje mambo hususa katika gazeti hilo ambayo wamepanga kutumia. Ni swali gani watakalouliza ili kuanzisha mazungumzo? Watasoma andiko gani kutoka kwenye makala? Ukitumia mapendekezo yaliyotajwa na wasikilizaji au yaliyoonyeshwa katika Huduma Yetu ya Ufalme, onyesha jinsi ya kutoa Mnara wa Mlinzi la Februari 1 na Amkeni! la Februari.
Juma Linaloanza Machi 3
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Pitia mambo makuu katika sanduku “Mambo ya Kukumbuka Wakati wa Ukumbusho.”
Dak. 20: Je, Unaweza Kuanzisha Funzo la Biblia Mwezi wa Machi? Mazungumzo na wasikilizaji. Mwezi wa Machi tutatoa kitabu Biblia Inafundisha tukiwa na lengo la kuanzisha mafunzo ya Biblia. Pitia mambo fulani katika kitabu hicho. Zungumzia jinsi kinavyoweza kutolewa tunapomrudia mtu aliyependezwa tulipomwachia mwaliko wa Ukumbusho, tunaporudi tulipoacha gazeti, na tunapotoa kitabu hicho nyumba kwa nyumba baada ya Machi 22. (Ona km 4/07 uku. 3; km 3/06 uku. 1, fu. 3; km 1/06 uku. 3-6.) Fanya onyesho la pendekezo mmoja au mawili.
Dak. 15: Tumia Biblia Kujibu Maswali. Hotuba na mazungumzo na wasikilizaji yakitegemea kitabu Shule ya Huduma, ukurasa wa 143-144. Tia ndani onyesho fupi la mhubiri akiulizwa swali ambalo watu wengi huuliza katika eneo lenu kisha anatumia Biblia kujibu.
[Maelezo ya Chini]
a Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendeleze mazungumzo kwa maswali na majibu.
b Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendeleze mazungumzo kwa maswali na majibu.