Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 2/08 uku. 2
  • Ratiba ya Mkutano Wa Utumishi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ratiba ya Mkutano Wa Utumishi
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2008
  • Vichwa vidogo
  • Juma Linaloanza Februari 11
  • Juma Linaloanza Februari 18
  • Juma Linaloanza Februari 25
  • Juma Linaloanza Machi 3
Huduma Yetu ya Ufalme—2008
km 2/08 uku. 2

Ratiba ya Mkutano Wa Utumishi

Juma Linaloanza Februari 11

Wimbo 168

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Ukitumia mapendekezo kwenye ukurasa wa 10 au utoaji mwingine unaofaa eneo lenu, toa maonyesho ya jinsi ya kutoa Mnara wa Mlinzi la Januari 1 na Amkeni! la Januari.

Dak. 15: Je, Unaweza Kutumikia Mahali Penye Uhitaji Mkubwa Zaidi? Hotuba na mazungumzo na wasikilizaji yakitegemea Mnara wa Mlinzi la Julai 15, 2003, ukurasa wa 20. Tia ndani maelezo katika kitabu Tengenezo, ukurasa wa 111, fungu la 1, hadi ukurasa wa 112, fungu la 1. Wahoji kwa ufupi wowote ambao wamehamia mahali penye uhitaji mkubwa zaidi. Walikabili magumu gani, nao walikabilianaje nayo? Walipata baraka gani?

Dak. 20: Wasaidie Wapya Wawe Wahudumu Wenye Maendeleo. Baada ya utangulizi usiozidi dakika moja, zungumzia Mnara wa Mlinzi la Desemba 1, 2005, ukurasa wa 31, kwa maswali na majibu ukitumia maswali ya funzo yaliyoonyeshwa. Baada ya kuzungumzia fungu la 18, panga kuwe na onyesho la mwenye nyumba akimtolea kipingamizi mhubiri mpya ambaye anahubiri na mhubiri mwenye uzoefu. Jibu la mhubiri mpya halina mafanikio naye mwenye nyumba anakatiza mazungumzo hayo. Wanapotoka kwenye nyumba hiyo, mhubiri mwenye uzoefu anampongeza mhubiri mpya kwa uchangamfu kuhusu jitihada zake kisha anamwonyesha jinsi wakati ujao anavyoweza kutumia kitabu Kutoa Sababu kujibu kizuia-mazungumzo hicho.

Wimbo 50

Juma Linaloanza Februari 18

Wimbo 17

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyoteuliwa katika Huduma Yetu ya Ufalme.

Dak. 10: “Ripoti ya Ujenzi wa Ofisi ya Tawi ya Tanzania.” Mazungumzo na wasikilizaji.

Dak. 25: “Ushuhuda wa Imani!”a Ishughulikiwe na mwangalizi wa utumishi. Malizia kwa kupitia mambo mazuri ambayo kutaniko lilitimiza katika mwaka wa utumishi uliopita.

Wimbo 194

Juma Linaloanza Februari 25

Wimbo 81

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Wakumbushe wahubiri watoe ripoti ya utumishi ya Februari. Soma ripoti ya hesabu na taarifa ya shukrani. Toa onyesho la jinsi ya kutumia mwaliko wa Ukumbusho kumkaribisha mshiriki wa familia au jirani.

Dak. 20: “Kukumbuka Fidia kwa Uthamini”b Kadiri wakati unavyoruhusu, waombe wasikilizaji watoe maelezo kuhusu maandiko yaliyotajwa.

Dak. 15: Jitayarishe Kutoa Magazeti ya Karibuni. Mazungumzo na wasikilizaji. Baada ya kutaja mambo machache katika Mnara wa Mlinzi la Februari 1 na Amkeni! la Februari, waulize wasikilizaji ni makala gani inayoweza kuwavutia watu katika eneo lenu na kwa nini. Waombe wasikilizaji wataje mambo hususa katika gazeti hilo ambayo wamepanga kutumia. Ni swali gani watakalouliza ili kuanzisha mazungumzo? Watasoma andiko gani kutoka kwenye makala? Ukitumia mapendekezo yaliyotajwa na wasikilizaji au yaliyoonyeshwa katika Huduma Yetu ya Ufalme, onyesha jinsi ya kutoa Mnara wa Mlinzi la Februari 1 na Amkeni! la Februari.

Wimbo 119

Juma Linaloanza Machi 3

Wimbo 223

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Pitia mambo makuu katika sanduku “Mambo ya Kukumbuka Wakati wa Ukumbusho.”

Dak. 20: Je, Unaweza Kuanzisha Funzo la Biblia Mwezi wa Machi? Mazungumzo na wasikilizaji. Mwezi wa Machi tutatoa kitabu Biblia Inafundisha tukiwa na lengo la kuanzisha mafunzo ya Biblia. Pitia mambo fulani katika kitabu hicho. Zungumzia jinsi kinavyoweza kutolewa tunapomrudia mtu aliyependezwa tulipomwachia mwaliko wa Ukumbusho, tunaporudi tulipoacha gazeti, na tunapotoa kitabu hicho nyumba kwa nyumba baada ya Machi 22. (Ona km 4/07 uku. 3; km 3/06 uku. 1, fu. 3; km 1/06 uku. 3-6.) Fanya onyesho la pendekezo mmoja au mawili.

Dak. 15: Tumia Biblia Kujibu Maswali. Hotuba na mazungumzo na wasikilizaji yakitegemea kitabu Shule ya Huduma, ukurasa wa 143-144. Tia ndani onyesho fupi la mhubiri akiulizwa swali ambalo watu wengi huuliza katika eneo lenu kisha anatumia Biblia kujibu.

Wimbo 145

[Maelezo ya Chini]

a Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendeleze mazungumzo kwa maswali na majibu.

b Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendeleze mazungumzo kwa maswali na majibu.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki