Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 4/08 uku. 4
  • Sanduku la Swali

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Sanduku la Swali
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2008
  • Habari Zinazolingana
  • Wako Peke Yao Lakini Hawajasahauliwa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2008
  • Utunzaji wa Wazee-Wazee Tatizo Lenye Kukua
    Amkeni!—1991
  • Je! Wewe Uko Tayari Kukabili Hali Ngumu ya Kitiba Yenye Kujaribu Imani?
    Huduma Yetu ya Ufalme—1990
  • Fungu Muhimu la Wauguzi
    Amkeni!—2000
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2008
km 4/08 uku. 4

Sanduku la Swali

◼ Je, ni sawa kwa Shahidi wa Yehova kutibiwa au kuhudumiwa katika makao ya kuwatunzia wagonjwa au hospitali inayoendeshwa na shirika la kidini?

Mashirika mbalimbali ya kidini yanaendesha makao ya kuwatunzia wagonjwa au hospitali ambazo zinatoa matibabu au kuwatunza watu wenye magonjwa ya kudumu. Kwa kawaida, hospitali hizo hazianzishwi ili kuendeleza tu masilahi ya Babiloni Mkubwa. (Ufu. 18:2, 4) Huenda mwanzoni zilianzishwa na mashirika ya kidini ili kuchuma fedha. Leo, hospitali fulani ni za kidini kwa jina tu, hata hivyo, baadhi ya wafanyakazi katika hospitali nyingine ni makasisi.

Ikiwa Shahidi wa Yehova anataka kuhudumiwa katika hospitali au makao fulani ya kuwatunzia wagonjwa, ni lazima afanye uamuzi wa kibinafsi ikiwa ataenda kwenye hospitali ambayo huenda inahusiana na shirika la kidini. Dhamiri yake inaweza kumruhusu kwenda katika hospitali hizo, lakini huenda dhamiri ya mwingine isimruhusu kwenda huko. (1 Tim. 1:5) Kuna hali fulani ambazo zinaweza kumwongoza mtu kufanya uamuzi, na inafaa kuzifikiria.

Kwa mfano, huenda eneo hilo halina hospitali nyingine yoyote isipokuwa hospitali au makao ya kuwatunzia wagonjwa yenye jina la kidini. Au huenda hospitali hiyo ya kidini inapendwa kwa sababu inatoa huduma bora zaidi kuliko hospitali nyingine iliyo karibu. Huenda matibabu unayohitaji yanaweza kupatikana tu katika hospitali hiyo yenye jina la kidini, au huenda daktari wako au daktari fulani wa upasuaji anaruhusiwa kuwahudumia wagonjwa katika hospitali hiyo tu. Pia, nyakati nyingine huenda hospitali za kidini zikaheshimu maoni yako ya Kikristo kuhusiana na matumizi ya damu, lakini huenda hospitali fulani za kibinafsi au za serikali zisiheshimu maoni yako. Kwa hiyo, hayo ndiyo baadhi ya mambo ambayo huenda ukahitaji kufikiria unapochagua hospitali.

Ukiamua kwenda katika makao ya kuwatunzia wagonjwa au hospitali ya kidini, huenda ukaona malipo unayotoa kuwa malipo kwa ajili ya huduma unazopata. Huenda ukaiona hospitali hiyo kama shirika la kidini linaloendesha biashara fulani, na unapohudumiwa hutakuwa ukitoa mchango wa hiari ili kuunga mkono dini ya uwongo. Utakuwa ukilipia tu bidhaa au huduma uliyopata.

Bila shaka, katika hali kama hizo, utahakikisha kwamba ukiwa Mkristo hushiriki katika matendo yoyote ya ibada ya uwongo. Pia, hutawaita wafanyakazi au watu wanaotembelea hospitali hiyo kwa majina ya kawaida ya vyeo vya kidini kama vile “Baba” au “Sista.” (Mt. 23:9) Utahitaji kuhakikisha kwamba shughuli zilizokupeleka huko ni kama za kibiashara tu, yaani, unapata matibabu na huduma fulani, na hazihusishi jambo lingine lolote.

Unapolazwa hospitalini, unaweza kutaja kwamba wewe ni Shahidi wa Yehova na ungependa kutembelewa na wazee wa kutaniko lenu. Hilo litahakikisha kwamba unapata utegemezo unaofaa wa kiroho ukiwa hospitalini.—1 The. 5:14.

Washiriki wa familia ambao ni Mashahidi, wazee wa kutaniko, na washiriki wengine wa kutaniko wanapaswa kuchukua kwa uzito wajibu wa kutimiza mahitaji ya kiroho ya ndugu na dada yeyote aliyezeeka ambaye anatunzwa katika makao ya kuwatunzia waliozeeka, hasa yale yanayoendeshwa na mashirika ya kidini. Jitihada hizo zitawatia moyo sana ndugu na dada hao waliozeeka na kuwalinda ili wasishirikishwe kimakosa katika ibada, sherehe, au shughuli nyingine za kidini zinazofanywa katika makao hayo.

Tukiwa na hayo akilini, kila mmoja wetu atahitaji kufikiria hali zote zinazohusika kisha afanye uamuzi wake binafsi anapochagua hospitali au makao ya kuwatunzia wagonjwa.—Gal. 6:5.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki