Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Juni 1
“Unafikiri Mungu anakubali dini zote? [Mruhusu ajibu.] Ona jinsi Mungu alivyotenda Waisraeli wa kale walipofuata mazoea ya kidini ya mataifa jirani. [Soma Ezekieli 6:6.] Makala hii inajibu swali hili, ‘Je, Kuna Njia Fulani Hususa Tunayopaswa Kumtumikia Mungu?’” Zungumzia makala inayoanza kwenye ukurasa wa 9.
Amkeni! Juni
“Bila shaka utakubali kwamba miaka ya ujana ni migumu hasa kwa vijana na wazazi wao pia. Unafikiri shauri hili linaweza kuwasaidia wazazi? [Soma Yakobo 1:19. Kisha mruhusu ajibu.] Utafurahia mapendekezo kutoka katika Biblia yanayopatikana katika gazeti hili.”
Mnara wa Mlinzi Julai 1
“Sisi sote huumia wakati watu tunaowapenda wanapokufa. Unafikiri Biblia inaweza kusaidia katika hali kama hiyo? [Mruhusu ajibu. Kisha soma Zaburi 55:22.] Gazeti hili linaonyesha baadhi ya hoja fulani kutoka katika Biblia zinazoweza kusaidia.”
Amkeni! Julai
“Watu waliofunga ndoa wanazidi kupata mikazo, na ndoa nyingi zinavunjika. Unafikiri kufuata shauri hili kutasaidia ndoa ifanikiwe? [Soma Methali 12:18. Kisha mruhusu ajibu.] Gazeti hili linazungumzia kanuni nyingine za Biblia zinazoweza kuwasaidia wenzi wa ndoa kuboresha uhusiano wao.”