Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 12/08 uku. 1
  • Kazi ya Kuhubiri Inahitaji Uvumilivu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kazi ya Kuhubiri Inahitaji Uvumilivu
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2008
  • Habari Zinazolingana
  • Shikamana na Tengenezo la Yehova
    Tengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova
  • “Acheni Uvumilivu Ukamilishe Kazi Yake”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2016
  • Uvumilivu—Muhimu kwa Wakristo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1993
  • Uvumilivu
    Ufahamu wa Kina wa Maandiko
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2008
km 12/08 uku. 1

Kazi ya Kuhubiri Inahitaji Uvumilivu

1 Kwa miaka zaidi ya 30, mtume Paulo alifurahia kazi yenye kuridhisha ya kueneza injili. Kama kazi nyingine zenye kuridhisha, kazi yake ya kuhubiri ilikuwa pia na matatizo fulani. (2 Kor. 11:23-29) Hata hivyo, Paulo hakufa moyo. (2 Kor. 4:1) Alielewa kwamba Yehova ndiye angempa nguvu za kuvumilia anapotimiza huduma yake. (Flp. 4:13) Kwa sababu ya mfano wake wa kuvumilia kwa uaminifu, Paulo alisema hivi: “Iweni waigaji wangu, kama vile mimi nilivyo mwigaji wa Kristo.”—1 Kor. 11:1.

2 Kuvumilia Majaribu Leo: Kila siku, ndugu zetu wengi wanadhihakiwa, wanapingwa, au kudharauliwa na washiriki wa familia zao, wafanyakazi, au wanashule wenzao. (Mt. 10:35; Yoh. 15:20) Huenda unakabili hali kama hizo. Au huenda una matatizo ya afya, au unapambana kila siku na mambo yanayokengeusha fikira na vishawishi vinavyojaribu imani na uvumilivu wako. Tunaweza kuimarishwa kwa kuchunguza mifano ya watumishi waaminifu wa zamani na pia Wakristo wenzetu leo ambao wamekabili na kushinda matatizo mbalimbali.—1 Pet. 5:9.

3 Tunaweza kupata nguvu za kubaki thabiti katika huduma yetu kwa kuhakikisha kwamba ‘tumevaa mavazi kamili ya silaha kutoka kwa Mungu.’ (Efe. 6:10-13, 15) Ni muhimu pia kusali ili tuweze kuvumilia. Mungu anatupa roho yake takatifu ili kutusaidia kuvumilia majaribu. (2 Kor. 6:4-7) Ili tufanikiwe katika vita vyetu vya kiroho, ni lazima tutii vikumbusho vya Mungu vya kuichochea upya roho yetu. (Zab. 119:24, 85-88) Kama vile mtoto anavyoweza kusoma tena na tena barua aliyoandikiwa na baba yake mwenye upendo, kusoma Biblia kila siku kunaimarisha uhusiano wetu na Yehova. Kupitia funzo la kibinafsi linalofanywa kwa ukawaida, tunapata hekima ya kukabiliana na majaribu, na hivyo tunaruhusu maoni ya Mungu yatuongoze tunapofanya maamuzi na hilo linaimarisha utimilifu wetu.—Met. 2:10, 11.

4 Uvumilivu Huleta Baraka: Tukivumilia kwa uaminifu kama Paulo huku tukitimiza huduma yetu, tutaufanya moyo wa Yehova ushangilie na tutapata baraka na kuwasaidia wengine pia kupata baraka. (Met. 27:11) Na tuazimie kuvumilia katika huduma, na hivyo kuthibitisha kwamba imani yetu inadumu na ina “thamani kubwa zaidi kuliko dhahabu ambayo huharibika ijapokuwa hiyo hujaribiwa kwa moto.”—1 Pet. 1:6, 7.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki