Kalenda ya 2011 Inakazia Ibada ya Familia
Kalenda ya 2011 ya Mashahidi wa Yehova ina kichwa, Ibada ya Familia. Kalenda hiyo inaonyesha familia za kisasa na familia za nyakati za Biblia. Pia inaonyesha watumishi wa Yehova ambao wamefunga ndoa na walio waseja wakijifunza Biblia.
Watu wanaotajwa katika Biblia ambao wanaonyeshwa katika kalenda walipenda sheria ya Yehova, na hilo liliwasaidia kukabiliana na matatizo mbalimbali yaliyowakumba. (Zab. 1:2, 3) Tunapochunguza kila picha, tutakumbushwa umuhimu wa Ibada ya Familia, iwe tuko katika familia kubwa au ndogo, iwe wote katika familia ni washiriki wa kutaniko au la. Nafasi ya kuandika siku ambayo familia yenu imetenga kwa ajili ya Ibada ya Familia imeandaliwa. Je, umeijaza?