Njia Moja ya Kutumia Broshua Ujumbe wa Biblia
Watu wengi katika eneo letu, hasa washiriki wa dini zisizo za Kikristo, hawafahamu kabisa yaliyomo katika Biblia. Wanapojifunza kitabu Biblia Inafundisha na watu kama hao, wahubiri fulani wametumia broshua Ujumbe wa Biblia ili kumsaidia mwanafunzi ajue yaliyomo katika Biblia. Kwa mfano, ndugu mmoja huanza kwa kupitia sehemu ya 1 ya broshua hiyo anapozungumzia sura ya 3 ya kitabu Biblia Inafundisha. Baada ya hapo na kuendelea, yeye hupitia sehemu nyingine baada ya kila kipindi cha funzo. Je, unajifunza na mtu ambaye anaifahamu Biblia kidogo tu au hata hajui chochote kuihusu? Ili kumsaidia ajifunze ‘maandishi matakatifu, ambayo yanaweza kumfanya awe mwenye hekima kwa ajili ya wokovu,’ unaweza kuongezea habari zilizo kwenye broshua Ujumbe wa Biblia kwenye mambo mnayojifunza katika kitabu, Biblia Inafundisha.—2 Tim. 3:15.