Mapendekezo kwa Ajili ya Utumishi
Kuanzisha Mafunzo ya Biblia Katika Jumamosi ya Kwanza Mwezi wa Septemba
“Watu wengi wanaamini kuna malaika. Je, wewe unaamini hivyo? [Mruhusu ajibu.] Kwa kuwa malaika ni viumbe wa roho, wana nguvu sana, lakini je, unafikiri wanaweza kutusaidia? Biblia inatueleza jinsi malaika wanavyowasaidia wanadamu leo.” Mwonyeshe ukurasa wa nyuma wa gazeti la Mnara wa Mlinzi la Septemba 1, na mzungumzie pamoja habari iliyo chini ya swali la kwanza na angalau andiko moja lililoonyeshwa. Mwachie magazeti na ufanye mpango wa kurudi ili mzungumzie swali linalofuata.
Mnara Wa Mlinzi Septemba 1
“Je, unafikiri wanadamu wataiharibu dunia kabisa? [Mruhusu ajibu.] Ingawa wanadamu hawawezi kurekebisha uharibifu waliofanya, Biblia inasema kwamba Mungu anaweza na anatamani kurekebisha dunia. Andiko la Zaburi 65:9 linatuhakikishia jambo hilo. [Soma.] Toleo hili la Mnara wa Mlinzi linazungumzia jinsi Mungu atakavyorekebisha dunia na jinsi ambavyo tunaweza kufurahia baraka hizo za wakati ujao. Je, ungependa kulisoma?”
Amkeni Septemba
“Watu wengi wanahisi kwamba wanalazimishwa na waajiri wao kufanya kazi kupita kiasi, na hawaoni njia ya kuepuka shinikizo linalotokana na kazi zao. Wataalamu wanasema kwamba kufanya kazi kupita kiasi kunaweza kumfanya mtu apate uchovu unaoweza kumsababishia madhara ya mwili na hisia. Unafikiri ni jambo gani linaloweza kumsaidia mtu aepuke hali ya kuchoka kupita kiasi? [Mruhusu ajibu.] Ona andiko hili lenye kuchochea fikira. [Soma Mhubiri 4:6.] Gazeti hili linaelezea njia nne tunazoweza kutumia ili kuamua mambo tunayopaswa kutanguliza na jinsi ya kukabiliana na uchovu unaopita kiasi kazini.”