“Hapatikani Tena Nyumbani!”
Je, umewahi kusema maneno hayo kuhusu mtu fulani aliyependezwa? Labda umemtembelea mtu aliyependezwa tena na tena lakini hujafaulu kutia maji mbegu ya kweli uliyopanda. (1 Kor. 3:6) Nyakati nyingine, wahubiri wenye uzoefu humwandikia barua au huacha ujumbe chini ya mlango wa mtu ambaye hawajampata nyumbani. Kwa sababu wanajua kwamba huenda ikawa vigumu kumpata tena mtu nyumbani, wahubiri fulani humwomba mwenye nyumba namba ya simu, labda kwa kumwuliza hivi: “Je, unapenda kuwasiliana kwa kutumia ujumbe mfupi?” Ikiwa tunamhubiria mtu tena kupitia barua, barua pepe, kumpigia simu, kumwandikia ujumbe mfupi wa simu, au kumwachia ujumbe mlangoni, tunaweza kuripoti ziara ya kurudia. Hata kama mwenye nyumba anapatikana nyumbani mara chache, bado tunaweza kukuza upendezi wake.