Kifaa Kipya cha Kufanyia Utafiti
Mamilioni ya wahubiri ulimwenguni pote wanatumia Fahirisi ili kufanya utafiti. Hata hivyo, kwa kuwa ina habari nyingi, inapatikana katika lugha chache tu. Kwa hiyo, Mwongozo wa Utafiti wa Mashahidi wa Yehova umetayarishwa katika lugha 170. Machapisho yanayorejelewa katika Mwongozo wa Utafiti ni ya kuanzia hasa mwaka wa 2000 na kuendelea. Mwongozo wa Utafiti haujachapishwa katika lugha ambazo tayari zina Fahirisi lakini unapatikana katika mfumo wa kielektroniki kwenye Watchtower Library na Watchtower—MAKTABA KWENYE MTANDAO. Mwongozo wa Utafiti utakusaidia kupata majibu ya maswali ya Biblia, kutafuta habari kuhusu mahangaiko yako, na kujitayarisha kwa ajili ya mikutano ya kutaniko na ibada ya familia.