Kumhubiria habari njema mchumaji-chai nchini Kamerun
Mapendekezo kwa Ajili ya Utumishi
MNARA WA MLINZI
Swali: Je, hukubali kwamba ikiwa Biblia ni kitabu kutoka kwa Mungu, inaweza kuokoka jaribio lolote la kuiangamiza?
Andiko: Isa 40:8
Pendekezo: Makala zilizo katika gazeti hili zinazungumzia jinsi ambavyo Biblia imeokoka.
MNARA WA MLINZI (ukurasa wa nyuma)
Swali: Ningependa kujua maoni yako kuhusu swali hili. [Soma swali la kwanza kwenye ukurasa wa 16.] Watu fulani wanaamini kwamba dini ilianzishwa na wanadamu. Wengine wanafikiri kwamba Mungu hutumia dini ili kutufanya tumkaribie. Wewe una maoni gani?
Andiko: Yak 1:27
Pendekezo: Makala hii inaeleza zaidi kuhusu kile ambacho Biblia inasema. Nitafurahi kurudi tena ili tuzungumzie mambo fulani katika makala hii.
HABARI NJEMA KUTOKA KWA MUNGU!
Swali: Watu wengi wanahisi kwamba kusoma unabii wa Biblia ni kama kusoma gazeti. Wewe umejionea au umesikia kuhusu jambo gani kati ya haya yaliyotabiriwa?
Andiko: 2Ti 3:1-5
Pendekezo: Broshua hii inaeleza kwa nini hali hizo ni habari njema kwa watu wanaompenda Mungu. [Zungumzia somo la 1, swali la 2.]
ANDIKA UTANGULIZI WAKO
Ukitumia mpangilio ulioonyeshwa katika mifano iliyotangulia tayarisha utangulizi wako kwa ajili ya utumishi.