Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • mwb17 Aprili uku. 2
  • Wakaribishe kwa Uchangamfu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Wakaribishe kwa Uchangamfu
  • Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2017
  • Habari Zinazolingana
  • Wafanye Wahisi Wamekaribishwa Kwenye Ukumbusho
    Huduma Yetu ya Ufalme—1994
  • Ushahidi Mkubwa Utatolewa
    Huduma Yetu ya Ufalme—2011
  • Kuwasaidia Wote Ambao Wameonyesha Kupendezwa
    Huduma Yetu ya Ufalme—1993
  • Karibisha Wageni
    Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo (2016)
Pata Habari Zaidi
Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2017
mwb17 Aprili uku. 2

MAISHA YA MKRISTO

Wakaribishe kwa Uchangamfu

Uwakaribishe nani kwa uchangamfu? Watu wote wanaohudhuria mikutano ya Kikristo, iwe ni mara yao ya kwanza au ni marafiki wa muda mrefu. (Ro 15:7; Ebr 13:2) Inawezekana ni mwabudu mwenzetu ambaye ametutembelea kutoka nchi nyingine au ni Mkristo asiyetenda ambaye amehudhuria mkutano kwa mara ya kwanza baada ya miaka mingi kupita. Wazia jinsi ambavyo ungehisi ikiwa ungekuwa katika hali kama yake. Je, usingethamini kusalimiwa kwa uchangamfu? (Mt 7:12) Kwa hiyo, kwa nini usijitahidi kuzunguka ndani ya Jumba la Ufalme ukiwasalimu watu kabla na baada ya mikutano? Hilo litachangia uchangamfu na upendo kutanikoni na litamtukuza Yehova. (Mt 5:16) Ni wazi kwamba huenda isiwezekane kuzungumza kibinafsi na kila mtu aliyehudhuria. Hata hivyo, kila mtu atahisi amekaribishwa kwa upendo ikiwa sisi sote tutatimiza sehemu yetu.a

Ukarimu wa kweli hauonyeshwi tu katika pindi za pekee kama vile wakati wa ukumbusho bali nyakati zote. Wageni wanapojionea upendo wa Kikristo, watachochewa kumsifu Mungu na kujiunga nasi katika ibada ya kweli.—Yoh 13:35.

a Kanuni za Biblia zinatuzuia tusishirikiane na watu waliotengwa au kujitenga na ushirika ambao huenda wakahudhuria mikutano.—1Ko 5:11; 2Yo 10.

Ndugu akimkaribisha mgeni kwenye Jumba la Ufalme

MAPENDEKEZO YA KUMSAIDIA MGENI

  • Jitambulishe na umwulize jina lake

  • Mkaribishe mkae pamoja

  • Tumia pamoja naye Biblia yako na kitabu chako cha nyimbo

  • Baada ya mkutano, uwe tayari kujibu maswali atakayouliza

  • Kama itafaa mwombe ujifunze naye Biblia

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki