Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • mwb17 Aprili uku. 5
  • Unaweza Kumtia Moyo Mkristo Asiyetenda

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Unaweza Kumtia Moyo Mkristo Asiyetenda
  • Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2017
  • Habari Zinazolingana
  • Usiwasahau Wasiotenda
    Huduma ya Ufalme—2007
  • “Nirudieni”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2020
  • Wasaidieni Warudi Haraka!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2008
  • Wasaidieni Kondoo Waliopotea
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2008
Pata Habari Zaidi
Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2017
mwb17 Aprili uku. 5

MAISHA YA MKRISTO

APRILI 10-16 Unaweza Kumtia Moyo Mkristo Asiyetenda

Mchungaji akijaribu kumwokoa kondoo aliyepotea

Kila mwaka, Wakristo wengi wasiotenda huhudhuria Ukumbusho. Walianza kukimbia mbio za uzima lakini wakarudi nyuma kwa sababu mbalimbali. Baadhi ya sababu hizo zimezungumziwa katika broshua Mrudie Yehova. (Ebr 12:1) Hata hivyo, wale wasiotenda bado wana thamani machoni pa Yehova, ambaye aliwanunua kwa damu ya Mwana wake. (Mdo 20:28; 1Pe 1:18, 19) Tunaweza kuwasaidiaje warudi kutanikoni?

Wazee wa kutaniko wanajitahidi kuwatafuta na kuwasaidia Wakristo wasiotenda kama tu mchungaji anavyowatafuta kwa bidii kondoo ambao wamepotea. (Lu 15:4-7) Jambo hilo linaonyesha utunzaji wenye upendo wa Yehova. (Yer 23:3, 4) Sisi sote tunaweza kuwatia moyo wasiotenda, si wazee tu. Jitihada zetu za kuonyesha fadhili na hisia-mwenzi zinampendeza Yehova na zinaweza kuwa na matokeo mazuri sana. (Met 19:17; Mdo 20:35) Kwa hiyo, fikiria ni nani unayeweza kumtia moyo, na ufanye hivyo bila kukawia!

Laura akiangalia nje ya dirisha, Abbey akisali, Abbey na Laura wakikumbatiana na wakijitayarisha kupiga picha

TAZAMA VIDEO WATIE MOYO WASIOTENDA, NA KISHA UCHUNGUZE MASWALI YAFUATAYO:

  • Abbey alichukua hatua gani alipokutana na Shahidi ambaye hakumfahamu?

  • Kwa nini tunapaswa kuzungumza na wazee tunapofikiria kumsaidia mtu fulani asiyetenda?

  • Abbey alijitayarishaje ili kumtembelea Laura mara ya pili?

  • Abbey alionyeshaje uvumilivu, subira, na upendo alipokuwa akijaribu kumtia moyo Laura?

  • Tunajifunza nini kutokana na mfano wa Yesu unaopatikana kwenye Luka 15:8-10?

  • Jitihada ambazo wote walifanya ili kumsaidia Laura zilitokeza baraka gani?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki