Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • mwb18 Aprili uku. 8
  • Kuhubiri na Kufundisha​—Sehemu Muhimu ya Kufanya Wanafunzi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kuhubiri na Kufundisha​—Sehemu Muhimu ya Kufanya Wanafunzi
  • Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2018
  • Habari Zinazolingana
  • Mwalimu, Ufundishaji
    Ufahamu wa Kina wa Maandiko
  • Kuboresha Ustadi Wetu Katika Huduma​—Kuwasaidia Watu Wenye “Mwelekeo Unaofaa” Kuwa Wanafunzi
    Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2018
  • Je, Unaweza Kushiriki Katika Kazi ya Kufanya Wanafunzi?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2021
  • Vichwa vya Mazungumzo ya Biblia
    Vichwa vya Mazungumzo ya Biblia
Pata Habari Zaidi
Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2018
mwb18 Aprili uku. 8

MAISHA YA MKRISTO

Kuhubiri na Kufundisha​—Sehemu Muhimu ya Kufanya Wanafunzi

Yesu aliwaamuru wafuasi wake waende wakafanye wanafunzi. (Mt 28:19) Hilo linahusisha kuhubiri na kufundisha. Mara kwa mara, sisi sote tunapaswa kujiuliza, ‘Ninawezaje kufanya maendeleo katika sehemu hizi muhimu za kufanya wanafunzi?’

KUHUBIRI

Badala ya kungoja watu watutafute, tunapaswa kuwatafuta kwa bidii watu ‘wanaostahili’. (Mt 10:11) Tunaposhiriki katika huduma, je, tunatafuta nafasi za kuzungumza na watu ‘tunaowakuta’? (Mdo 17:17) Lidia alikuwa mwanafunzi kwa sababu mtume Paulo alihubiri kwa bidii.—Mdo 16:13-15.

Samweli akimwonyesha Ezekieli gazeti; Sulemani na Maria wakimhubiria Ezekieli na Abigaili

“Panda mbegu zako asubuhi na usipumzishe mkono wako mpaka jioni” (Mhu 11:6)

TAZAMENI VIDEO ENDELEA KUHUBIRI “BILA KUACHA”—ISIVYO RASMI NA NYUMBA KWA NYUMBA, KISHA MJIBU MASWALI YAFUATAYO:

  • Katika shughuli zake za kila siku, Samweli alionyeshaje kwamba alitafuta nafasi za kupanda mbegu za kweli kwa bidii?

  • Kwa nini tunapaswa kushiriki kwa bidii katika aina zote za kuhubiri?

  • Ni nani unayeweza kuhubiria ujumbe wa Ufalme unapokuwa katika shughuli zako za kila siku?

KUFUNDISHA

Ili tufanye wanafunzi, haitoshi tu kuwaachia watu machapisho. Ili tuwasaidie wafanye maendeleo ya kiroho, tunahitaji kufanya ziara za kurudia na kuanzisha mafunzo ya Biblia. (1Ko 3:6-9) Lakini, vipi ikiwa jitihada zetu za kumfundisha mtu kweli za Ufalme hazifanikiwi? (Mt 13:19-22) Tunapaswa kuendelea kuwatafuta wale ambao mioyo yao ni kama “udongo mzuri.”—Mt 13:23; Mdo 13:48.

Sulemani na Maria wakijifunza Biblia pamoja na Ezekieli na Abigaili; Ezekieli na Abigaili wakiwa katika utumishi wa hadharani

“Mimi nilipanda, Apolo akatia maji, lakini Mungu akaendelea kuikuza” (1Ko 3:6)

TAZAMENI VIDEO ENDELEA KUHUBIRI “BILA KUACHA”—HADHARANI NA KUFANYA WANAFUNZI, KISHA MJIBU MASWALI YAFUATAYO:

  • Solomoni na Mary walitiaje maji mbegu za kweli katika mioyo ya Ezekieli na Abigaili?

  • Tunapaswa kuwa na lengo gani tunaposhiriki katika nyanja zote za huduma, kutia ndani mahubiri ya hadharani?

  • Tunaweza kufanya nini ili tuonyeshe tunajitahidi kuwafundisha wengine kweli?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki