MAISHA YA MKRISTO
Epuka Mitego ya Mitandao ya Kijamii
KWA NINI NI MUHIMU?: Kama tu vifaa vingi, mitandao ya kijamii inaweza kuwa na faida na madhara. Baadhi ya Wakristo wamechagua kutotumia mitandao ya kijamii. Wakristo wengine hutumia mitandao ya kijamii kuwasiliana na watu wa familia na marafiki. Hata hivyo, Ibilisi anataka tutumie mitandao ya kijamii kwa njia isiyo na hekima, na hilo litaharibu sifa yetu na hali yetu ya kiroho. Kama Yesu, tunaweza kutumia kanuni za Neno la Mungu ili kutambua na kuepuka hatari.—Lu 4:4, 8, 12.
MITEGO YA KUEPUKA:
Kutumia mitandao ya kijamii kupita kiasi. Kutumia mitandao ya kijamii kwa saa nyingi kunaweza kutunyima wakati wenye thamani tunaohitaji ili kufanya mambo ya kiroho
Kanuni za Biblia: Efe 5:15, 16; Flp 1:10
Kutazama mambo yasiyofaa. Kutazama picha zisizofaa kunaweza kutufanya tuwe waraibu wa ponografia au kujihusisha katika maadili mapotovu. Kusoma habari za waasi-imani kunaweza kuharibu imani ya mtu
Kuweka picha au maelezo yasiyofaa. Kwa kuwa moyo ni wenye hila, huenda mtu akawa na mwelekeo wa kuweka picha au maelezo yasiyofaa kwenye mtandao wa kijamii. Hata hivyo, hilo linaweza kuharibu sifa ya mtu au kudhoofisha imani yake
TAZAMENI VIDEO YENYE KICHWA TUMIA MITANDAO YA KIJAMII KWA HEKIMA, KISHA ZUNGUMZIENI JINSI YA KUEPUKA HALI ZIFUATAZO: