MAISHA YA MKRISTO
Upendo Unawatambulisha Wakristo wa Kweli—Shangilia Pamoja na Kweli
KWA NINI NI MUHIMU: Kwa kumwiga Yesu, tunapaswa kutoa ushahidi kuhusu kweli ya makusudi ya Mungu. (Yoh 18:37) Pia tunapaswa kushangilia pamoja na kweli, kusema kweli, na kukazia fikiria mambo yoyote yaliyo ya kweli, licha ya kuishi katika ulimwengu uliojaa uwongo na ukosefu wa uadilifu.—1Ko 13:6; Flp 4:8.
JINSI YA KUFANYA HIVYO:
Azimia kutosikiliza au kueneza porojo zenye kudhuru.—1Th 4:11
Usishangilie mwingine anapoumia
Furahia mambo mazuri, yenye kutia moyo
TAZAMENI VIDEO YENYE KICHWA ‘IWENI NA UPENDO KATI YENU WENYEWE’—SHANGILIA PAMOJA NA KWELI, USISHANGILIE JUU YA UKOSEFU WA UADILIFU, KISHA MJIBU MASWALI YAFUATAYO:
Ni katika maana gani Debbie “alishangilia juu ya ukosefu wa uadilifu”?
Alice alibadilishaje mazungumzo yake na Debbie yahusu mambo yanayofaa?
Tunaweza kuzungumzia mambo gani mazuri?
Shangilia pamoja na kweli, usishangilie juu ya ukosefu wa uadilifu