MAISHA YA MKRISTO
Yehova Anawapenda Watu Safi
“Nawa mikono. Safisha chumba chako. Fagia sakafu. Nenda utupe takataka.” Wazazi wengi huwafundisha watoto wao jinsi ya kudumisha usafi wa kimwili. Hata hivyo, Mungu wetu mtakatifu ndiye chanzo cha usafi. (Kut 30:18-20; Kum 23:14; 2Ko 7:1) Tunapodumisha miili yetu na vitu vyetu vikiwa safi, tunamletea Yehova heshima. (1Pe 1:14-16) Namna gani kuhusu nyumba zetu na mazingira yetu? Tofauti na watu wanaotupa takatakata barabarani na kwenye bustani, Wakristo hujitahidi kuidumisha dunia ikiwa safi. (Zab 115:16; Ufu 11:18) Hata mambo madogo, kama vile kutupa karatasi za peremende, chupa za maji na soda, au big-G (chingamu), kunaweza kufunua mtazamo wetu kuhusu usafi. Katika maisha yetu yote, tungependa “kujipendekeza kuwa wahudumu wa Mungu.”—2Ko 6:3, 4.
TAZAMENI VIDEO MUNGU ANAWAPENDA WATU WALIO SAFI, KISHA MJIBU MASWALI YAFUATAYO:
Huenda watu wakatoa visingizio gani vya kutodumisha vitu vyao vikiwa safi?
Sheria ya Musa ilifunuaje maoni ya Yehova kuhusu usafi?
Tunawezaje kutoa ushahidi kimyakimya kumhusu Yehova?
Ninawezaje kuonyesha mtazamo wa Yehova kuhusu usafi katika maisha yangu binafsi?