MAISHA YA MKRISTO
Fahamu Mambo Yote Yanayohusika
Unaposoma masimulizi ya Biblia, jaribu kufahamu mambo yote yanayohusika. Jifunze kuhusu muktadha, watu waliohusika, na sababu ambazo huenda ziliwafanya watu watende kama walivyotenda. Tumia uwezo wako wa kuwazia ili kuona maeneo yanayotajwa, kusikia sauti mbalimbali, kunusa harufu zinazosimuliwa, na kutambua hisia za wahusika.
TAZAMENI VIDEO YENYE KICHWA BORESHA USOMAJI WAKO WA BIBLIA—KISEHEMU, KISHA MJIBU MASWALI YAFUATAYO:
Huenda ni mambo gani ambayo yalichangia kuwe na mkazo kati ya Yosefu na ndugu zake?
Huenda ni sababu zipi ambazo ziliwafanya ndugu za Yosefu watende kwa hisia kali na bila kufikiria matokeo?
Maandiko yanatusaidia kutambua nini kumhusu Yakobo, baba ya Yosefu?
Yakobo aliwafundisha watoto wake somo gani kuhusu kutatua kutokuelewana?
Umefaidikaje kwa kutazama video hii?