Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • mwb20 Julai uku. 7
  • Yehova Huwalinda Watu Wake

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Yehova Huwalinda Watu Wake
  • Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2020
  • Habari Zinazolingana
  • Jumba la Hifadhi ya Uangamizo na Mashahidi wa Yehova
    Amkeni!—1993
  • Jumba la Makumbusho la Uingereza Larekebishwa
    Amkeni!—2001
  • Faida za Kutembelea Majumba ya Ukumbusho
    Amkeni!—2005
  • Imani Thabiti Licha ya Mateso
    Amkeni!—2000
Pata Habari Zaidi
Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2020
mwb20 Julai uku. 7

MAISHA YA MKRISTO

Yehova Huwalinda Watu Wake

Baba Mwisraeli na mvulana wake wakinyunyiza damu kwenye miimo ya mlango wa nyumba yao.

Pasaka ilikuwa tukio muhimu sana. Usiku huo, Farao alipogundua kwamba mwana wake wa kwanza alikuwa amekufa, alimwambia Musa hivi: “Amkeni! Ondokeni kati ya watu wangu, ninyi wawili na Waisraeli wengine. Nendeni mkamtumikie Yehova, kama mlivyosema.” (Kut 12:31) Yehova alionyesha kwamba sikuzote yeye huwalinda watu wake.

Tunapochunguza historia ya siku za kisasa ya watu wa Yehova, tunaona uthibitisho wa wazi kwamba Yehova anaendelea kuwaongoza na kuwalinda. Unaweza kuona hilo kwenye maonyesho yaliyo kwenye makao makuu yenye kichwa “Watu kwa Ajili ya Jina la Yehova.”

TAZAMENI VIDEO YENYE KICHWA MAONYESHO YA WARWICK: “WATU KWA AJILI YA JINA LA YEHOVA,” KISHA MJIBU MASWALI YAFUATAYO:

  • Bango na picha kutoka kwenye ‘Photo-Drama of Creation.’

    Ni kifaa gani kilichotumiwa na Wanafunzi wa Biblia kuanzia mwaka wa 1914 ili kuimarisha imani katika Biblia, na kilikuwa na matokeo gani?

  • Picha za akina ndugu waliokamatwa na kufungwa mnamo 1918.

    Ni majaribu gani ya imani yaliyotokea katika mwaka wa 1916 na 1918, na kuna uthibitisho gani unaoonyesha kwamba Yehova alikuwa akiliongoza tengenezo?

  • Picha kwenye jumba la makumbusho zinazoonyesha wengi waliofungwa kwa sababu ya imani yao. Milango inayoelekeza kwenye chumba kilicho na picha za Paradiso.

    Watu wa Yehova wamefauluje kusimama imara katika imani licha ya upinzani?

  • A museum gallery showing some of the preaching methods used in the 1930’s and 1940’s.

    Ni uelewaji gani mpya ambao watu wa Yehova walipata katika mwaka wa 1935, na kulikuwa na matokeo gani?

  • Ikiwa umetembelea maonyesho hayo, ni nini ulichoona ambacho kiliimarisha imani yako kwamba Yehova anawaongoza na kuwalinda watu wake?

Ili kuona jinsi unavyoweza kutembelea maonyesho hayo, nenda kwenye jw.org® na ubofye tabo yenye kichwa Kutuhusu

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki