MAISHA YA MKRISTO
Yehova Huwalinda Watu Wake
Pasaka ilikuwa tukio muhimu sana. Usiku huo, Farao alipogundua kwamba mwana wake wa kwanza alikuwa amekufa, alimwambia Musa hivi: “Amkeni! Ondokeni kati ya watu wangu, ninyi wawili na Waisraeli wengine. Nendeni mkamtumikie Yehova, kama mlivyosema.” (Kut 12:31) Yehova alionyesha kwamba sikuzote yeye huwalinda watu wake.
Tunapochunguza historia ya siku za kisasa ya watu wa Yehova, tunaona uthibitisho wa wazi kwamba Yehova anaendelea kuwaongoza na kuwalinda. Unaweza kuona hilo kwenye maonyesho yaliyo kwenye makao makuu yenye kichwa “Watu kwa Ajili ya Jina la Yehova.”
TAZAMENI VIDEO YENYE KICHWA MAONYESHO YA WARWICK: “WATU KWA AJILI YA JINA LA YEHOVA,” KISHA MJIBU MASWALI YAFUATAYO:
Ni kifaa gani kilichotumiwa na Wanafunzi wa Biblia kuanzia mwaka wa 1914 ili kuimarisha imani katika Biblia, na kilikuwa na matokeo gani?
Ni majaribu gani ya imani yaliyotokea katika mwaka wa 1916 na 1918, na kuna uthibitisho gani unaoonyesha kwamba Yehova alikuwa akiliongoza tengenezo?
Watu wa Yehova wamefauluje kusimama imara katika imani licha ya upinzani?
Ni uelewaji gani mpya ambao watu wa Yehova walipata katika mwaka wa 1935, na kulikuwa na matokeo gani?
Ikiwa umetembelea maonyesho hayo, ni nini ulichoona ambacho kiliimarisha imani yako kwamba Yehova anawaongoza na kuwalinda watu wake?