MAISHA YA MKRISTO
Je, Unaweza Kutoa Wakati na Nguvu Zako?
Kama nabii Isaya alivyotabiri, tunajionea ukuzi mwingi sana katika sehemu ya kidunia ya tengenezo la Yehova. (Isa 54:2) Kwa sababu ya ukuzi huo, tunahitaji kujenga Majumba ya Ufalme, Majumba ya Kusanyiko, na majengo ya ofisi za tawi. Baada ya ujenzi, majengo kama hayo yanahitaji kudumishwa, na hatimaye baadhi yake lazima yafanyiwe ukarabati. Tunapata nafasi zipi za kumpa Yehova wakati na nguvu zetu?
Tunaweza kushiriki katika usafi wa Jumba la Ufalme wakati ambapo kikundi chetu cha utumishi kina mgawo huo
Tunaweza kujitolea kupata mazoezi ya kudumisha Jumba letu la Ufalme
Tunaweza kujaza fomu ya Ombi la Kujitolea Katika Kazi ya Usanifu na Ujenzi (DC-50) ili kusaidia mara kwa mara katika miradi ya ujenzi na udumishaji iliyo karibu na eneo tunaloishi
Tunaweza kujaza fomu ya Ombi la Kuwa Mjitoleaji (A-19) na kujitolea kusaidia kwa juma moja au zaidi katika eneo la ofisi yetu ya tawi iwe ni Betheli au katika jengo lingine la ofisi ya tawi
TAZAMENI VIDEO YENYE KICHWA MIPANGO INAFANYWA YA MRADI MPYA WA UJENZI—KISEHEMU, KISHA MJIBU MASWALI YAFUATAYO:
Kumekuwa na ongezeko gani kubwa katika matumizi ya video kuanzia mwaka 2014?
Ili kukabiliana na ongezeko la kutokezwa kwa video, ni mradi gani unaopangwa, na ujenzi umepangwa kufanywa lini?
Wajitoleaji wanaweza kusaidiaje katika mradi huu?
Ikiwa tungependa kusaidia katika ujenzi kule Ramapo, kwa nini tunapaswa kujaza fomu ya ombi (DC-50) na kusaidia katika miradi ya Idara ya Usanifu-Majengo na Ujenzi iliyo karibu na eneo letu?
Kumekuwa na uthibitisho gani kwamba Yehova amekuwa akiongoza mradi huu?
Tunawezaje kuunga mkono mradi huu hata ikiwa hatuwezi kusaidia katika ujenzi wenyewe?