Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • yb16 uku. 16-uku. 17 fu. 4
  • Ujenzi wa Majumba ya Ufalme Waharakishwa

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ujenzi wa Majumba ya Ufalme Waharakishwa
  • 2016 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
  • Habari Zinazolingana
  • Idara ya Ulimwenguni Pote ya Usanifu-Majengo na Ujenzi
    2015 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
  • Kazi ya Ujenzi Inayomletea Yehova Sifa
    Ufalme wa Mungu Unatawala!
  • Je, Unaweza Kutoa Wakati na Nguvu Zako?
    Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2020
  • Kujenga Pamoja Duniani Pote
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
Pata Habari Zaidi
2016 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
yb16 uku. 16-uku. 17 fu. 4
Mashahidi wa Yehova wakijenga Jumba la Ufalme

MATUKIO MUHIMU YA MWAKA ULIOPITA

Ujenzi wa Majumba ya Ufalme Waharakishwa

INASISIMUA sana kuona jinsi ambavyo Yehova anaharakisha ukuzi wa ibada ya kweli ulimwenguni pote. (Isa. 60:22) Hivyo, kumekuwa na uhitaji mkubwa unaongezeka wa Majumba ya Ufalme. Ulimwenguni pote, Majumba ya Ufalme zaidi ya 13,000 yanahitaji kujengwa au kufanyiwa ukarabati mkubwa.

Ili kujenga haraka na kwa gharama ndogo, Baraza Linaloongoza limefanya mabadiliko katika idara mbalimbali za ujenzi. Hivi karibuni, idara inayoitwa Idara ya Ulimwenguni Pote ya Usanifu-Majengo na Ujenzi (WDC) iliyo katika makao makuu huko Brooklyn, New York, ilianzishwa ili kushughulikia na kuharakisha miradi ya ujenzi na ukarabati ulimwenguni pote. Idara za Mkoa za Usanifu-Majengo na Ujenzi zilizoko katika ofisi ya tawi ya Afrika Kusini, Australia, Marekani, na Ujerumani huratibu ujenzi katika maeneo yao, hasa ujenzi wa Majumba ya Ufalme kwa muda mfupi na kwa gharama ndogo. Idara hiyo pia huandaa mazoezi kwa ndugu na dada wanaodumisha majengo katika eneo la ofisi yao ya tawi. Pia, katika kila ofisi ya tawi, Idara ya Mahali ya Usanifu-Majengo na Ujenzi huratibu ujenzi na udumishaji wa Majumba ya Ufalme na ya Kusanyiko.

Mwezi wa Januari 2015, wazee wote nchini Marekani walihudhuria mkutano uliounganishwa kupitia video uliozungumzia utaratibu mpya wa kusanifu, kujenga na kudumisha Majumba ya Ufalme. Walijifunza mambo yafuatayo.

  • Ujenzi: Muundo na vifaa vya ujenzi utategemea hali ya eneo na mwongozo kutoka Halmashauri ya Uchapishaji ya Baraza Linaloongoza. Majengo hayo yanapendeza, ni imara na rahisi kuyadumisha.

  • Udumishaji: Katika kila kutaniko, wajitoleaji watazoezwa jinsi ya kutunza majengo yetu ya ibada ili yadumu.

Kwa kweli, kujenga na kudumisha majengo ni kazi kubwa. Hata hivyo, bidii ya watu wa Mungu itaharakisha kazi, na hivyo michango itatumiwa kwa busara.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki