Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • yb15 uku. 16-uku. 17 fu. 4
  • Idara ya Ulimwenguni Pote ya Usanifu-Majengo na Ujenzi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Idara ya Ulimwenguni Pote ya Usanifu-Majengo na Ujenzi
  • 2015 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
  • Habari Zinazolingana
  • Ujenzi wa Majumba ya Ufalme Waharakishwa
    2016 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
  • Kazi ya Ujenzi Inayomletea Yehova Sifa
    Ufalme wa Mungu Unatawala!
  • Kujenga Pamoja Duniani Pote
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
  • Majumba ya Ufalme Yanajengwa Jinsi Gani na Kwa Nini?
    Ni Nani Wanaofanya Mapenzi ya Yehova Leo?
Pata Habari Zaidi
2015 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
yb15 uku. 16-uku. 17 fu. 4
Picha katika ukurasa wa 16

MATUKIO MUHIMU YA MWAKA ULIOPITA

Idara ya Ulimwenguni Pote ya Usanifu-Majengo na Ujenzi

ONGEZEKO la haraka katika tengenezo la Yehova linafanya kuwe na uhitaji mkubwa wa Majumba ya Ufalme, Majumba ya Kusanyiko, majengo kwa ajili ya shule za kitheokrasi, ofisi za utafsiri, na pia ofisi za tawi katika maeneo mbalimbali. Kwa hiyo, katika mwezi wa Oktoba 2013, Baraza Linaloongoza lilianzisha idara mpya ili kazi ya kusanifu, kujenga, kukarabati, na kudumisha majengo yetu ifanywe kwa njia bora zaidi na kwa gharama ndogo. Idara hii mpya inayoitwa Idara ya Ulimwenguni Pote ya Usanifu-Majengo na Ujenzi (WDC), iko katika makao makuu huko Broolyn, New York, na inafanya kazi chini ya mwelekezo wa Halmashauri ya Utangazaji ya Baraza Linaloongoza.

WDC husimamia Idara za Mkoa za Usanifu-Majengo na Ujenzi zilizoko katika ofisi ya tawi zilizoko Afrika Kusini, Australia, Marekani, na Ujerumani. Idara hizi huratibu usanifu, ujenzi, na udumishaji wa majengo katika maeneo yao. Lengo lao ni kuharakisha ujenzi wa Majumba ya Ufalme. Awali, Majumba ya Ufalme yalijengwa kwa msaada wa Halmashauri ya Ujenzi ya Mkoa au programu ya ujenzi katika nchi maskini. Idara hizo mbili zimeunganishwa ili ujenzi ufanywe kwa uharaka.

Ili kuratibu ujenzi wa Majumba ya Ufalme na Majumba ya Kusanyiko yanayohitajika, Idara ya Mahali ya Usanifu-Majengo na Ujenzi iliundwa katika kila ofisi ya tawi. Idara hii inasimamiwa na Halmashauri ya Ofisi ya Tawi. Jambo la kupendeza kuhusu marekebisho haya ni kwamba sasa ofisi zote za tawi zinaweza kuwapa mgawo watumishi wa ujenzi wa kudumu watakao wasaidia ndugu wenyeji kujenga Majumba ya Ufalme na Majumba ya Kusanyiko.

Kufikia Aprili 2014, kulikuwa na miradi mikubwa zaidi ya 270 ambayo ilihitaji kukamilishwa, kutia ndani ofisi za utafsiri 90, Majumba ya Kusanyiko 35, na Ofisi za tawi 130. Pia, kuna uhitaji mkubwa wa Majumba ya Ufalme zaidi ya 14,000 ambayo lazima yajengwe au kufanyiwa ukarabati mkubwa.

Imani yetu inaimarishwa sana tunapoona watu wa Yehova wenye umoja kutoka mataifa, tamaduni na lugha mbalimbali wakijenga majengo yanayotukuza na kuliheshimu jina takatifu la Yehova! Dan Molchan, wa Halmashauri ya Wafanyakazi katika makao makuu anasema hivi: “Kuna kazi nyingi ambayo bado inahitaji kufanywa, na kwa sababu hiyo tunathamini sala za akina ndugu na dada, pamoja na michango yao ili kuendeleza kazi hii. Hata hivyo, tunawashukuru sana ndugu na dada ambao wamejitoa kwa hiari ili kusaidia katika miradi hii ya ujenzi.”

KUFIKIA APRILI 2014, KULIKUWA NA MIRADI MIKUBWA ZAIDI YA 270 AMBAYO ILIHITAJI KUKAMILISHWA, KUTIA NDANI:

  • Ofisi za Utafsiri 90

  • Majumba ya Kusanyiko 35

  • Ofisi za Tawi 130

Pia, kuna uhitaji mkubwa wa Majumba ya Ufalme zaidi ya 14,000 ambayo yanahitaji kujengwa au kufanyiwa ukarabati mkubwa.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki