“Upendo alio nao Kristo hutuchochea.”—2Ko 5:14
MAISHA YA MKRISTO
Je, Utatumikia Ukiwa Painia Msaidizi Mwezi wa Machi au Aprili?
Je, ungependa kufanya mengi zaidi katika utumishi wa Yehova wakati wa majira ya ukumbusho? (2Ko 5:14, 15) Katika mwezi wa Machi na Aprili, mapainia wasaidizi wanaweza kuchagua kutimiza takwa la saa 30 au 50. Ikiwa unaweza kushiriki katika utendaji huo wa pekee, wasilisha ombi lako kwa Halmashauri ya Utumishi ya Kutaniko. Kila mwezi, kutaniko litatangaziwa majina ya wale walioidhinishwa kutumikia wakiwa mapainia wasaidizi. Kwa njia hiyo, kutaniko linaweza kuwaunga mkono mapainia hao katika huduma. Sote na tutumie kikamili nafasi zitakazojitokeza wakati wa majira ya ukumbusho ili kuboresha ustadi wetu wa kuhubiri na kuwatia wengine moyo.—1Th 5:11.