Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • mwb21 Septemba kur. 3-16
  • Tumia Furahia Maisha Milele! Katika Huduma Yako

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Tumia Furahia Maisha Milele! Katika Huduma Yako
  • Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2021
  • Habari Zinazolingana
  • Jinsi ya Kuongoza Mafunzo ya Biblia kwa Kutumia Kitabu “Furahia Maisha Milele!”
    Wapende Watu—Fanya Wanafunzi
  • Wasaidie Wanafunzi Wako wa Biblia Wafikie Ubatizo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2021
  • Jinsi ya Kumsaidia Mwanafunzi wa Biblia Afikie Hatua ya Ubatizo—Sehemu ya Kwanza
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2020
  • Jinsi ya Kutumia Broshua Habari Njema Kutoka kwa Mungu!
    Huduma ya Ufalme—2013
Pata Habari Zaidi
Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2021
mwb21 Septemba kur. 3-16
Wenzi wa ndoa wakitumia broshua “Furahia Maisha Milele!” kuzungumza na mwanamume kwenye kituo cha basi.

MAISHA YA MKRISTO

Tumia Furahia Maisha Milele! Katika Huduma Yako

Tumefurahi sana kupata broshua na kitabu kipya kwa ajili ya kuongoza mafunzo ya Biblia. Tunasali kwamba Yehova atabariki jitihada zetu za kufanya wanafunzi wengi zaidi. (Mt 28:18-20; 1Ko 3:6-9) Tunaweza kutumiaje vifaa hivyo vipya?

Kwa kuwa Furahia Maisha Milele! masomo ya kujifunza Biblia, ni njia mpya ya kufundisha, fuata miongozo hii unapojitayarisha na unapoongoza mafunzo ya Biblia.a

  • Someni habari, na mzungumzie maswali

  • Someni maandiko yaliyoandikwa “soma” na umsaidie mwanafunzi kuelewa jinsi maandiko hayo yanavyomhusu

  • Onyesha video zilizoonyeshwa na kuzizungumzia, ukitumia maswali yoyote yaliyoonyeshwa

  • Jaribu kumaliza somo moja kila mara mnapojifunza

Katika huduma, kwanza mtolee mwenye nyumba broshua ili kuona ikiwa anapendezwa. (Ona sanduku lenye kichwa “Jinsi ya Kutoa Broshua Furahia Maisha Milele! Katika Ziara ya Kwanza.”) Mnapomaliza kujifunza broshua hiyo pamoja na mwanafunzi angependa kuendelea, mpe kitabu na mwanzie kwenye somo la 04. Ikiwa tayari mnajifunza kitabu Biblia Inatufundisha au kitabu Dumu Katika Upendo wa Mungu, hamisha funzo hilo kwenye kitabu Furahia Maisha Milele! na uamue mahali mtakapoanzia.

Wenzi hao wakitumia kitabu “Furahia Maisha Milele!” kuongoza funzo la Biblia na mwanamume hiyo akiwa nyumbani.

TAZAMENI VIDEO YENYE KICHWA KARIBU KWENYE FUNZO LAKO LA BIBLIA, KISHA MJIBU MASWALI YAFUATAYO:

  • Wanafunzi watajifunza nini katika kitabu kipya?

  • Kwa nini unapaswa kuwaonyesha wanafunzi wapya video hii?

  • Unapaswa kumtia moyo mwanafunzi ajiwekee miradi gani na kuifikia hatua kwa hatua?—Ona chati yenye kichwa “Wazo Kuu na Lengo kwa Ajili ya Kila Sehemu.”

a ZINGATIA: Ingawa sehemu ya “Chunguza Zaidi” si ya lazima kusoma wakati wa funzo, tenga wakati wa kusoma au kutazama kila sehemu unapojitayarisha. Kisha utajua ni nini ambacho kitampendeza na kumsaidia zaidi mwanafunzi wako. Nakala za kielektroni zinatia ndani viunganishi kwa ajili ya video na habari za ziada.

WAZO KUU NA LENGO KWA AJILI YA KILA SEHEMU

 

MASOMO

WAZO KUU

MALENGO YA MWANAFUNZI

1

01-12

Chunguza jinsi Biblia inavyoweza kukusaidia na jinsi unavyoweza kumjua Mtungaji wa Biblia

Mtie moyo mwanafunzi asome Biblia, ajitayarishe kwa ajili ya funzo, na aanze kuhudhuria mikutano

2

13-33

Ona mambo ambayo Mungu ametufanyia na ibada inayomfurahisha

Mchochee mwanafunzi awaeleze wengine kuhusu kweli na kustahili kuwa mhubiri

3

34-47

Jifunze mambo ambayo Mungu anataka waabudu wake wafanye

Mchochee mwanafunzi ajiweke wakfu kwa Yehova na abatizwe

4

48-60

Jifunze jinsi unavyoweza kubaki katika upendo wa Mungu

Mfundishe mwanafunzi kutofautisha kati ya mambo yanayofaa na yasiyofaa na umsaidie kufanya maendeleo ya kiroho

JINSI YA KUTOA BROSHUA FURAHIA MAISHA MILELE! KATIKA ZIARA YA KWANZA

Sawa na trakti zetu, ukurasa wa nyuma wa broshua yetu una swali lenye kuamsha upendezi. Jaribu kufanya mambo yafuatayo:

  • Muulize swali lililoonyeshwa lililo na majibu kadhaa

  • Soma jibu la Biblia kwenye Zaburi 37:29

  • Zungumzia habari zilizo chini ya kichwa “Hilo Linawezaje Kuboresha Maisha Yako?” Muda ukiruhusu, soma maandiko na uzungumzie picha zilizoonyeshwa

  • Muulize swali “Je, Kweli Tunaweza Kuamini Ahadi za Biblia?” lililoonyeshwa kwenye ukurasa huo, kisha ujaribu kuanzisha funzo la Biblia kwenye somo la kwanza

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki