BORESHA HUDUMA YAKO | ONGEZA SHANGWE YAKO KATIKA HUDUMA
Kubali Msaada wa Yehova Kupitia Sala
Yehova ndiye anayefanya mbegu ya kweli itie mzizi na kukua katika moyo wa mtu. (1Ko 3:6-9) Hivyo, ili tufanikiwe katika huduma, ni lazima tumtegemee Yehova ili atusaidie sisi na wanafunzi wetu wa Biblia.
Mwombe Yehova awasaidie wanafunzi wako kuvumilia wanaposhinikizwa na waweze kushinda vikwazo. (Flp 1:9, 10) Taja mambo hususa. Sali upate roho takatifu ili iongoze mawazo na matendo yako. (Lu 11:13) Wafundishe wanafunzi wako wa Biblia jinsi ya kusali, na uwahimize wafanye hivyo. Sali pamoja na wanafunzi wako wa Biblia na kwa niaba yao, ukitaja majina yao.
TAZAMENI VIDEO YENYE KICHWA PATA SHANGWE YA KUFANYA WANAFUNZI—KUBALI MSAADA WA YEHOVA—SALA, KISHA MJIBU MASWALI YAFUATAYO:
Neema alikabili changamoto gani alipokuwa akijifunza na Lulu?
1 Wakorintho 3:6 ilimsaidiaje Neema?
Changamoto ambayo Neema alikabili ilishughulikiwaje?