MAISHA YA MKRISTO
Sehemu Muhimu za Furahia Maisha Milele!
Unapotumia kitabu Furahia Maisha Milele! je, unafurahia kutumia video na maswali ya maoni yaliyomo? Vipi sehemu ya “Watu Fulani Husema,” “Lengo,” na “Chunguza Zaidi”? Ni sehemu gani nyingine ambayo umeona kuwa yenye manufaa unaposhiriki katika kazi ya kufanya wanafunzi?—Mt 28:19, 20.
Marejeo: Ikiwa unapenda kuongoza funzo la Biblia kwa kutumia kitabu kilichochapishwa, unawezaje kupata video na habari nyingine katika sehemu moja? Kwenye kitabu cha kielektroni, teua sehemu moja kati ya sehemu zile nne kuu. Chini kabisa kwenye orodha ya vichwa vya masomo, utapata marejeo yote ya sehemu hiyo moja. (Ona picha ya 1.)
Mfumo wa “Toleo Lililochapishwa”: Unapojifunza na mtu kwa kutumia kifaa cha kielektroni, huenda ikafaa kutumia mfumo wa “Toleo Lililochapishwa” pindi kadhaa wakati wa funzo. Baada ya kufungua somo, bofya vitufe vitatu kwenye sehemu ya juu ya ukurasa na uteue sehemu iliyoandikwa “Toleo Lililochapishwa.” Mpangilio huo unaweza kukusaidia kuelewa wazi jinsi habari mnayozungumzia inavyopatana na mada kuu ya somo lote. Ili kurudi kwenye toleo la kawaida, bofya vitufe hivyo vitatu tena na uteue “Toleo la Kidijitali.”
“Je, Niko Tayari?”: Masanduku hayo yaliyo karibu na mwisho wa kitabu yanaonyesha sifa za msingi za kustahili kuhubiri pamoja na kutaniko na kubatizwa. (Ona picha ya 2.)
Maelezo ya Ziada: Maelezo ya ziada huandaa habari zinazofafanua mambo fulani muhimu. Kitabu cha kielektroni kina kiunganishi mwishoni mwa kila maelezo ya ziada, ambacho kitakurudisha mahali ulipoachia kwenye somo. (Ona picha ya 2.)
Hakikisha unamaliza kujifunza Furahia Maisha Milele! pamoja na wanafunzi wa Biblia wanaofanya maendeleo, hata ikiwa watabatizwa kabla ya kukimaliza. Unaweza kuendelea kuhesabu muda, ziara za kurudia, na funzo hilo hata ikiwa mwanafunzi tayari amebatizwa. Mhubiri akiandamana nawe na kushiriki katika funzo, yeye pia anaweza kuhesabu muda huo