Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w22 Aprili kur. 2-3
  • Jinsi ya Kukabiliana na Mahangaiko kwa Mafanikio

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Jinsi ya Kukabiliana na Mahangaiko kwa Mafanikio
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2022
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • JINSI DAUDI ALIVYOKABILIANA NA MAHANGAIKO KWA MAFANIKIO
  • MWIGE DAUDI UNAPOKABILIANA NA MAHANGAIKO
  • YEHOVA ATAKUSAIDIA UFANIKIWE
  • Mtupie Yehova Mahangaiko Yako Yote
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2016
  • Mtwikeni Yehova Hangaiko Lenu Lote
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
  • Biblia Inasema Nini?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2017
  • Ninaweza Kukabilianaje na Mahangaiko?
    Vijana Huuliza
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2022
w22 Aprili kur. 2-3
Ndugu akisali kwa ajili ya mke wake mgonjwa, aliyelala kwenye kitanda cha hospitali.

Jinsi ya Kukabiliana na Mahangaiko kwa Mafanikio

WASIWASI au mahangaiko yanaweza kuwa kama mzigo mzito unaotulemea moyoni. (Met. 12:25) Je, umewahi kukabili mkazo mkubwa unaosababishwa na mahangaiko maishani mwako? Je, umewahi kuhisi kwamba umelemewa kihisia na huwezi kuvumilia tena? Ikiwa ndivyo, huko peke yako. Huenda wengi wetu tunatunza wapendwa wetu, tumefiwa na mpendwa, tumekabili janga la asili, au tumekabili hali nyingine ambayo imetulemea kimwili, kiakili, na kihisia. Lakini ni mambo gani yanayoweza kutusaidia kukabiliana na mahangaiko kwa mafanikio?a

Tunaweza kujifunza mengi kuhusu jinsi ya kukabiliana na mahangaiko kwa kuchunguza maisha ya Mfalme Daudi. Alikabili hali nyingi ngumu maishani mwake, na wakati mwingine uhai wake ulikuwa hatarini. (1 Sam. 17:34, 35; 18:10, 11) Daudi alikabilianaje na mahangaiko kwa mafanikio? Tunaweza kuigaje mfano wake?

JINSI DAUDI ALIVYOKABILIANA NA MAHANGAIKO KWA MAFANIKIO

Daudi alikabili majaribu mbalimbali kwa wakati uleule. Kwa mfano, fikiria hali iliyotokea alipokuwa akimkimbia Mfalme Sauli aliyetaka kumuua. Daudi na wanaume wake waliporudi kutoka vitani, walishangaa walipotambua kwamba maadui walikuwa wamepora mali zao, wameteketeza nyumba zao, na kuchukua mateka familia zao. Daudi alitendaje? “Daudi na wanaume waliokuwa pamoja naye wakaanza kulia kwa sauti kubwa mpaka wakakosa nguvu za kuendelea kulia.” Isitoshe Daudi alipata mkazo hata zaidi wakati wanaume aliowatumaini ‘walipotaka kumpiga mawe.’ (1 Sam. 30:1-6) Pindi hiyo Daudi alikabili hali tatu ngumu sana kwa wakati mmoja: Familia yake ilikuwa hatarini, aliogopa kwamba wanaume wake wangemuua, na bado Mfalme Sauli alikuwa akimwinda. Wazia jinsi Daudi alivyokuwa na wasiwasi mwingi!

Daudi alichukua hatua gani? Mara moja “akajitia nguvu kwa msaada wa Yehova Mungu wake.” Huenda Daudi alifanya hivyo jinsi gani? Daudi alikuwa na zoea la kusali kwa Yehova na kutafakari jinsi alivyokuwa amemsaidia wakati uliopita. (1 Sam. 17:37; Zab. 18:2, 6) Daudi alitambua kwamba alihitaji kutafuta mwongozo wa Yehova, basi akatafuta habari kutoka kwa Yehova kuhusu jambo ambalo alipaswa kufanya. Baada ya Daudi kupata mwongozo kutoka kwa Yehova, alichukua hatua mara moja. Matokeo ni kwamba Yehova alimbariki yeye na wanaume wake, nao wakakomboa familia na mali zao. (1 Sam. 30:7-9, 18, 19) Je, umetambua mambo matatu ambayo Daudi alifanya? Alisali kwa Yehova ili kupata msaada, alitafakari jinsi Yehova alivyomsaidia wakati uliopita, kisha akatenda kulingana na mwongozo wa Yehova. Tunaweza kumwigaje Daudi? Fikiria njia tatu zifuatazo.

MWIGE DAUDI UNAPOKABILIANA NA MAHANGAIKO

Mkusanyo wa picha: Hatua tunazoweza kuchukua tunapokuwa na mahangaiko. 1. Sali. Ndugu akisali kwa ajili ya mke wake mgonjwa, aliyelala kwenye kitanda cha hospitali. 2. Tafakari. Ndugu huyo anakumbuka wakati yeye alipokuwa hospitali na ndugu mwingine alishiriki naye andiko. 3. Tenda. Ndugu akiwa ameketi pamoja na mke wake mgonjwa, akishiriki naye andiko.

1. Sali. Kila mara tunapopatwa na mahangaiko, tunaweza kusali kwa Yehova na kumwomba atupe msaada na hekima. Tunaweza kupunguza wasiwasi kwa kusali kwa bidii na kummiminia mahangaiko yaliyo moyoni mwetu. Au tunaweza kutoa sala fupi kimyakimya, ikiwa hilo ndilo jambo tunaloweza kufanya kwa wakati huo. Kila mara tunapomwomba Yehova msaada, tunaiga uhakika huu aliokuwa nao Daudi: “Yehova ni jabali langu na ngome yangu na Mwokozi wangu. Mungu wangu ni mwamba wangu, ninayemkimbilia.” (Zab. 18:2) Je, kweli kusali kunaweza kutusaidia? Dada painia anayeitwa Kahlia, anasema hivi: “Baada ya kusali, mimi huhisi amani. Sala hunisaidia kupatanisha mawazo yangu na fikira za Yehova, nami ninamtumaini hata zaidi.” Kwa kweli, sala ni msaada wenye nguvu kutoka kwa Yehova ambao unatusaidia kukabiliana na mahangaiko.

2. Tafakari. Unapofikiria mambo uliyopitia maishani, je, unakumbuka majaribu ambayo ulifaulu kuvumilia kupitia tu msaada wa Yehova? Tunapotafakari jinsi ambavyo Yehova ametusaidia sisi na pia alivyowasaidia watumishi wake zamani, tunaimarishwa na kuwa na uhakika zaidi katika Yehova. (Zab. 18:17-19) Mzee wa kutaniko anayeitwa Joshua, anasema hivi: “Nina orodha ya sala ambazo zilijibiwa. Hilo linanisaidia kukumbuka nyakati ambazo nilimwomba Yehova jambo hususa, naye akanipa kile ambacho hasa nilihitaji.” Naam, tunapofikiria kuhusu mambo ambayo tayari Yehova ametutimizia, tunapata nguvu tunazohitaji ili kukabiliana na mahangaiko.

3. Tenda. Kabla ya kuamua jambo tutakalofanya katika hali fulani, tunaweza kuchunguza Neno la Mungu ili kupata mwongozo unaotegemeka zaidi. (Zab. 19:7, 11) Wengi wametambua kwamba wanapofanya utafiti kuhusu andiko fulani, wanaelewa vizuri zaidi jinsi wanavyoweza kutumia andiko hilo maishani mwao. Mzee wa kutaniko anayeitwa Jarrod, anaeleza hivi: “Kufanya utafiti hunisaidia kutambua mambo mbalimbali kuhusu andiko fulani na kuelewa jambo ambalo Yehova ananiambia. Hilo hunisaidia kukazia kabisa jambo hilo moyoni mwangu ili nitende kulingana na mwongozo wake.” Tunapotafuta mwongozo wa Yehova katika Maandiko na kutenda kulingana na mwongozo huo, tunaweza kukabiliana vizuri zaidi na mahangaiko.

YEHOVA ATAKUSAIDIA UFANIKIWE

Daudi alitambua kwamba alihitaji msaada wa Yehova ili afaulu kukabiliana na mahangaiko. Alithamini sana msaada wa Yehova, hivi kwamba alichochewa kusema hivi: “Kwa nguvu za Mungu ninaweza kuupanda ukuta. Mungu wa kweli ndiye anayenivisha nguvu.” (Zab. 18:29, 32) Huenda tukahisi kwamba majaribu yetu ni kama ukuta tusioweza kuupanda. Lakini kwa msaada wa Yehova, tunaweza kushinda majaribu yoyote yaliyo kama ukuta! Naam, tunaposali ili kupata msaada wa Yehova, tunapotafakari mambo ambayo ametufanyia, na kutenda kulingana na mwongozo wake, tunaweza kuwa na uhakika kwamba atatupatia nguvu na hekima tunayohitaji ili tufaulu kukabiliana na mahangaiko yetu!

a Huenda mtu aliye na ugonjwa wa kuwa na wasiwasi kupita kiasi akahitaji kutafuta msaada wa daktari.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki