Utangulizi
Mamilioni ya watu ulimwenguni huathiriwa na matatizo ya afya ya akili. Hali hizo huwapata watu wote, haijalishi taifa, dini, vijana, wazee, maskini, matajiri, wenye elimu au wasio na elimu. Magonjwa ya akili ni nini, nayo huwaathirije watu? Gazeti hili litazungumzia umuhimu wa kupata matibabu yanayofaa na pia litaonyesha jinsi Biblia inavyoweza kuwasaidia watu wenye matatizo hayo kwa njia mbalimbali zinazofaa.