Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • wp23 Na. 1 kur. 6-7
  • 1 | Sala—‘Mtupie Mahangaiko Yako Yote’

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • 1 | Sala—‘Mtupie Mahangaiko Yako Yote’
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2023
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Inamaanisha Nini?
  • Hilo Linaweza Kutusaidiaje?
  • Mtupie Yehova Mahangaiko Yako Yote
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2016
  • Ninaweza Kukabilianaje na Mahangaiko?
    Vijana Huuliza
  • Mtwikeni Yehova Hangaiko Lenu Lote
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
  • Jinsi Biblia Inavyoweza Kuwasaidia Wanaume Kukabiliana na Mahangaiko
    Habari Zaidi
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2023
wp23 Na. 1 kur. 6-7
Kijana mwenye mahangaiko akisali huku akiwa ameshika kifua chake.

1 | Sala​—‘Mtupie Mahangaiko Yako Yote’

BIBLIA INASEMA HIVI: “Mkitupa mahangaiko yenu yote juu yake [Mungu], kwa sababu yeye anawajali ninyi.”​—1 PETRO 5:7.

Inamaanisha Nini?

Yehova Mungu anatualika tuzungumze naye kuhusu tatizo lolote linalolemea akili na moyo wetu. (Zaburi 55:22) Unaweza kusali kuhusu jambo lolote, liwe kubwa au dogo. Ikiwa jambo hilo ni la muhimu kwetu, ni la muhimu kwa Yehova pia. Ni muhimu tusali kwake ili tupate amani ya akili.​—Wafilipi 4:6, 7.

Hilo Linaweza Kutusaidiaje?

Huenda tukahisi upweke tunaposumbuliwa na matatizo ya akili. Mara nyingi watu wengine hawaelewi kikamili hali tunazopitia. (Methali 14:10) Lakini tukisali na kumweleza Mungu hisia zetu kwa unyoofu, atatusikiliza kwa fadhili na ataelewa hali yetu. Yehova anaona, anajua maumivu na mahangaiko yetu na anataka tusali kuhusu kitu chochote kinachotuhangaisha.​—2 Mambo ya Nyakati 6:29, 30.

Kusali kwa Yehova kunaimarisha uhakika wetu kwamba anatujali. Tunaweza kuhisi kama alivyohisi mtunga Zaburi aliyesali hivi: “Umeona dhiki yangu; unajua mateso makali yaliyo ndani yangu.” (Zaburi 31:7) Kujua kwamba Yehova anaona mambo tunayokabili, kunaweza kutusaidia kuvumilia nyakati ngumu. Lakini anafanya mengi zaidi ya kuona matatizo yetu. Anajua vizuri sana mambo tunayopitia kuliko mtu mwingine yeyote, na anatusaidia kupata faraja na kitia moyo kupitia Biblia.

Jinsi Biblia Inavyomsaidia Julian

Jinsi Mahangaiko Yanavyoniathiri

Julian.

“Ninasumbuliwa na mahangaiko na ugonjwa wa kushindwa kudhibiti mawazo na misukumo (OCD). Ninapatwa na mahangaiko wakati wowote bila kutarajia. Wakati fulani ninakuwa sawa na wakati mwingine ninakuwa na mahangaiko sana bila sababu yoyote ya msingi. Ninakuwa na mahangaiko hasa ninapokuwa pamoja na watu. Ninafikiria sana jinsi wanavyohisi kunihusu.

“Wale wanaojua matatizo yangu, wananitegemeza sana. Kusema kweli wakati mwingine wananiambia mambo ambayo sikutarajia waniambie. Lakini ninathamini msaada wao.

“Wakati mwingine ninashindwa kusali kwa sababu ya mahangaiko na OCD. Ninahitaji jitihada nyingi sana za kiakili ili niweze kukaza fikira na kuzungumza na Yehova katika sala. Ninafikiria mambo mengi sana kwa wakati mmoja kiasi kwamba ninashindwa kudhibiti mawazo yangu. Ninaposhindwa kudhibiti mawazo yangu, inakuwa vigumu kumweleza Yehova mambo ninayohisi au kufikiri.”

Jinsi Biblia Inavyonisaidia

“Nimejifunza katika Biblia kwamba sihitaji kusali sala ndefu au kwa ufasaha ili Mungu aisikilize. Ninaposhindwa kueleza hisia zangu, ninasali tu: ‘Yehova tafadhali nisaidie.’ Hata nikisali hivyo, ninatambua kwamba Yehova ananielewa na atanipatia kile ninachohitaji wakati huo. Zaidi ya kusali, nimetafuta pia msaada wa matibabu. Ninafurahi kusema kwamba njia hizo zimenisaidia. Sasa hali yangu imekuwa bora zaidi. Ingawa jitihada nyingi sana zinahusika ili kumwomba Baba yangu wa mbinguni msaada, ninasali kwake kwa sababu ninajua ananipenda na anataka kunisaidia.”

Msaada kwa Ajili ya Vijana

Video “Uwe Rafiki ya Yehova—Sali Wakati Wowote.”

Katika tovuti ya jw.org/sw, utajifunza kwa nini unaweza kuwa na uhakika kwamba Yehova husikiliza na kujibu sala zako.

Tazama video Uwe Rafiki ya Yehova —Sali Wakati Wowote.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki