Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • wp23 Na. 1 kur. 8-9
  • 2 | ‘Faraja Kutoka Kwenye Maandiko’

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • 2 | ‘Faraja Kutoka Kwenye Maandiko’
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2023
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Inamaanisha Nini?
  • Hilo Linaweza Kutusaidiaje?
  • Ni Nini Kinachoweza Kuwasaidia Vijana Walioshuka Moyo?
    Amkeni!—2017
  • Msaada Kutoka kwa “Mungu wa Faraja”
    Amkeni!—2009
  • Hisiamoyo Zisizofaa— Zinaweza Kushindwaje?
    Amkeni!—1992
  • Jinsi Unavyoweza Kuzuia Hisia Zisizofaa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2010
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2023
wp23 Na. 1 kur. 8-9
Mwanamume mzee akitafakari mambo anayosoma katika Biblia.

2 | ‘Faraja Kutoka Kwenye Maandiko’

BIBLIA INASEMA HIVI: “Mambo yote yaliyoandikwa zamani yaliandikwa ili kutufundisha, ili kupitia uvumilivu wetu na kupitia faraja kutoka kwa Maandiko tuwe na tumaini.”​—WAROMA 15:4.

Inamaanisha Nini?

Biblia ina mawazo yenye kufariji yanayotusaidia kupata nguvu na uvumilivu, tunapokabiliana na mawazo yasiyofaa. Pia, Biblia inatuahidi kwamba hivi karibuni maumivu ya kihisia yataisha.

Hilo Linaweza Kutusaidiaje?

Sisi sote huhisi huzuni nyakati fulani; lakini wale wenye mshuko moyo au mahangaiko huenda wakahisi maumivu ya kihisia wakati wote. Biblia inaweza kuwasaidiaje?

  • Biblia ina mawazo mengi mazuri yanayoweza kuchukua nafasi ya mawazo mabaya. (Wafilipi 4:8) Inaweza kujaza akili zetu mawazo yenye kufariji na yanayotuliza, ambayo yatatusaidia kudhibiti hisia zetu.​—Zaburi 94:18, 19.

  • Biblia inaweza kutusaidia tuache kufikiri kwamba hatufai.​—Luka 12:6, 7.

  • Mistari mingi ya Biblia inatuhakikishia hatuko peke yetu na kwamba Mungu, Muumba wetu, anaelewa kikamili hisia zetu.​—Zaburi 34:18; 1 Yohana 3:19, 20.

  • Biblia inaahidi kwamba Mungu atatuondolea kumbukumbu mbaya. (Isaya 65:17; Ufunuo 21:4) Tunaposumbuliwa na mawazo na hisia zenye kuumiza, ahadi hiyo inaweza kutupatia nguvu za kuvumilia.

Jinsi Biblia Inavyomsaidia Jessica

Jinsi Ninavyoathiriwa na Mshuko Moyo

Jessica amelala huku Biblia yake ikiwa mkononi.

“Nilipokuwa na umri wa miaka 25, nilichoka sana kiakili na kihisia na mwishowe niligunduliwa nina mshuko moyo mbaya sana. Nilisumbuliwa na kumbukumbu za mambo mabaya niliyopitia zamani. Madaktari walinisaidia kutambua kwamba nilishuka moyo kwa sababu niliendelea kufikiria mambo mabaya yaliyonipata maishani. Zaidi ya kupewa dawa zinazofaa, nilihitaji kupata ushauri utakaonisaidia kutambua na kurekebisha njia yangu ya kufikiri.”

Jinsi Biblia Inavyonisaidia

“Nilipokuwa nimeshuka moyo sana, nilikuwa na wasiwasi sana, mahangaiko mengi, na kukosa usingizi. Mara nyingi usiku nililemewa na mawazo mengi mabaya. Kama Zaburi 94:19 inavyosema, Mungu anaweza kutufariji na kutubembeleza tunapolemewa na mahangaiko. Hivyo, niliweka karibu na kitanda changu Biblia, na daftari lenye maandiko ya kunitia moyo. Niliposhindwa kulala, nilisoma mistari kadhaa ya Biblia na hivyo kuruhusu mawazo ya Mungu yanifariji.

“Biblia inatutia moyo tuondoe mawazo yasiyopatana na mambo tunayojua kumhusu Mungu. Zamani niliamini sina thamani, sipendwi, na sifai. Nimejifunza kwamba mambo hayo hayapatani na maoni ya Biblia, inayoonyesha kwamba Mungu ni Baba mwenye upendo na huruma, ambaye anamjali kila mmoja wetu. Hatua kwa hatua, nilianza kuyadhibiti mawazo yangu badala ya kuyaruhusu yanidhibiti. Nimejifunza kujiona kama Mungu anavyoniona. Hiyo ilikuwa hatua muhimu ya kuondoa mawazo yasiyofaa kujihusu.

“Ninatazamia wakati ambapo kumbukumbu zenye kuumiza na njia mbaya ya kufikiri zitaondolewa. Ninajua kwamba wakati ujao, hakutakuwa na magonjwa ya akili. Hilo linanisaidia kuvumilia sasa na kutazamia wakati ujao ambapo sitakuwa na mshuko moyo tena.”

Kwa Msaada Zaidi:

Soma makala yenye kichwa, “Msaada Kutoka kwa ‘Mungu wa Faraja,’” kwenye gazeti la Amkeni! la Julai 2009 linalopatikana katika jw.org/sw.

Sikiliza rekodi ya usomaji wa kitabu cha Zaburi katika Kiingereza inayopatikana kwenye jw.org.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki