Dokezo la Kujifunza
Pata Hazina za Kiroho Kumhusu Yehova
Tunaposoma Biblia, tunaweza kutumia vifaa mbalimbali vya kujifunzia ili kuelewa vizuri mambo tunayosoma. Hata hivyo, hatujifunzi ili tu kuongeza ujuzi wetu. Tungependa kupata hazina za kiroho kuhusu utu wa Yehova na hivyo kuongeza upendo wetu kumwelekea. Ili kufanya hivyo, tunaweza kujiuliza hivi, ‘Simulizi hili la Biblia linanifundisha nini kumhusu Yehova?’
Tunaweza kuchunguza jinsi ambavyo Yehova ameonyesha upendo, hekima, haki, na nguvu. Hata hivyo, utu wa Yehova hauhusiani tu na sifa hizo. Unatia ndani sifa nyingine zenye kuvutia. Unaweza kupata wapi habari zaidi kuhusu sifa zake?
Chunguza orodha yenye sifa nyingine zaidi ya 50 katika Fahirisi chini ya kichwa kikuu “Yehova” kisha kichwa kidogo “Sifa Kulingana na Majina.” Fanya utafiti kuhusu sifa zinazohusiana na simulizi la Biblia ambalo unasoma. (Ikiwa unaweza tu kupata Mwongozo wa Utafiti wa Mashahidi wa Yehova, tazama chini ya kichwa kikuu “Yehova Mungu,” kisha kichwa kidogo “Sifa za Yehova.”)