Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • wp24 Na. 1 kur. 14-15
  • Mema na Mabaya: Uamuzi Unaopaswa Kufanya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mema na Mabaya: Uamuzi Unaopaswa Kufanya
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2024
  • Habari Zinazolingana
  • Je, Viwango vya Biblia Kuhusu Mema na Mabaya Bado Vinafaa?
    Habari Zaidi
  • Mtumikie Yehova Kulingana na Viwango Vyake vya Juu
    Izingatie Siku ya Yehova Maishani
  • Viwango vya Yehova Vinatusaidia
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
  • Watu wa Yehova Wanapenda Uadilifu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2022
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2024
wp24 Na. 1 kur. 14-15
Kijana aliyeonyeshwa katika makala zilizopita anatazama kwa furaha baada ya kufika kwenye kilele cha mlima.

Mema na Mabaya: Uamuzi Unaopaswa Kufanya

Viwango vya maadili tunavyochagua maishani vitaathiri jinsi maisha yetu yatakavyokuwa. Yehova Mungu anajua jambo hilo. Kwa sababu hiyo, anataka tuishi kulingana na viwango vyake.

Yehova anataka tuwe na maisha yenye furaha na amani.

“Mimi, Yehova, ni Mungu wako, Ninayekufundisha ili ujifaidi mwenyewe, Ninayekuongoza katika njia unayopaswa kutembea. Laiti ungesikiliza amri zangu! Ndipo amani yako ingekuwa kama mto na uadilifu wako kama mawimbi ya bahari.”—Isaya 48:​17, 18.

Akiwa Muumba Wetu, Mungu anajua njia bora zaidi ya kuishi. Anatusihi tufuate mwongozo wake kwa sababu utatunufaisha. Tukifuata amri za Mungu, maamuzi yetu yatakuwa na matokeo mazuri. Tutafanya maamuzi mazuri yatakayotuletea amani na furaha.

Yehova hatuambii tufanye mambo yasiyowezekana.

“Amri hii ninayowaamuru leo si ngumu sana kwenu, wala haiko mbali msiweze kuifikia.”—Kumbukumbu la Torati 30:11.

Ili kuishi kulingana na viwango vya Mungu vya maadili huenda tukahitaji kubadili jinsi tunavyofikiri na kutenda. Hata hivyo, Yehova hatuambii tufanye mambo yasiyowezekana. Kwa kuwa yeye ni Muumba wetu, anajua uwezo wetu. Kadiri tunavyoendelea kumjua Yehova, tunagundua kwamba “amri zake si mzigo mzito.”—1 Yohana 5:3.

Mashahidi wa Yehova wakimfundisha mwanamke Biblia kwa kutumia kitabu, “Furahia Maisha Milele! ”

Yehova anaahidi kuwasaidia wale wanaoamua kuishi kulingana na viwango vyake.

“Mimi, Yehova Mungu wako, ninaushika kwa nguvu mkono wako wa kulia, Mimi ninayekuambia, ‘Usiogope. Nitakusaidia.’”— Isaya 41:13.

Tunaweza kuishi kulingana na viwango vya Mungu kwa sababu atatusaidia kufanya hivyo. Anatupatia msaada kupitia Neno lake, Biblia, ambalo linatutia moyo na kutupa tumaini.

Mamilioni ya watu ulimwenguni wamejionea kwamba wanapoishi kulingana na viwango vya Biblia maisha yao yanakuwa bora. Tunakutia moyo ujifunze zaidi kuhusu ushauri mzuri ulio katika Biblia. Unaweza kuanza kwa kuchunguza broshua Furahia Maisha Milele! inayotegemea Biblia na inapatikana bila malipo kwenye jw.org. Ina masomo yafuatayo:

  • Biblia Inawezaje Kukusaidia?

  • Biblia Inatupatia Tumaini

  • Je, Unaweza Kuiamini Biblia?

Unapochunguza Neno la Mungu, Biblia, utagundua kwamba halijapitwa na wakati; ‘linategemeka sikuzote, sasa na milele.’ (Zaburi 111:8) Kufuata viwango vya maadili vilivyo katika Biblia ndio njia bora zaidi ya kuishi. Hata hivyo, Mungu hatulazimishi kuvifuata. (Kumbukumbu la Torati 30:​19, 20; Yoshua 24:15) Ni uamuzi ambao kila mmoja wetu anapaswa kujifanyia.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki