MRADI WA KUJIFUNZA
Watu wa Kiroho Hufanya Maamuzi Yenye Hekima
Soma Mwanzo 25:29-34 ili ujifunze ikiwa Esau na Yakobo walifanya maamuzi yenye hekima.
Chimba zaidi kwenye muktadha. Ni jambo gani lilitukia mapema? (Mwa. 25:20-28) Ni jambo gani lilitukia baadaye?—Mwa. 27:1-46.
Chimba zaidi katika habari hususa. Katika siku hizo, mzaliwa wa kwanza alikuwa na haki na majukumu gani?—Mwa. 18:18, 19; w10 5/1 13.
Je, sikuzote mtu alihitaji kuwa mzaliwa wa kwanza ili awe babu wa Masihi? (w17.12 14-15)
Tafakari mambo ambayo umejifunza na uyatumie. Kwa nini Yakobo alithamini zaidi haki ya mzaliwa wa kwanza kuliko Esau? (Ebr. 12:16, 17; w03 10/15 28-29) Yehova alihisije kuhusu ndugu hao wawili, na kwa nini? (Mal. 1:2, 3) Esau angeweza kufanya jambo gani tofauti ili afanye maamuzi mazuri zaidi?
Jiulize hivi, ‘Ninawezaje kuonyesha kwamba ninathamini mambo ya kiroho inapohusu ratiba yangu ya kila juma, kama vile ninapopanga muda wa ibada ya familia?’