Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w24 Septemba uku. 19
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2024
  • Habari Zinazolingana
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
  • Yesu Awatuma Wanafunzi 70 Wakahubiri
    Yesu—Njia, Kweli, na Uzima
  • Kutii Maneno ya Yesu ya Kuaga
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1996
  • “Siku Hii Itakuwa Ukumbusho Kwenu”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2024
w24 Septemba uku. 19
Yesu akianzisha Mlo wa Jioni wa Bwana akiwa pamoja na mitume wake waaminifu.

Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Yesu alipoanzisha Mlo wa Jioni wa Bwana, wanafunzi 70 ambao awali alikuwa amewatuma kuhubiri walikuwa wapi? Je, walikuwa wamemwacha?

Hakuna sababu ya kufikiri kwamba wale wanafunzi 70 hawakukubaliwa na Yesu au kwamba walimwacha kwa kuwa hawakuwa pamoja naye alipoanzisha Mlo wa Jioni wa Bwana. Yesu alitaka tu kuwa na mitume wake katika pindi hiyo.

Aliwakubali wale mitume 12 na pia wale wanafunzi 70. Yesu alichagua kwanza wanaume 12 kati ya wanafunzi wake wengi, naye aliwaita wanaume hao mitume. (Luka 6:​12-16) Alipokuwa Galilaya, “akawaita . . . wale 12” na “akawatuma kuhubiri kuhusu Ufalme wa Mungu na kuponya.” (Luka 9:​1-6) Baadaye, alipokuwa Yudea, Yesu “akachagua wengine 70, akawatuma wawili wawili.” (Luka 9:51; 10:1) Kwa hiyo, Yesu alikuwa na wafuasi katika maeneo mbalimbali ambapo ujumbe wake ulikuwa ukihubiriwa.

Wayahudi waliokuwa wanafunzi wa Yesu bado wangeadhimisha Pasaka ya kila mwaka, inawezekana wakiwa pamoja na familia zao. (Kut. 12:​6-11, 17-20) Muda mfupi kabla ya kifo chake, Yesu na mitume wake walienda Yerusalemu. Lakini Yesu hakuwaita wanafunzi wake wote kutoka Yudea, Galilaya, na Perea waje kusherehekea Pasaka pamoja wakiwa kikundi kikubwa. Ni wazi kwamba Yesu alitaka kuwa pamoja na mitume wake katika pindi hiyo. Aliwaambia hivi: “Nimetamani sana kula Pasaka hii pamoja nanyi kabla sijateseka.”—Luka 22:15.

Alikuwa na sababu nzuri ya kufanya hivyo. Baada ya muda mfupi Yesu angekufa akiwa “Mwanakondoo wa Mungu ambaye huondoa dhambi ya ulimwengu.” (Yoh. 1:29) Hilo lingetokea Yerusalemu, mahali ambapo dhabihu zilikuwa zikitolewa kwa Mungu kwa muda mrefu. Kifo cha Yesu kingetokeza ukombozi mkubwa zaidi kuliko ule uliopatikana kupitia mwanakondoo aliyeliwa na Waisraeli usiku ambao walitoka Misri. (1 Kor. 5:​7, 8) Dhabihu ambayo Yesu alitoa ingewawezesha wale mitume 12 kuwa sehemu ya msingi wa kutaniko la Kikristo. (Efe. 2:​20-22) Inapendeza kwamba lile jiji takatifu Yerusalemu lina “mawe ya msingi 12” ambayo juu yake yameandikwa “majina 12 ya mitume 12 wa Mwanakondoo.” (Ufu. 21:​10-14) Naam, mitume waaminifu wangekuwa na wajibu mkubwa katika kutimizwa kwa kusudi la Mungu. Hivyo, inaeleweka kwamba Yesu alitaka kuwa pamoja nao kwenye Pasaka hiyo ya mwisho na kwa ajili ya jambo ambalo lingefuata muda mfupi baadaye, yaani, Mlo wa Jioni wa Bwana.

Wale wanafunzi 70 na wanafunzi wengine hawakuwa pamoja na Yesu katika mlo huo. Hata hivyo, wanafunzi wote waliothibitika kuwa waaminifu wangenufaika na jambo ambalo Yesu alianzisha—Mlo wa Jioni wa Bwana. Wanafunzi hao wote ambao baadaye wangekuwa Wakristo watiwa-mafuta wangeingia katika agano la ufalme, ambalo Yesu alilitaja alipokuwa na mitume wake usiku huo.—Luka 22:​29, 30.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki