DOKEZO LA KUJIFUNZA
Tumia Vizuri Kioo
Mwanafunzi Yakobo alilinganisha Biblia na kioo kinachotusaidia kuona utu wetu wa ndani. (Yak. 1:22-25) Tunawezaje kuitumia Biblia vizuri kama kioo?
Isome kwa makini. Ikiwa tutajitazama haraka na kuondoka, huenda tukashindwa kuona tatizo kubwa tulilo nalo. Ili tuone sehemu za utu wetu wa ndani tunazopaswa kurekebisha, inafaa tuchunguze Neno la Mungu kwa kulisoma kwa makini.
Jitazame zaidi kuliko unavyowatazama wengine. Mara nyingine, tunapojitazama katika kioo tunaweza kuwaona watu wengine walio nyuma yetu na huenda tukaanza kukazia fikira kasoro zao. Vivyo hivyo, tunaweza kusoma Biblia na kuanza kufikiria kasoro ambazo wengine wanahitaji kurekebisha. Lakini hilo halitatusaidia kurekebisha kasoro zetu wenyewe.
Uwe na usawaziko. Huenda tukavunjika moyo ikiwa tutakazia fikira kupita kiasi kasoro tulizo nazo. Tunahitaji kuwa na usawaziko tunaposoma Neno la Mungu kwa kutotarajia mengi zaidi ya yale ambayo Yehova anatarajia tutimize.—Yak. 3:17.