DOKEZO LA KUJIFUNZA
Nufaika Kutokana na Marejeo ya Pambizoni
Marejeo ya pambizoni katika Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya yanaonyesha jinsi Biblia inavyopatana kwa kukuelekeza kwenye maandiko yaliyo na habari za ziada. Ili kupata marejeo ya pambizoni, tafuta kwanza herufi ndogo kando ya neno. Katika Biblia iliyochapishwa, tafuta herufi inayofanana na iliyo kando ya neno kwenye sehemu ya katikati au pembeni ya ukurasa ili kupata maandiko yanayohusiana. Katika tovuti ya jw.org au programu ya JW Library®, bofya herufi hiyo ili kuona maandiko yanayorejelewa.
Marejeo ya pambizoni yanaweza kukupeleka kwenye mambo yafuatayo na mengine zaidi:
Simulizi Linalolingana: Rejeo litakupeleka katika simulizi kuhusu tukio lilelile katika kitabu kingine cha Biblia. Kwa mfano, tazama 2 Samweli 24:1 na 1 Mambo ya Nyakati 21:1.
Nukuu: Rejeo linaonyesha chanzo cha maneno hayo. Kwa mfano, tazama Mathayo 4:4 na Kumbukumbu la Torati 8:3.
Unabii Uliotimizwa: Rejeo linakupeleka kwenye utimizo wa unabii. Kwa mfano, tazama Mathayo 21:5 na Zekaria 9:9.