1988 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
YEYE alikuwa na umri wa miaka 33 tu wakati maisha yake yalipokatishwa kwa kuuawa. Na bado, miaka 1,900 baadaye, ujumbe wake ungali unaishi! Jina lake lilikuwa Yesu Kristo. Punde kuliko siku tatu kabla ya kifo chake chenye maumivu makali, alipokuwa anaketi katika shamba la mizeituni kwenye kilima kuelekea Yerusalemu, yeye alisema unabii ambao utimizo wao unamkabili kila mmoja anayeishi leo kukiwa na uchaguzi wa uhai au kifo. Yeye alitabiri kwamba zile “habari njema” za Ufalme wa Mungu zingehubiriwa katika dunia yote inayokaliwa.—Mt. 24:14.
Kukubali habari njema hizo leo kunamaanisha uhai wa milele; kuzikataa—kunaleta kifo cha milele. (Ufu. 14:6, 7) Kama Yoshua wa kale, watu wanaotamani uhai lazima wachague kumtumikia Yehova. (Yos. 24:15) Faida za Ufalme wa Mungu lazima zichukue mahali pa kwanza katika maisha zao. (Mt. 6:33) Lakini ujumbe huu muhimu ungeenezwaje?
Maagizo ya Yesu kwa wafuasi wake yalikuwa mepesi na ya moja kwa moja: Hubirini na kufundisha. Yeye alitaka wanafunzi wake waige yale ambayo yeye mwenyewe alifanya. (Mt. 4:23; 9:35) Iliwapasa wao wawe wahubiri wa habari njema za Ufalme; kazi ya kuhubiri Ufalme yenye kuelekezwa kwa roho ingekuwa ndiyo nguvu yenye kusukuma Ukristo wa kweli. Hivyo, utimizo wa Mathayo 24:14 umesogeza mbele ujumbe wa Ufalme wa Mungu kwenye sehemu ya mbali zaidi sana ya dunia.
Ni nani wanaotimiza kazi hii tukufu leo? Ni Mashahidi wa Yehova. Kumbukumbu letu la kuhubiri Ufalme kwa zaidi ya miaka 100 lajisemea lenyewe. Sisi tunafuata kiolezo kile kile na kutumia kichwa cha habari kile kile katika kuhubiri na kufundisha kwetu kama wanafunzi wa Kristo walivyofanya katika karne ya kwanza. Ripoti yetu ya sasa inathibitisha kwamba sisi hatukupunguwa mwendo katika kazi hii.
“WEWE UMEFANYA KULE KUSHANGILIA KUWE KUKUBWA”
Mashahidi wa Yehova wanavuna kwa roho ya kushangilia. Kama ilivyosemwa kwenye Isaya 9:3, NW: “Wewe umefanya lile taifa liwe na watu wengi; kwalo wewe umefanya kule kushangilia kuwe kukubwa. Wao wameshangilia mbele zako kama kule kushangilia katika wakati wa mavuno, kama wale ambao wanajawa shangwe wakati wao wanagawanya nyara.” Sisi tunashangilia kwamba Yehova amebariki kazi yetu ya kuhubiri na kufanya wanafunzi kwa kuwa na wafanya kazi wa Ufalme zaidi na kwamba yeye ametupa sisi vifaa tuwasaidie. Hivyo, ripoti ifuatayo inatupa sisi sababu zenye kutokeza za kuwa wenye kushangilia!
Wakati wa mwaka wa utumishi uliopita, kwa wastani kila mwezi Mashahidi wa Yehova 3,237,751 walikuwa wakihubiri kwa bidii wakiwa na kilele cha wahudumu 3,395,612. Katika muda wa mwaka mmoja, sisi tulitumia jumla yenye kustaajabisha ya saa 739,019,286—ulingano wa miaka 84,000—ya kuhubiri Ufalme!
Mashahidi wa Yehova ni walimu pia. Ni nini kusudi la kufundisha kwa Kikristo? Kufanya wanafunzi waliobatizwa wa Kristo. (Mt. 28:19, 20) Na kwa kuwa Yesu Kristo aliabudu Yehova, wanafunzi wake lazima pia wawe waabudu wa Yeye.
Katika mwaka wa utumishi wa 1987, 230,843 walibatizwa wakiwa Mashahidi wa Yehova na wanafunzi wa Yesu Kristo. Ule uwezekano wa kupata wanafunzi zaidi ni mkubwa, kwa kuwa sisi tuliongoza kwa wastani mafunzo ya Biblia 3,005,048 kila mwezi. Acheni sasa tuchukue mtazamo wa haraka wa kuzunguka ulimwengu kwenye baadhi ya mambo makuu ya kitheokrasi ambayo pia yatatufanya tushangilie.
Mwaka wa utumishi uliopita ulileta matokeo bora katika Ufaransa, kukiwa na vilele vifuatavyo katika Mei: wahubiri 96,954—kutia mapainia wasaidizi 10,180 na mapainia wa kawaida 3,411. Hiki kilikuwa kilele cha 22 mfululizo kwa mapainia wa kawaida. Wakati wa Mei, asilimia ipatayo 15 ya jumla ya wahubiri walikuwa katika namna fulani ya utumishi wa wakati wote. Pia, wahubiri walitumia wastani wa saa 12.9 katika huduma na wakaripoti kilele cha mafunzo ya Biblia 65,806 katika pindi ya mwezi ule ule.
Mwaka wa utumishi wa Ureno umekuwa umebarikiwa kwa vilele vipya vya wahubiri katika nchi zote na maeneo ambako tawi linasimamia kazi ya kuhubiri Ufalme. Ureno pekee ilikuwa na vilele saba vya wahubiri, ikipita alama ya 32,000 kwa mara ya kwanza. Tukio lenye kutokeza ni kwamba hesabu ya mafunzo ya Biblia ya nyumbani yanayoongozwa sasa inapita hesabu ya wahubiri katika tano za nchi hizo na maeneo yanayoripoti kwenye tawi hili. Ni matazamio yenye kusisimua kama nini yaliyoko mbele kwa mavuno mengi!
“Sisi ni wenye shukrani kwa Yehova kwamba tuliweza kuwa na mwaka mwingine wa utendaji wenye kubarikiwa,” lasema tawi la Japani. Wakati wa mwaka wa utumishi, makundi mapya 125 yaliundwa katika Japani. Hesabu ya wahubiri wa Ufalme iliongezeka kufika 120,722 katika Agosti—kilele cha 104 mfululizo kila mwezi. Lililokuwa lenye kutia moyo zaidi ilikuwa hesabu ya mafunzo ya Biblia ya nyumbani. Katika Juni 166,277 yaliongozwa—ongezeko la asilimia 14 juu ya wastani wa mwaka uliopita. Ile broshua mpya “Tazama! Mimi Nafanya Vitu Vyote Kuwa Vipya” ilithibitika kuwa kifaa chenye matokeo sana katika Japani kwa kufanya ziara za kurudia na kuanzisha mafunzo ya Biblia ya nyumbani.
Katika Mei, ule mwezi wa mapinduzi ya kijeshi katika nchi hiyo, tawi la Fiji lilishuhudia kilele chalo mfululizo cha 29 katika wahubiri. Juni uliona kilele kingine cha wahubiri zaidi ya 1,300 katika shamba. “Yote ambayo ninyi watu mmekuwa mkituambia katika wakati uliopita yanatimia,” inspekta mmoja wa polisi akakiri kwa Shahidi mmoja. “Kama watu wote katika nchi hii wangekuwa Mashahidi wa Yehova, sisi hatungekuwa na msukosuko huu.”
Kwa mara ya kwanza, ile tarakimu ya wahubiri ilipita 45,000 katika Australia, na karibu kila mwezi uliona kilele kipya katika mapainia wa kawaida. Wahubiri walikuwa wenye bidii kwa utumishi wa shambani, hasa katika Aprili wakati wao walifanya wastani wa saa 12.1.
Tangu 1947, uhamaji kutoka nchi za ng’ambo umesababisha karibu asilimia 40 ya ukuzi wa idadi ya watu wa Australia. Nchi za Ulaya za Uingereza, Ailandi, Italia, Yugoslavia, Ugiriki, Ujeremani, Uholanzi, na Polandi ndizo ambazo zimekuwa wachangiaji wakuu. Kwa sababu ya mmiminiko huu, makundi 58 yenye lugha za kitaifa na vikundi 39 yameundwa. Wao wanafurahia kuwa na mikutano kwa ukawaida pamoja na programu za makusanyiko ya mzunguko na mikusanyiko ya wilaya zilizopangwa katika lugha 20 mbalimbali.
Hivi majuzi zaidi, Australia imeona mmiminiko wa wakimbizi kutoka Vietnam, Laos, Kampuchea, Thailandi, na nchi nyinginezo za Esia Kusini-mashariki. Walio wengi wa watu hawa wamepatwa na mateso makali na kupungukiwa mahitaji. Sasa kwa kuwa wao wanaishi katika mazingira yaliyo thabiti zaidi, wengi wao wanaitikia zile habari njema. Mathalani, katika Sydney wahubiri 124 na mapainia 24 wanafanyiza kundi ambalo lina idadi kubwa ya Waesia katika eneo lalo. Kundi hili linafurahia mafunzo ya Biblia yalo 220. Tawi linatoa elezo hili, “Kweli kweli, umati mkubwa kutoka mataifa yote unakusanywa uje uokolewe!”
Katika nchi moja ya Afrika ambako kazi ya Mashahidi wa Yehova imekuwa chini ya marufuku kwa karibu miaka 20, makundi mapya 17 yameundwa katika mwaka wa utumishi uliopita. Makundi yalipata ongezeko la asilimia 18 katika wastani wa hesabu ya mapainia wasaidizi. Mapainia wasaidizi hao wenye shughuli nyingi walivuna nini? Mafunzo ya Biblia zaidi yanaongozwa—ongezeko la asilimia 22!
Zambia ilifikia kilele kipya cha wahubiri 67,144 katika Aprili—asilimia 16.5 kupita wastani wa mwaka jana. Wengi zaidi wanashiriki katika huduma ya painia pia. Mapainia wa kawaida waliongezeka asilimia 13.5 na mapainia wasaidizi waliongezeka asilimia 20.5 ikilinganishwa na mwaka mmoja uliopita. Wakati wa mwaka tawi liliandikisha kundi la namba 1,715, ongezeko la makundi 93 tangu mwanzo wa mwaka wa utumishi wa 1987.
Painia mmoja katika Kanda ya Shaba ya Zambia aligundua njia tofauti ya kufanya habari njema zivutie wengine. Yeye anasema: “Mimi sikuzote nimejaribu kuongea na mfanya-kazi mwenzangu juu ya habari njema za Ufalme, lakini yeye alikataa katakata kuchukua kitabu au gazeti lo lote. Siku moja mimi nilichukua kalenda yetu yenye kupendeza kazini na kumwonyesha yeye wakati wa chakula cha mchana. Yule mwanamume akapaaza sauti, ‘Lo! ni kalenda yenye sura nzuri kama nini!’ Yeye alivutiwa sana hivi kwamba hata alikubali funzo la Biblia na anafanya maendeleo mazuri ya kiroho.”
Jambo kuu la mwaka katika Burkina Faso lilikuwa ule uamuzi wa kutumia zaidi ile lugha ya kienyeji Moore katika kufundisha makundi. Tangu Februari, makala za funzo zilizochaguliwa kutoka Mnara wa Mlinzi zimetafsiriwa na kuchapishwa katika toleo la kila mwezi. Baadaye, Huduma ya Ufalme Yetu ilitafsiriwa pia. Hivyo, tisa ya yale makundi yenye kusema Kifaransa yalipanga kwa shangwe mikutano yao iongozwe katika lugha ya Moore.
MAGAZETI—YASAIDIA KATIKA KUHUBIRI UFALME
Wahubiri katika Liberia wamekuwa wakifanya wastani wa saa 15.4 kila mwezi katika huduma ya shambani, hiyo ikitokeza kilele kinachostahili kuangaliwa katika mwenezo wa magazeti. “Magazeti 17,630 yakiwa yameenezwa, magazeti zaidi yaliwekwa mikononi mwa watu zaidi ya mwezi mwinginewo wote tangu Machi 1972,” laandika tawi hilo. “Ile sura yenye kuvutia ya magazeti yetu yenye kurasa nzima-nzima zenye rangi bila shaka imechochea utendaji wa magazeti katika nchi hii. Wahubiri wanaona kwamba akiba yao imekwisha baada ya siku chache za kupokea matoleo mapya. Mara nyingi watu wanawafikia wahubiri barabarani na kuwauliza, ‘Je! mna zile “Biblia” zo zote kwa ajili yangu?’—kumaanisha Mnara wa Mlinzi na Amkeni!”
“Magazeti yetu yakiwa yanachapishwa katika rangi nne tangu Aprili 1987, wahubiri wengi wamezidisha sana kazi yao ya magazeti,” laripoti tawi la Zimbabwe. Baada ya kupokea mojapo matoleo ya kwanza ya haya magazeti yenye kurasa nzima-nzima zenye rangi, ndugu mmoja kutoka eneo la mashambani la nchi aliandika hivi: “Mimi nilichukua kiasi kimoja na kusimama kwenye kitovu cha biashara ili kuwatolea magazeti wapitaji. Watu wachache walikubali nakala fulani. Walipokuwa wakienda nyumbani, walizionyesha kwa majirani wao, na muda mfupi baada ya hapo kulikuwako na wingi wa watu kutoka ujirani wakija ili wapate magazeti. Katika muda wa dakika chache, kiasi changu kilikuwa kimekwisha.”
Katika kundi moja la Côte d’Ivoire (Ivory Coast), baada ya kumaliza kujifunza juu ya kutoa ushuhuda kwa magazeti katika toleo la Machi 1, 1987, la Mnara wa Mlinzi, ndugu wawili waliamua kutumia baadhi ya madokezo wakiwa njiani kutoka kwenye Jumba la Ufalme. Kwa idili wao walianza kutoa magazeti kwa kila mmoja waliyekutana naye njiani. Kufikia wakati walipofika nyumbani mwao, walikuwa wameangusha magazeti 20.
Wahubiri fulani wanajaribu njia mpya ili kuangusha maandikisho. Katika Ajentina ndugu mmoja aliamua kumpelekea mwanafunzi wake wa Biblia buku lake lililojalidiwa la gazeti la Amkeni! na kumwonyesha vichwa vya habari mbalimbali vilivyozungumzwa wakati wa mwaka. Yule mwanafunzi wa Biblia alivutiwa na habari yote hiyo iliyotolewa. Yeye alikuwa ndipo tu amegharimia vitabu fulani vilivyokuwa vimezungumzia vichwa vya habari ambavyo vilihusiana na hizo kwa dola zipatazo 24. Sasa yeye angeweza kupata habari ile kutoka kwa magazeti yetu kwa dola 5 tu kwa andikisho la mwaka mmoja. Bila uhitaji wa kusema, yule ndugu aliangusha andikisho.
HADHIRINA YA UKUMBUSHO YENYE KUTOKEZA!
Katika Aprili 12, 1987, katika wakati ulio punde kuliko ule uliochukua mzunguko mmoja wa dunia kwenye mhimili wayo, Mashahidi wa Yehova na wakaribishwa wao 8,965,221 wasemao zaidi ya lugha 160, walikusanyika katika nchi 210 kuadhimisha Chakula cha Bwana cha Jioni. Matawi ya Mnara wa Mlinzi yamepeleka ripoti fulani zenye kusisimua.
Hadhirina ya Ukumbusho ya El Salvador ilikuwa 58,933. Kwa kuwa kilele cha hesabu ya wahubiri kwa mwaka ule kilikuwa 16,041 wakati wa mwezi Mei, kungali kuna kazi nyingi ya kufanywa kule. Belize jirani ya El Salvador ilikuwa na hadhirina ya Ukumbusho yenye kutokeza pia. Jumla ya watu 3,928 walikusanyika, ambayo ni mara tano ya kilele cha hesabu ya wahubiri! Hili lamaanisha kwamba kulikuwa yapata mtu mmoja katika hadhirina kwa kila wakazi 44 wa ile nchi.
Hadhirina ya Zambia kwenye Ukumbusho ilikuwa 381,129—asilimia 16 kupita tarakimu ya mwaka jana. Kweli kweli, hesabu kubwa ya watu wanatamani msaada wa kiroho katika nchi hii. Katika Hong Kong 3,583 walihudhuria Ukumbusho, 45,466 walikuwapo katika Ubelgiji, na 198,797 walikusanyika katika Ufaransa—mara mbili hesabu ya wahubiri kwa nchi zote tatu. Na United States iliona watu wapitao 86,000 zaidi wakihudhuria Ukumbusho wa mwaka huu kuliko mwaka jana, jumla ya 1,778,066. Meksiko, ikiwa na kilele cha wahubiri 222,168, ilikuwa na hadhirina ya Ukumbusho yenye kutokeza ya 957,081!
SHULE YA UTUMISHI WA PAINIA
Kukiwa na mapainia wapya zaidi ya 44,000, Shule ya Utumishi wa Painia haijakuwa na matatizo ya uandikisho. Baada ya kuwapo kwa muda wa miaka kumi, shule ile inazidi kuwa na matokeo katika kuzoeza waeneza-evanjeli wa wakati wote. Akasema dada mmoja katika Guyana ambaye ana umri wa miaka 74 na ni mjane, “Ingawa nilikuwa mgonjwa wakati huo, mimi nilikuwa na shangwe ya kuhudhuria Shule ya Utumishi wa Painia.” Ingawa hivyo, ilikuwa jitihada kubwa kwake kuhudhuria. “Kwa sababu mimi nilitembea kwa shida sana,” yeye anaendelea, “mwalimu wa shule angekuja kunichukua kila asubuhi na kuambatana nami kwenye darasa na kunirudisha nyumbani kila alasiri. Kwa kuwa na kitia-moyo kutoka Shule ya Utumishi wa Painia, sasa mimi ninaweza kufanya mengi zaidi katika utumishi.”
Shule ya Utumishi wa Painia hutoa shauri lenye mafaa juu ya jinsi ya kusaidia wanafunzi wa Biblia wafanye maendeleo kuelekea ubatizo. Painia mwingine kutoka Guyana alisema: “Kabla ya mimi kuhudhuria ile shule ya painia, nilikuwa na mwanafunzi wa Biblia ambaye hakuweza kuhudhuria mikutano. Udhuru wake? Sikuzote yeye alikuwa na shughuli mno akifanya kazi za nyumbani. Baada ya kujifunza kwenye shule jinsi ya kuonyesha kupendezwa zaidi kwa kibinafsi katika wengine, mimi nilitia katika zoezi niliyojifunza. Kwenye funzo la Biblia langu lililofuata, mimi nilimtolea yule mwanafunzi wangu shauri lililoleta matokeo mazuri. Kwa kuwa ziara za mara kwa mara kutoka kwa marafiki na watu wa ukoo zilimzuia kumaliza kazi zake za nyumbani, mimi nilidokeza kwamba yeye awaombe wamsaidie baadhi ya kazi za nyumbani. Sasa mwanafunzi wangu ana wakati si wa mikutano tu bali pia wa huduma ya shambani.”
Katika Lebanoni, Desemba 1986 ulikuwa mwezi wa kwanza wa Shule ya Utumishi wa Painia tangu 1978. “Sisi hatukuwa na kikundi cho chote kikubwa vya kutosha mbeleni kuwa na darasa,” yaeleza afisi ya tawi. “Lakini kwa baraka ya Yehova, roho ya kupainia ilienea haraka sana hivi kwamba sisi tulikuwa na mapainia wa kutosha wanaostahili kujaza darasa moja.”
Painia mmoja ambaye alithamini kuhudhuria shule katika Zambia aliandika: “Mimi nimekisoma kitabu chote cha painia mara tatu kila mwaka tangu wakati wa ile shule nami nimefanyia maendeleo utumishi wangu sana sana.”
“TUMAINI KATIKA YEHOVA” MIKUSANYIKO YA WILAYA
Kadiri wasiwasi wa kimataifa unavyoongezeka, ndivyo wakati ujao wa ulimwengu unavyokuwa usio na matumaini kwa watu zaidi na zaidi. Kwa sababu gani? Kwa sababu wao wanaweka tumaini lao katika mambo kama vile mali zao, hekima yao, nguvu zao, au viongozi wao wa kisiasa. (Luka 21:25-28) Lakini Mashahidi wa Yehova wana matazamio yaliyo tofauti. Sisi tunauelekea wakati ujao tukiwa na uhakika kwa sababu sisi ‘tunatumaini katika Yehova kwa moyo wetu wote na hatuegemei uelewevu wetu wenyewe.’ (Mit. 3:5, NW) Kwa hiyo lilikuwa jambo la wakati unaofaa kwamba mifululizo ya mikusanyiko ya wilaya ya siku tatu ambayo ilianza katika Juni 1987 ilipasa kukazia kile kichwa “Tumaini katika Yehova.”
Kwenye mikusanyiko 24 katika Jamhuri ya Muungano ya Ujeremani, kilele kipya katika hadhirina kilifikiwa—159,361—wapatao 8,500 zaidi ya mwaka mwinginewo wote uliotangulia. Hesabu ya watu waliobatizwa ilikuwa pia kilele kipya kwa mikusanyiko ya kiangazi—1,455.
Tawi la United States linaripoti: “Sisi tulitiwa moyo kuona hadhirina ya 1,288,313 kwenye ile Mikusanyiko ya Wilaya ya ‘Tumaini Katika Yehova’ 123, kukiwa na ipatayo zaidi ya asilimia moja ya wale katika hadhirina, au 13,562, wakibatizwa. Hii ndiyo mara ya kwanza katika miaka mitano kwamba hesabu ya waliobatizwa imekuwa zaidi ya asilimia 1.”
Katika sehemu fulani za ulimwengu, Mikusanyiko ya Wilaya ya “Amani ya Kimungu” iliyoanza katika sehemu ya pili ya mwaka wa utumishi wa 1986 iliendelea na kuingia katika mwaka wa utumishi wa 1987. Panama na Ghana ni vielelezo viwili.
Akina ndugu katika Panama walikuwa na tatizo. Kwa kuwa msukosuko wa kisiasa ulikuwa ukihangaisha ile nchi, je! mikusanyiko ingeweza kufanywa kwa uhuru? Hali hazikuonekana zikitumainisha. Watu walikuwa wamekuwa wakigomea kazi na kufanya maandamano barabarani, nayo serikali ilikuwa imetuma vikosi vya kuzuia ghasia viwatawanye kwa mabomu ya gesi yenye kutoza machozi. Lawama liliwekwa juu ya Kanisa Katoliki kwa kutumia mimbari zalo kuchochea wanaparokia walalamike. Mathalani, nyusipepa moja ya serikali ilichapisha maandishi makubwa kwenye ukurasa wa mbele ikimshtaki askofu mkuu kwa kukaidi serikali na kuchochea watu waasi. Katika maandishi makubwa kwenye sehemu ya chini ya ukurasa wa mbele yalionekana maneno haya: “‘Dini Katika Siasa—Je! Ni Mapenzi ya Mungu?’ (Ona ukurasa 4).” Kwenye ukurasa 4 wa nyusipepa hii, makala yenye kichwa hicho ilinakiliwa kutoka Amkeni! (Kiingereza) la Aprili 22, 1987 (Kiswahili, Mei 8, 1988). Ilitia ndani picha ya kiongozi wa kidini mmoja akipeana salamu za mkono na dikteta wa Nazi Adolf Hitler.
“Ile makala ya nyusipepa kwa wazi ilichapishwa kuonyesha tofauti iliyoko baina ya msimamo wetu na ule wa Kanisa Katoliki,” laandika tawi la Panama. “Kama tokeo, ingawa mikutano ya siasa ilikuwa imekatazwa kufanyiwa katika sehemu za kufanyia mikutano ya watu wote, katikati ya huu msukosuko wa kisiasa, sisi tuliweza kufanya mikusanyiko yetu ya wilaya tukiwa na hadhirina ya jumla ya watu zaidi ya 10,000.”
Ile Halmashauri ya Tawi la Ghana ilihangaikia kutoa ushuhuda kikamilifu katika maeneo yasiyogawiwa mtu katika sehemu ya kaskazini ya ile nchi. Kwa sababu hiyo, akina ndugu na dada kutoka upande wa kusini walitiwa moyo wahudhurie “Amani ya Kimungu” Mkusanyiko wa Wilaya ulioratibiwa kwa ajili ya mji wa kaskazini wa Tamale. Itikio likawaje? La kustaajabisha!
“Sisi tulitazamia washiriki wapatao elfu moja, baadhi yao tulifikiria wangefanya mipango yao wenyewe ya kusafiri,” yaripoti afisi ya tawi. “Kwa hiyo sisi tuliandikia kampuni ya basi na kuomba mabasi kumi yenye viti 70 kila moja. Lakini wakati fomu za maombi ya nafasi ya kusafiria kutoka kwenye makundi ziliporudi, zaidi ya 3,000 walikuwa wameamua kuhudhuria ule mkusanyiko wa Tamale! Sisi tungepata wapi mabasi ya kuwapeleka wote kwenye ule mkusanyiko?”
Usafirishaji katika Ghana ni haba, na sehemu kubwa ya ile barabara yenye urefu wa kilometa 640 kutoka ule mji wa bandari wa Accra katika upande wa kusini, liliko tawi, kwenda Tamale iko katika hali mbaya. Kwa hiyo makampuni ya basi hayapendi kuchukua ile kazi. Lakini makampuni mawili ya basi yalikubali kukodisha tawi jumla ya mabasi 28. Hata hivyo, mabasi manne zaidi yalihitajiwa.
“Wizara ya Biashara na Utalii ilikuwa imeingiza nchini makochi manne yenye hali ya raha, yenye visawazisha-hewa kwa kusudi la kusitawisha utalii katika Ghana,” yaendelea ripoti ya tawi. “Hata hivyo, ile wizara, ilikuwa imekataa kukodisha yale makochi kwa kikundi cho chote cha utalii. Sisi tulituma ombi la kutaka makochi haya. Mwanzoni lilionekana kuwa jambo lisilo na tumaini. Mwishowe, Jumanne alasiri, kabla tu ya asubuhi ya Jumatano wakati yale makochi yalihitajiwa, waziri alitia sahihi barua ya kuachilia yale mabasi kwetu. Yule mkurugenzi wa utalii kwenye afisi ya waziri aliwaambia hivi wenzake alipoona yule waziri akitia sahihi barua ya kuachilia: ‘Yehova anafanya kazi!’”
Basi akina ndugu wakasafiri pamoja na jamaa zao katika msafara wa mabasi 32. Tamasha hii yenyewe ilikuwa ushuhuda mkubwa mwendo wote kufika Tamale. Hakuna kikundi kingine ambacho kilikuwa kimepata kusafirisha watu wengi hivyo katika wakati mmoja. Watu kote kote njiani walikuwa wanavuma kwa msisimuko, wakisema juu ya mambo ya kushangaza ambayo Mashahidi wa Yehova wanaweza kutimiza.
Kwa kuongezea, chapa ya Ghana ya Huduma ya Ufalme Yetu iliwatia moyo akina ndugu waliokuwa wakienda Tamale kuhakikisha kwamba wanatumia angalau saa moja kila siku katika utumishi wa shambani, ama kabla ama baada ya vipindi vya mkusanyiko. Kwa hiyo saa moja asubuhi moja, ndugu wawili walitembelea ile nyumba ya wageni walimokuwa wamepewa makao washiriki watatu wa Halmashauri ya Tawi waliokuwa wanahudhuria ule mkusanyiko. Walisema: “Kina ndugu, sisi tunafanya kazi katika eneo hili na tumeishiwa vitabu. Je! ninyi mna cho chote tunachoweza kutumia ili tuweze kuendelea?”
Kwa hiyo, Tamale, mji ambao wakazi wao sana sana ni Waislamu wenye idadi ya watu 146,000, ulienezwa kikamili kwa ushuhuda wa nyumba kwa nyumba. Hata mafunzo ya Biblia yalianzishwa. Kilele cha hadhirina cha watu 4,220 huonyesha kwamba watu wengi wenye kupendezwa kutoka mji ule walihudhuria mkusanyiko. Ile ripoti ya tawi ilimalizia hivi: “Sisi tunatumaini kweli kweli kwamba yale makundi mawili ya Tamale yatafanya kazi nzuri ya kutilia maji zile mbegu zilizopandwa kwa wingi sana na kwamba katika wakati wake mwenyewe, Yehova atazifanya zikue.”—1 Kor. 3:6.
‘KUTIWA TAJI KWA WEMA’ KWATOKEZA MPANUKO
“Wewe umetia taji mwaka kwa wema wako,” akaandika mtunga zaburi. (Zab. 65:11, NW) Jitihada za ndugu zetu katika shamba ‘zilitiwa taji’ kwa maongezeko ambayo yamefanya ihitajiwe kabisa kuwe na Majumba ya Ufalme na ujenzi wa upanuzi wa tawi. Vifuatavyo ni vielelezo vichache:
Ikiwa na mwaka mwingine mzuri ajabu wa utendaji nyuma yayo, Meksiko inatazamia kwa furaha mwaka wa utumishi wenye kusisimua katika 1988. Ujenzi wa jengo jingine jipya la Betheli la vyumba 126 tayari unaendelea vizuri sana. Jengo kubwa linaongezwa pia kwenye matbaa ya sasa. Na Meksiko ndilo tawi la kwanza kuweka mashine mbili mpya za kupigia chapa za rangi nne na mashine mbili za kujalidi sawia. Miradi yote hii yapasa imalizwe wakati wa mwaka mpya wa utumishi.
Ujenzi wa Ureno wa Kao la Betheli jipya waendelea kuchukua sehemu kubwa ya programu ya ujenzi wao. “Kufikia leo hii,” yasema ripoti ya tawi, “gharama zote za ujenzi zimelipwa kwa michango ya wenyeji.” Hii ilitia ndani thamani ya vitu na mali nyingi za kibinafsi. Vifaa vya ujenzi vya kila namna, pamoja na nguruwe, kuku, kondoo, na bata, pia vilifanywa vipatikane.
Si miaka mingi sana iliyopita katika Kolombia, ilionwa kuwa vema ikiwa makundi mapya 15 yangeongezwa wakati wa mwaka. Sasa katika siku moja tu, Idara ya Utumishi ilipokea maombi 13 kwa ajili ya makundi mapya katika ule mji mmoja tu wa pwani wa Barankwila! Wakati wa kipindi cha mwaka wa utumishi uliopita, makundi mapya 143 yameundwa katika nchi hiyo.
Miaka ipatayo 30 iliyopita, ule mji wa Medellín ulijulikana kuwa kitovu cha Ukatoliki katika Kolombia, na ile nchi ilijigamba kwamba asilimia 99 ya idadi yayo ya watu walikuwa Wakatoliki. Kwa sababu ya kushuka kwa maadili, mauzo haramu ya dawa za kulevya, na kupungua kwa imani ya idadi ya watu wao, Medellín sasa ni mojapo majiji yanayokosa usalama sana katika ile nchi. Mabadiliko haya yamefanya watu wengi wenye mioyo myeupe kuitikia ifaavyo kuhubiriwa kwa habari njema. Sasa kuna makundi 35 katika na kuzunguka Medellín. “Ongezeko lote hili limesababisha ‘dharura’ za Majumba ya Ufalme,” lasema tawi. Walilofanya akina ndugu wenyeji katika mji mdogo wa Segovia, si mbali na Medellín, hutoa kielezi cha nia yao ya kutaka kukabiliana na hali hii ya dharura.
Mwangalizi wa Wilaya aliripoti hivi: “Katika Segovia kuna konzi la wahubiri 32. Kati ya jumla hii, 17 ni akina dada, wote wakiwa wafanya kazi wenye bidii. Mwaka mmoja uliopita kikundi hiki kidogo kilinunua kisehemu cha ardhi, wakaanza kutengeneza matufali yao wenyewe yenye saruji ya kujengea, na wakakusanya vifaa vingine kwa ujenzi wa Jumba la Ufalme. Mwangalizi wa mzunguko alikuwa amezuru muda mfupi baada ya kile kisehemu cha ardhi kununuliwa. Aliporudi miezi mitano baadaye, alishtuka kama nini kuona jumba lililomalizika! Kazi yote ilikuwa imefanywa siku za Jumamosi, Jumapili, na wakati wa usiku.” Lile jumba hata ni kubwa vya kutosha kufanyiwa kusanyiko la mzunguko dogo. La kwanza lililofanyiwa pale lilikuwa na 263 katika hadhirina, kukiwa na watu watano waliobatizwa.
Mlipuko mmoja wa volkano ukifuatwa na mmomonyoko wa matope wenye kuua ulikumba eneo kuzunguka Armero, Kolombia. Udugu wetu wa ulimwenguni pote uliitikia kwa njia ya kupenda. Baada ya mahitaji ya kimwili ya waliookoka kutimizwa, Baraza Linaloongoza lilitoa kibali kwa tawi kutumia fedha zilizobaki kutimiza masilahi ya kiroho ya akina ndugu. Kwa hiyo, Majumba ya Ufalme yanayofaa yalijengwa katika eneo lile lililoathiriwa na volkano ili kwamba elimu ya kiroho ingeweza kuendelea bila kukatizwa.
Kundi la La Dorada lilikuwa mojapo makundi matatu yaliyokuwa yakipokea msaada wa kimataifa kusaidia katika ujenzi wa Jumba la Ufalme jipya. Kazi nyingi ya ujenzi ilifanywa na akina dada na watu wenye kupendezwa, kwani kulikuwako wanaume waliobatizwa sita tu katika kundi lile. Hata hivyo, msaada wenye upendo uliandaliwa na kikundi cha akina ndugu kutoka Bogotá. Na katika muda uliopungua wiki moja, La Dorada likawa na Jumba la Ufalme jipya. Ujenzi ulianza Alhamisi, na jioni ya Jumatatu iliyofuata, walifanya mkutano wao wa kwanza, wakiwako 200 katika hadhirina. Mipango ilifanywa pia kwa majumba mapya katika Mariquita na Lérida. Baada ya kuokoka uharibifu wa ukuta wa matope wa volkano wenye kwenda kasi, Wakolombia wengi sasa wanatafuta maji yenye kuburudisha ya ukweli.
Ili kuangalia umayamaya mkubwa wa waabudu katika Ajentina, makundi mapya 121 yaliundwa wakati wa mwaka wa utumishi—wastani wa makundi 10 kila mwezi! Katika mahali pengi, Majumba ya Ufalme ni madogo mno, na kwingine kuna makundi manne au matano yanayokutana katika jengo lile lile. Tawi lilianzisha mfuko wa Jumba la Ufalme na upesi litaanza kutoa mikopo kwa majumba mapya. Mipango ya pekee sasa inafanywa kuunganisha pamoja wafanya kazi na michango ya makundi ili kumaliza hesabu kadhaa ya Majumba ya Ufalme na kisha kuanza kujenga mengine mapya.
Tawi la Sri Lanka liliona makundi mapya matatu yakipangwa kitengenezo mwaka huu wa utumishi uliopita, moja la hayo katika upande wa kaskazini wenye msukosuko wa kisiasa. Makundi matano yamejenga Majumba ya Ufalme yayo yenyewe. Lile la Chilaw lilimalizwa kwa msaada wa akina ndugu waliokuwa wakizuru kutoka Jamhuri ya Muungano ya Ujeremani.
Mwangalizi wa mzunguko mmoja katika Kerala, India, anaripoti kwamba hivi karibuni makundi mawili yalijenga Majumba ya Ufalme yayo yenyewe. Mojapo haya lina nafasi ya kukaliwa na watu 120. Katika mwaka huu wa kwanza hadhirina ilikua sana hivi kwamba lile kundi linahitaji kufanya vipindi viwili vya mikutano katika nyakati tofauti.
Kuandaa Majumba ya Ufalme ni tatizo kweli kweli katika Taiwan, kwa kuwa makundi yana ugumu wa kukodisha vifaa vinavyofaa, hasa katika majiji. Mara nyingi wakati mahali panapatikana, mwenye-mali anapandisha kodi juu sana baada ya mwaka wa kwanza hivi kwamba akina ndugu hawana budi kuondoka. Katika pindi ya mwaka uliopita, makundi manane—asilimia 38 ya jumla ya makundi yote—ama yamehamia katika Majumba ya Ufalme mapya au yameanza kupata majengo yayo yenyewe. Makundi katika majiji makubwa zaidi yananunua majengo kadhaa ya orofa yaliyo karibu karibu katika sakafu ile ile ya jengo na kuyageuza kuwa Jumba la Ufalme.
Katika United States, hesabu ya makundi iliongezeka kwa 211 kufikia mwisho wa mwaka huu wa utumishi. Hiyo ni wastani ya makundi mapya manne kila juma! Kukiwa na maongezeko haya, Majumba ya Ufalme zaidi yanahitajiwa. Kufikia Desemba 1987, Mfuko wa Majumba ya Ufalme wa Sosaiti uliwezesha fedha zipatikane kwa ujenzi wa Majumba ya Ufalme 387. Katika pindi ya mwaka huo wa utumishi uliopita, majumba 108 yamenufaika na mfuko huu.
MAJUMBA YA UFALME YENYE KUJENGWA HARAKA-HARAKA YAKO KILA MAHALI
Lile wazo la kujenga Majumba ya Ufalme kamili na kuwa tayari kwa ajili ya mikutano katika muda wa siku chache tu lilianza katika United States. Lilisitawishwa na likawa lenye kupangwa zaidi kitengenezo wakati wa mwongo uliopita. Kufikia 1987 wazo hilo lilikuwa limezaa tunda kuzunguka ulimwengu. Mathalani, katika mwisho-juma wa Juni 26-28, 1987, Mashahidi wa New Zealand walianza na wakamaliza Jumba la Ufalme la kwanza lenye kujengwa haraka-haraka katika nchi hiyo katika Kambriji katika Ailandi Kaskazini—na watu waliona.
“Mradi Unaokaribia Kuwa Kama Muujiza” ndiyo yaliyokuwa maandishi makubwa ya ukurasa wa kwanza katika Cambridge Edition, nyusipepa ya mahali hapo. Makala-andamani iliendelea kusema: “Katika Ijumaa ilionekana kama ulimwengu kwa ujumla ulikuwa umehamia Arnold Street. Mashahidi [wa] Yehova wapatao 800 kutoka kote kote Ailandi Kaskazini walishuka kwenye kiwanja fulani na kuendelea kufanyiza kitu fulani kilicho kama muujiza. Wao walianza kujenga Jumba la Ufalme kamili likiwa na bustani yenye mandhari nzuri katika siku mbili na nusu. Na walifanya hivyo! Pengine upande wenye kuduwaza akili zaidi wa kazi hiyo ulikuwa ule mpango wa kitengenezo na kazi kufanywa kwa utulivu kabisa.”
Katika Belize, kikundi kimoja cha wahubiri 13 kilikuwa na hadhirina ya 30 au 40 kwenye mikutano yao katika San Pedro, Ambergris Cay, lakini wao hawakuwa na Jumba la Ufalme. Walikuwa wakikutania kwenye varanda ya kao la ndugu mmoja, kwa hiyo wao waliamua kuendelea na mradi wa Jumba la Ufalme lenye kujengwa haraka-haraka. Hata hivyo, vizuizi vilifunga njia yao. Kwa kuwa wao wako kwenye kisiwa kilicho peke yacho kilometa zipatazo 58 kutoka Jiji Belize, ingewabidi kusafirisha kila kipande cha Jumba la Ufalme lao kwenye kisiwa. Mradi kama huo ulikuwa haujapata kufanywa mbeleni katika Belize. Walipanga kutumia aina fulani ya mbao ngumu sana za kienyeji ambazo zinaweza kustahimili hali. Ilibidi mashimo yatobolewe kwanza kabla ya zile sehemu mbalimbali kuunganishwa pamoja kwa misumari. Ilibidi wale wote waliokuwa wakifanya kazi kwenye mradi huo wavukie huko kwa meli au ndege. Baraka ya Yehova ilikuwa wazi, kwa kuwa lile Jumba la Ufalme lilijengwa na likawekwa wakfu wakiwapo 247 katika hadhirina.
Septemba 1986 ndio mwezi uliowekwa kwa ajili ya Jumba la Ufalme la kwanza lenye kujengwa haraka-haraka la Denmark. Ripoti nzuri juu ya tukio hilo ilitolewa na nyusipepa, redio na televisheni. Tangu hapo, ule mwaka ‘umetiwa taji ya wema’ kwa ujenzi wa majumba saba zaidi yenye kujengwa haraka-haraka.
Katika Uholanzi, kwa muda mrefu ilifikiriwa kwamba Majumba ya Ufalme yenye kujengwa haraka-haraka hayangeweza kujengwa huko kwa sababu ya sheria na amri za serikali. Lakini ushirikiano wa wenye mamlaka na moyo wa kupenda wa akina ndugu ulifanya jumba la kwanza la nchi hiyo lenye kujengwa haraka-haraka liwe fanikio kubwa ajabu. Kama tokeo, kupendezwa kwingi katika ujumbe wa Ufalme kuliamshwa katika eneo hilo la Ulaya.
Kati ya makundi 20 ya Luxembourg, 12 yalihusika katika kujenga Majumba ya Ufalme mapya au kupanua yaliyokuwako wakati wa mwaka huu wa utumishi. Hayo hufanyiza asilimia 60 ya makundi ya nchi hiyo. Upande wa kaskazini tu, Ubelgiji kufikia sasa ina timu mbili za ujenzi nchini ambazo zimesimamisha majumba sita yenye kujengwa haraka-haraka kukiwa na miradi zaidi iliyo tayari kuanzwa. Ni sababu zilizoje za kushangilia!
Kanada, pia ikionyesha ukuzi, ilijenga Majumba ya Ufalme 11 mwakani. Kufikia sasa, Kanada ina jumla ya Majumba ya Ufalme 120 yenye kujengwa haraka-haraka. Tisa ya haya ni majumba maradufu. Jumba la Kusanyiko jipya linaendelea kujengwa katika Montreal, kukiwa na mipango ya kuanza kulitumia kufikia mwisho wa 1987. Kanada sasa ina Majumba ya Kusanyiko manane.
Jamhuri ya Muungano ya Ujeremani ina halmashauri za ujenzi 11. Pindi ya mwaka wa utumishi uliopita, majumba 19 yenye kujengwa haraka-haraka yamejengwa. Majumba ya Ufalme zaidi 62 yamejengwa au yanaendelea kujengwa. Yehova ameutia taji mwaka huu wa utumishi si kwa kazi ya ujenzi wa haraka wa Majumba ya Ufalme 81 tu bali pia kwa kuwekwa wakfu kwa Jumba la Kusanyiko la tisa. Hivyo, mizunguko yote katika Jamhuri ya Muungano ya Ujeremani inakusanyika katika Majumba ya Kusanyiko mazuri, ambayo pia yanatumiwa kwa ajili ya mikusanyiko ya wilaya ya lugha za kigeni.
Uingereza sasa ina Majumba ya Kusanyiko matano yakitumikia asilimia 75 ya wahubiri wa Ufalme wa bara hilo.
Mwaka wa utumishi uliopita uliletea watu wa Yehova vilele vipya vya wahubiri katika Norowei. Ongezeko hili, hata hivyo, limetokeza uhitaji mkubwa wa Majumba ya Ufalme. “Kufikia sasa tumemaliza Majumba ya Ufalme 25 yenye kujengwa haraka-haraka, jambo ambalo limenasa upendezi wa waandikaji habari na umma,” yaripoti afisi ya tawi. Mathalani, katika mji mmoja wa Norowei, akina ndugu waliendea wenye mamlaka wa ujenzi wa mji kupata ufafanuzi wa mambo fulani kuhusiana na ujenzi. Kabla ya kuondoka, walisema juu ya mipango yao ya kujenga jumba kwa muda wa siku tatu. Akina ndugu walipokuwa wakishuka kwenye ngazi, mngurumo wa kicheko ulitoka kwa wote waliokuwa ndani ya afisi. Wale wakuu hawangeweza kuitikadi hata kidogo kwamba ingewezekana kujenga jengo kubwa kama hilo katika muda wa siku tatu tu!
Kazi juu ya lile jumba ilisonga mbele hata upesi zaidi ya ilivyopangwa. Kufikia adhuhuri ya Ijumaa, paa ilikuwa imewekwa nao waashi walikuwa wamefikia nusu ya kazi yao. Ndipo mmoja wa wale wakuu ambaye alikuwa amecheka akaja kwa gari lake na kuona lililokuwa likitukia. Kwa kusisimuka yeye alienda mbiombio afisini na kusema “Jamani, wanafaulu!”
Wakuu wote walipatwa na haya na wakakubali kwamba inawapasa waombe radhi katika njia fulani. Mshiriki fulani wa wafanya kazi alikuwa kiongozi wa bendi yenye wafanya kazi katika maafisi ya manisipaa. Yeye alidokeza kwamba Jumamosi wapige miguu kuelekea mahali pa ujenzi na kuwapigia muziki Mashahidi wa Yehova, “wakiomba radhi” katika njia hii. Wote wakakubali. Kwa hiyo wale ndugu 180 walishtuka kuona bendi ikipiga miguu barabarani kupanda na kuja kwenye mahali pa ujenzi, ikipiga melodia kadhaa kwa ajili ya furahio lao.
‘KUTHIBITISHA KISHERIA HABARI NJEMA’
Mwaka wa utumishi uliopita ulijawa na tendo. Ndugu zetu wameelekeana na uhitaji wa kuthibitisha kisheria kazi ya kuhubiri habari njema.—Flp. 1:7, NW.
Kuhusu visiwa vya Pasifiki Kusini vya Vanuatu, afisi ya tawi ya New Caledonia inaandika juu ya ushindi wa kisheria mkubwa juu ya suala la ujenzi wa Jumba la Ufalme. Baraza la Makanisa ya Kiprotestanti lilipinga vikali mradi huu. Ujapokuwa uhakika wa kwamba akina ndugu walikuwa wamepata haki ya kukodi ardhi na walikuwa wamefanya mipango mahususi ya kupata ruhusa ya ujenzi, walipokea barua kutoka serikali ikitaarifu kwamba, kwa sababu ya upinzani wa makanisa, haingewezekana kujenga vifaa kama hivyo. Waziri mkuu aliandikiwa barua juu ya tatizo hili. Miezi mingi ilipita kabla ya kundi la huko kupokea jibu kutoka kwa waziri mkuu ambayo iliruhusu ujenzi uendelee mbele.
Itikadi za kidini za mtu zinazidi kutumiwa kuwa kabari ili kuvuta maamuzi ya mahakama katika kesi za utunzi wa watoto. Katika Alaska, mathalani, mume asiyeitikadi aliomba utunzi wa mtoto kwa sababu yeye hakutaka mwanaye apewe malezi ya kuwa mmoja wa Mashahidi wa Yehova. Dada yetu anaeleza hivi:
“Wakati mimi nilipochagua kutumikia Yehova kwa nafsi nzima yote, mume wangu aliomba talaka. Yeye alipinga itikadi yetu juu ya matumizi yanayofaa ya damu. [Matendo 15:28, 29] Wala wakili wangu hakuafikika sana na msimamo wetu juu ya damu, lakini kwa kutumia kitabu Reasoning From the Scriptures, mwanamke huyo akawa mwenye kusikitika sana juu ya suala hilo. Alitaarifu kwamba sasa hata yeye angefikiri mara tatu au zaidi kabla ya kuwapa watoto wake mwenyewe damu. Aliuliza kama kile kitabu Reasoning kingeweza kutumiwa mahakamani. Kwa hiyo nilipokuwa kwenye sanduku la ushahidi, mimi nilitumia habari kutoka kitabu Reasoning karibu neno kwa neno. Tokeo? Mimi nilipewa haki ya utunzi wa mtoto wangu. Siku iliyofuata, yule hakimu akatoa amri ya mahakamani ikitaarifu kwamba wakati mwana wangu angekuwa akitembelea baba yake, ikiwa kungetokea aksidenti ingebidi baba yake awaambie wafanya kazi wa kitiba kwamba mwana wangu ni wa imani ya Mashahidi wa Yehova na kwamba ingebidi wao watafute njia tofauti za kuongezea damu.”
Katika United States, Idara ya Kisheria ya Sosaiti huwezesha pakiti ya habari yenye maamuzi mema ya kisheria na madokezo juu ya mbinu za kujaribiwa ipatikane kwa wahubiri wa Ufalme wanaokabili kesi ya utunzi wa watoto. Pakiti hiyo imekuwa kifaa cha kusaidia baadhi ya wahubiri waliokabili tendo la talaka kutoka kwa wenzi wa ndoa wenye kupinga wabaki na utunzi wa watoto wao. Anaandika mhubiri mmoja: “Mimi nilihisi kwamba ile pakiti ya kesi za kisheria ilikuwa kitia-moyo kwangu kwa kuwa ilionyesha waziwazi sana jinsi Yehova anaandalia na kuangalia watumishi wake duniani. Pia, mimi nilithamini yale madokezo ya kushughulikia jaribio, jambo lililothibitika kuwa lenye kunufaisha.”
Tawi la Kanada laripoti: “Sisi tulishinda kesi kumi za utunzi wa watoto ama kwa uamuzi wa mahakama au zikikatwa kwa njia ya masikilizano.” Kesi hizo ziliongozwa ili kukinga haki za wazazi wenye kuitikadi wawape mafundisho ya kidini wazao wao na kuwapeleka kwenye mikutano ya kundi—haki ambazo baadhi ya wazazi wasioitikadi na mahakimu wa mahakama za chini walijaribu kunyima. Ndugu zetu wametetea pia kesi 11 ambamo madaktari wanajaribu kulazimisha juu ya wagonjwa utiaji damu mishipani. Kesi moja ilihusu mtu mzima na zile nyingine zilihusu watoto ambao wazazi wao walikuwa wametaka matibabu tofauti.
Katika Denmark, madaktari wawili wasio Mashahidi wakiandika katika Ugeskrift for læger (Gazeti la Kitiba la kila Juma) wameshughulikia swali la Mashahidi wa Yehova na utiaji damu mishipani. Wale madaktari waliomba miongozo iliyo wazi kutoka kwa mamlaka zenye madaraka. Ingawa mamlaka za afya hazikutaka kufanya jambo hili, zimeonyesha kwamba hakutakuwa na shtaka la kutoka kwenye mamlaka dhidi ya madaktari wanaotaka kuheshimu katao la Mashahidi la damu, hata ikiwa mgonjwa angekufa.
Makabiliano makali na madaktari na mahospitali fulani juu ya utiaji damu mshipani yangali yanatokea katika Korea. Lakini kumekuwako na mafanikio machache. Katika toleo layo la Oktoba 20, 1986, nyusipepa ya kitiba Hu Saing Bo iliripoti kile kisa chenye kufanikiwa cha upasuaji wa moyo bila damu juu ya mwana mwenye umri wa miaka minane wa mmoja wa Mashahidi wa Yehova. Dakt. Park Young-kwan alisema: “Damu nyingi kupita kiasi imetumiwa katika upasuaji wa moyo katika Korea mpaka leo. Lazima sisi tusitawishe mbinu katika nchi hii ya kufanya upasuaji wa moyo kwa kutumia kiasi kidogo zaidi cha damu iwezekanavyo au bila damu kabisa.” Makala hiyo ya habari ilitaja kwamba Hospitali Buchun Sejong inapanga kuandaa upasuaji wa moyo bila tumizi la damu kwa mgonjwa ye yote. Inatia moyo kujua kwamba mipasuo ya moyo imefanywa kwa kufanikiwa juu ya watoto wa Mashahidi wa Yehova.
Huenda mapigano ya kisheria yakashindwa au kushinda katika mahakama. Hata hivyo, jambo la maana ni nani anayeshinda lile pigano la mwisho. Tokeo hilo ni hakika. Kunaweza kuwa na mshindi mmoja tu—Yehova Mungu ambaye jina na neno lake litatetewa.
Afrika Yapaaza Sauti
Mtunga zaburi alisema: “Vinywani mwa watoto wachanga na wanyonyao umeiweka misingi ya nguvu.” (Zab. 8:2) Moses mchanga mwenye umri wa miaka minane, wa Sierra Leone, ni kielelezo chema cha jambo hili. Yeye huona shangwe katika huduma ya shambani na mara nyingi hufanya mipango yake mwenyewe afanye kazi pamoja na wengine katika kundi. Lakini jambo fulani lilimsumbua. Sikuzote yeye alikuwa hana budi kuazima magazeti na broshua za kutumia katika utumishi. Ni jinsi gani, ingawa hivyo, yeye angeweza kupata vitabu vyake mwenyewe, kwa kuwa wazazi wake hawakumpa yeye fedha zo zote za kutumia? Bila ya yeye kuzungumza tatizo lake na ye yote, yeye aliamua njia ya kufuata—yeye angeokoa baadhi ya pesa zake anazotumia kununua chakula cha mchana shuleni! Baada ya siku tatu, yeye alikuwa ameokoa akiba ya kutosha broshua tatu. Yeye atafanya nini na zile pesa anapoangusha zile broshua? “Mimi nitazipeleka kwenye Jumba la Ufalme na kujipatia [broshua] zaidi!” ajibu Moses.
“Mwake roho” hueleza vizuri watu wa Yehova katika Liberia. (Rum. 12:11, NW) Wao waliona kilele kipya cha wahubiri katika Juni, 1,463 wakiripoti—ongezeko la asilimia 11 juu ya wastani wa mwaka jana. Hadhirina ya Ukumbusho ya 8,254 ni kipimio chenye kusisimua cha kadiri ya kupendezwa katika ujumbe wa Ufalme kulivyo katika bara lile.
Kichocheo kwenye matendo makubwa zaidi ya utumishi kilikuwa kuwekwa wakfu kwa afisi yao jipya ya tawi Machi uliopita. Uwanja wa michezo mpya uliojengwa na Wachina ulichaguliwa kwa ajili ya programu ya kuwekwa wakfu huko. Huo ndio uliokuwa wakati wa kwanza ambao uwanja huo ulitumiwa kwa tukio la kidini. Wale wasimamizi Wachina wasioitikadi kuwako kwa Mungu wangeitikiaje? Walipoona ile njia ambayo katika hiyo wale wahudhuriaji 2,126 walijiendesha wenyewe, mjumbe mmoja wa wasimamizi alisema: “Sisi tunaweza kuona kwamba ninyi watu mmepata kufanya jambo la namna hii hapo mbeleni. Mnakaribishwa kurudi wakati wo wote.”
Siku mbili kabla ya Ukumbusho, kundi moja katika Liberia lilielekewa na tatizo halisi. Mahali pao pa kawaida pa mikutano palikuwa pamekodishwa kwa ajili ya tukio la kilimwengu, na pale mahali pengine pekee palikuwa jumba tupu lisilo na viti. Zaidi ya 400 walitazamiwa kuhudhuria, na kwa hiyo akina ndugu waliuendea mfumo wa shule wa huko ambako walikuwa wameazima viti mbeleni. Ombi lao lilikataliwa katakata. Viti vingi sana vilikuwa vimeibiwa na vikundi vingine, wakaambiwa. Mara moja kikundi cha kidini kilikuwa kimeacha viti nje kwa mwisho-juma mzima.
Kusihi kwa akina ndugu kulishindwa. Mamlaka walikataa kubadili msimamo wao. Mwishowe, baada ya utumishi wa shambani, kikundi kimoja cha akina ndugu kilimtembelea msimamizi wa ule mfumo wa shule kufanya sihi moja la mwisho. Ndugu mmoja alieleza yule mwanamke msimamizi wa shule kwamba Mashahidi wa Yehova ni watu waliopangwa vizuri kitengenezo na wanafuata haki, na kwamba kwenye makusanyiko yetu si jambo lisilo la kawaida kwa mtu ambaye amepoteza senti kumi kuzipata tena kwenye Idara ya Vilivyopotea na Kupatikana. Hakika hakungekuwa na tatizo ikiwa vile viti vingetumiwa na Mashahidi wa Yehova pindi hii, yeye akasababu.
Ijapokuwa ombi hili, yule msimamizi alibaki na msimamo ule ule. Dakika hii ile hali ya kimya ilikomeshwa wakati mpwa wa kiume mwenye umri wa miaka sita na nusu wa mmoja wa wale akina ndugu alikimbia na kuingia ndani kutoka upande wa mbele wa uwanja wa nyumba ya yule msimamizi, akisema kwa msisimuko kwamba yeye alikuwa amepata fedha katika huo uwanja wa nyumba. Alimpa mjomba wake dola 5, ambaye alimrudishia yule msimamizi aliyeduwazwa. “Kama wo wote wa watoto wangu mwenyewe wangekuwa wamepata pesa hizi,” mwanamke huyo akakiri, “wao wangaliziweka mfukoni, wakiziona kuwa ‘bahati njema’ yao kutoka kwa Mungu.”
Wale akina ndugu walipata ruhusa ya kutumia viti vyote vilivyopatikana. Mwanamke huyu angesimulia tendo hilo la ufuataji haki kwa kikundi cha sala cha dini yake, na kama dini nyingineyo yote ingemuuliza ni kwa sababu gani aliruhusu ndugu zetu watumie vile viti, yeye angejibu kwamba Mashahidi wa Yehova ni wafuataji haki, naye angejua kwamba wangevitunza vizuri. Wale 474 waliokuwa katika hadhirina waliufurahia Ukumbusho, na vile viti vyote vikarudishwa usiku ule ule.
Katika Afrika Kusini aliyekuwa hapo kwanza akinyanyasa Mashahidi wa Yehova ameukubali ukweli. Siku moja wakati mwanamume huyu na rafiki zake walipokuwa wakizungumza juu ya siasa, ndugu mmoja aliyakatiza mazungumzo yao kwa upole na akawajulisha maoni ya Biblia juu ya habari hii. Wale wanaume, wakiwa na hamu nyingi ya kupata habari zaidi, walimshambulia kwa maswali. Mmoja wa wanaume hao alionyesha kupendezwa sana na majibu ya Biblia. Wakati yule ndugu alipomtembelea nyumbani kwake, yeye alisema: “Mimi nataka kweli kweli kusoma Biblia, lakini ni nani anayeweza kunisaidia?” Yule ndugu alipangia funzo la Biblia akitumia chapa ya lugha ya Kizulu ya kile kitabu Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani. Upesi yule mwanamume akakiri kwa haya kwa yule ndugu kwamba miaka iliyopita yeye alikuwa ameishi katika nchi moja ambako Mashahidi wa Yehova walikuwa wamepigwa marufuku. Alipokuwa akitumikia akiwa askari katika jeshi la nchi hiyo, yeye alinyanyasa Mashahidi. Sasa ukweli umebadili maisha yake. Yeye amekuwa mtangazaji Ufalme mwenye bidii, ambaye anafurahia kubeba mkoba wa vitabu vya Biblia badala ya kubeba bunduki.
Esia ‘Yasifu Yah’
“Sifuni Yah, ninyi watu!” ndicho kilio chenye kishindo kinachomalizia kile kitabu cha Zaburi. (Zab. 150:6, NW) Soma mambo yaliyoonwa yafuatayo uone jinsi nchi za Esia pia zilivyomaliza mwaka wa utumishi wazo kwa kelele ya shangwe kama hiyo.
Tawi la Hong Kong liliona elekeo lenye kupendeza wakati wa mwaka wa utumishi uliopita. Wahubiri wako chonjo zaidi kuona nafasi za kusema kweli, na kama tokeo, si kwamba tu watu wanasikiliza bali wanakuwa wepesi kuonyesha uthamini. Wenye kupendezwa wanahudhuria mikutano kwa ukawaida upesi baada ya kuanza kujifunza Biblia. Mathalani, baba ya kijana mmoja mwanamume alikufa. Kuhusiana na mambo fulani yanayohusu kifo hicho, yule mwanamume kijana, pamoja na mama yake, walienda kwenye afisi iliyomwajiri baba. Akiona kihoro cha yule mwanamume kijana, ndugu mmoja aliyekuwa akifanya kazi katika afisi alisema naye juu ya tumaini la ufufuo na akampa nakala moja ya kitabu Je! Uzima Ndio Uu Huu Tu? Si muda mrefu baada ya hilo, mhubiri mwingine alifika mlangoni pa yule mwanamume kijana na akamwangushia kitabu Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani. Yule mwanamume kijana alisoma kwa hamu nyingi kitabu hicho kizima na akaamua kuhudhuria mkutano kwenye Jumba la Ufalme. Yeye alivutiwa na ukaribishaji mchangamfu aliopokea na akakubali kuwa na funzo la Biblia la nyumbani. Baada ya kujifunza kwa mwezi mmoja, yeye anahudhuria mikutano kwa ukawaida. Zaidi ya hilo, yeye sasa amesoma kitabu Life—How Did It Get Here? By Evolution or by Creation? na sasa anasoma kitabu Usalama Ulimwenguni Pote Chini ya “Mwana-Mfalme wa Amani.”
Dada mmoja painia mzee-mzee kutoka Japani hukiona chumba cha kungojea cha hospitali kuwa eneo lake. Yeye anatumia mbinu gani ya kitheokrasi? Yeye anaketi chini na kusoma vichapo vya Sosaiti, akingojea mtu fulani mwenye utafiti atue na kuuliza vitabu vyake vinasema juu ya nini. Siku moja sauti ilisema nyuma yake, “Nifanye nini nipate nakala moja?” Yeye aligeuka na kuona mwanamume mmoja kijana wa umri wa koleji. Yeye alikuwa amekuwa akitazama nyuma ya bega la yule dada, akijaribu kusoma kile kijitabu In Search of a Father. “Waona, mimi pia namtafuta baba yangu,” akaeleza. Yule dada alimpa kile kijitabu na kuahidi kukutana naye tena kwenye hospitali. Siku chache baadaye yule dada alikutana naye tena. Wakati huu alimtia moyo asome juu ya Baba mwingine, Yehova Mungu. Alipokutana na yule mwanamume kijana baada ya miezi kadhaa, yule dada alishtuka na kufurahi mno kujua kwamba yule kijana mwanamume alikuwa amepata baba wawili—mmoja, baba yake wa asili na yule mwingine, Yehova Mungu mweza yote. Yule mwanamume kijana, mama yake, pamoja na baba yake, sasa walipata onyo la upole lenye mafaa katika kile kijitabu. Kama tokeo, jamaa yote ikaanza kujifunza Biblia pamoja na Mashahidi.
“Huu umekuwa mwaka wenye kutokeza sana kwetu,” latangaza tawi la Taiwan. Ongezeko lao katika wahubiri ni asilimia 13—asilimia iliyo juu zaidi ya ongezeko kwa lile tawi tangu 1959—Majumba ya Ufalme yaliyojengwa mahali kadhaa mwaka mmoja uliopita sasa yamejaa pomoni.
Ili kuendelea kiroho, wapya ambao wameanza karibuni kuwa washiriki lazima wawe na moyo wa kupenda kufanya marekebisho katika maisha zao. Kutoa kielezi: Wanawake kadhaa waliofanya kazi katika kiwanda kile kile walianza kujifunza na wamisionari. Matokeo ya ukweli upesi yakaanza kuonekana waziwazi. Walikataa kufanya ovataimu jioni za mikutano, jambo lisilopata kusikiwa katika vingi vya viwanda, ambako wafanya kazi hufanya saa ndefu. Hata hivyo, kufuata kwao haki na mazoea ya kazi yaliyo kielelezo kizuri upesi yakawachumia madaraka zaidi. Wao walipewa migawo ya kazi yenye kuitibarika ya kutunza maandishi ya mazao.
Tatizo moja lilizuka katika kile kiwanda wakati wale wanafunzi wa Biblia wote walipopeleka maombi ya siku za likizo zile zile ili kuhudhuria mkusanyiko wa wilaya. Uvumbuzi? Wale wanawake walikubali kurudi kwenye kiwanda kila siku baada ya mkusanyiko na kufanya kazi kwa saa moja usiku. Ile kampuni iliwatolea wale wanawake mshahara wa siku kamili kwa utumishi huo, lakini wale wanawake walikataa kwa sababu wao walikuwa wameomba wakati wa likizo kuhudhuria mkusanyiko na hawakutaka kuchukua mshahara wa siku nzima kwa kazi ya saa moja.
Baada ya ubatizo wao, walitamani kupainia na kwa hiyo wakaacha kazi hiyo ya wakati wote katika jitihada ya kupata kazi ya ratiba yenye kuwafaa zaidi. Mwajiri-kazi wao wa hapo kwanza, ingawaje, aliwaendea wale akina dada na kuwatolea kila mmoja wao kazi ya siku tatu kwa juma na akakubali masharti yao ya “hakuna ovataimu jioni za mkutano na kutokuwa kazini siku za makusanyiko.” Ile kampuni iliwaza kwamba ingeokoa fedha kwa kuwaajiri kazi tena wale akina dada. Jinsi gani hivyo? Kwa sababu wao wangeweza kufanya kazi vizuri bila msimamizi. Pia, wao hawangeiba. Yule tajiri alikata maneno kwamba ikiwa Mashahidi wangekuwa waaminifu hivyo kwa Mungu wao, basi hakika wangekuwa wenye kuitibarika katika ile kampuni.
Tawi la Ufilipino laripoti: “Kutoka kisiwa cha Mindanao huja jambo hili lililoonwa la kushika ukamilifu mahali pa kazi pa mtu.” “Dada mchanga katika Jiji la Davao alikuwa akifanya kazi katika afisi ya meya akiwa sekretari. Yeye alikuwa mwenye kudhamiria katika kazi yake, akiripoti mapema na bila kutanga-tanga kazini pake. Hata hivyo, cheo chake hakikuwa cha kudumu, kwa hiyo baada ya kipindi cha wakati kilifikiriwa tena. Yule mkuu wa cha idara yake wakati huo hakumpendekeza aendelee kuajiriwa kazi katika cheo hicho. Yeye alimtolea cheo cha juu zaidi, mradi yeye angejihusisha katika tendo la ukosefu wa adili pamoja naye. Yeye alikataa hilo katakata hata ingawa ingemaanisha kupoteza kazi yake ya kuajiriwa. Aliweka imani yake kamili katika Yehova, na alithawabishwa. Kazi yake nzuri ya kilimwengu ilifikiriwa na wakuu wengine. Wao walimhamisha kumpeleka kwenye afisi nyingine ya serikali akiwa na cheo na mshahara wa juu zaidi.”
Malesia inaonyesha vilele vipya katika sehemu zilizo nyingi za utumishi. Ingawa hali ya kisiasa na kiuchumi si imara, walio kama kondoo na wenye moyo mweupe wanasikia sauti ya yule Mchungaji Mwema. Mathalani, funzo la Biblia lilianzishwa pamoja na mwanamke mmoja wa asili ya Esia-Ulaya na wanaye. Wao waliishi katika hali ya ufukara kwa sababu mumeye hakuweza kuruzuku jamaa. Pia, tangu utoto, mwanaye aliye mkubwa zaidi alikuwa amepagawa na mashetani. Ili kupata msaada, mara nyingi mama aliwaendea Watao Wachina walio vyombo vya kuwasiliana na ulimwengu wa roho na waganga (bomohs) Wamalei. Kwa kweli, ili wajihami wenyewe dhidi ya mashambulio ya mashetani, wote katika jamaa hiyo, kutia na baba, walivalia hirizi (tangkal). Wakati ile jamaa iling’amua kwamba Yehova anachukia hata cho chote kilicho mithili ya kuwasiliana na ulimwengu wa roho, wote waliondoa mara moja hirizi zao ‘zenye kuwahami’ isipokuwa yule baba. Hilo lilikuwa kosa. Baba alishambuliwa tena na mashetani. Ingawa hivyo, wakati huu, mama alitaja jina la Yehova kwa sauti kuu na kusali kwa sauti kuu kwa muda wa nusu saa. Mwishowe, lile shambulio likakoma. Baada ya hilo, baba pia akaondoa tangkal yake. Juma moja baadaye yeye alipata kazi, na mambo yakaanza kubadilika kifedha kwa ile jamaa. Yule mwanamume na mwanamke pia wakang’amua kwamba ilikuwa sharti waandikishe kisheria ndoa yao, na sasa ile jamaa kwa ujumla inafanya maendeleo mazuri katika ukweli.
Milipuko mikali ya vita inayoharibu hali ya amani ya Sri Lanka haikupooza ile roho ya Mashahidi wa Yehova katika nchi hiyo. Wao wamefurahia ongezeko la asilimia 13 katika wastani wa hesabu ya watangazaji wa Ufalme. Ni kweli, lile pambano lilileta hasara ya mali za baadhi ya Mashahidi, lakini kufikia sasa, hakuna ye yote ambaye amepatwa na dhara la kimwili. Kwa kurekebisha nyakati na mahali zifaane na mastakimu na kafyu za kiserikali, mikutano yote ya kundi imefanywa. Hii ilitia ndani makusanyiko ya mzunguko na mikusanyiko ya wilaya pamoja na shule ya painia katika kaskazini yenye kusumbuliwa na vita.
Ingawa hivyo, wahubiri walio katika kanda za vita za kaskazini na mashariki wameponea chupuchupu mara kadha wa kadha. Watu wamechimba mahandaki na kuyafunika kwa mifuko yenye mchanga ili kwamba mabomu yanapoanguka na bunduki mimina-risasi zinapomimina risasi kutoka mahelikopta, wana mahali pa kujificha. Tofauti za kidini na za kitabaka zinasahauliwa upesi wakati watu wanapojitupa ndani ya mahandaki hayo wapate himaya. Wakati wa pindi moja ya pigo la bomu, Wahindu waliokuwa wamesongamana pamoja katika handaki moja walikuwa wakililia mungu wao Muragah wapate msaada. Mmoja aliyekuwa amejifunza habari za Yehova aliwaambia wamwite kwa sauti kuu Yehova kwa sababu ndiye Mungu pekee ambaye angeweza kuwaokoa. Kwa haraka wote wakafanya hivyo.
Pia katika Sri Lanka, painia mmoja mchanga alitembelea Mmethodisti mzee-mzee aliyepinga ziara yake kwa kusema, “Mchanga kama wewe angewezaje kufundisha mimi Biblia?” Yule painia akajibu: “Kwa kweli, mimi sikuja kufundisha wewe bali kushiriki pamoja nawe jambo fulani ambalo mimi nilijifunza likanifanya nifurahi sana na sharti mimi niwaambie wengine.” Itikio la yule painia liliamsha kupendezwa kwa yule mwanamume mzee-mzee. “Basi niambie, ulijifunza nini?” akauliza. “Mimi nimejifunza jinsi ya kuishi milele,” yule painia akajibu. Yule painia alialikwa aingie ndani na mambo ya Kimaandiko yakazungumzwa kirefu. Sasa yule mwanamume mzee-mzee anajifunza Biblia pamoja na yule painia.
Amerika ya Kilatini ‘Yafanya Kazi ya Mweneza-evanjeli’
“Wenye kutenda” ni maneno ambayo yanawaeleza vizuri ndugu zetu wanaoishi katika nchi za Amerika ya Kati na ya Kusini. Wao wamekuwa na shughuli sana ‘wakiifanya kazi ya mweneza-evanjeli’ mwaka huo wa utumishi uliopita, kama mambo yaliyoonwa yanayofuata yanavyoonyesha waziwazi.—2 Tim. 4:5, NW.
Brazili inajipatia mwaka mwingine wa mpanuko katika hesabu ya watangazaji Ufalme na, kwa umaana zaidi, katika ubora wa huduma yao pia. Hadhirina ya Ukumbusho ilikuwa asilimia 23 juu zaidi ya 1986, ikiwa na watu 657,784 katika hadhirina. Vilele vipya sita vya wahubiri vilifikiwa mwakani, kilele cha mwisho kikiwa 216,216. Pia kulikuwa na kilele cha mafunzo ya Biblia ya nyumbani 261,423 yakiongozwa.
Ubora ulionekana wazi katika hesabu yenye kuongezeka ya watangazaji Ufalme walioingia kwenye utumishi wa wakati wote na katika wahubiri waliosafiri ili kufungua maeneo mapya. Vilele kumi katika mapainia wa kawaida viliorodheshwa katika pindi ya mwaka huo. Wahubiri zaidi ya 750 walitumia miisho-juma na malikizo katika angalau miji 110 ambayo haikuwa imetangulia kufanyiwa kazi, kukawa na matokeo yenye kushangaza. Maelfu ya vichapo viliangushwa, dazani za mafunzo ya Biblia yakaanzishwa, na hesabu fulani ya hotuba za watu wote zikatolewa. Barua ifuatayo ni mfano wa itikio la watu wenye kupendezwa katika maeneo haya:
“Mimi nina furaha sana kwamba ninyi mlituma wanawake wawili vijana kwenye mji wangu, kwa kuwa hilo liliniwezesha kupata kujua tengenezo la Yehova. Wao walikuwa baraka halisi kwangu kutoka kwa Yehova. Mimi nasikitika kujifunza kwamba upesi watatuacha. Tafadhali, akina ndugu wapendwa, ikiwezekana, waacheni wakae pamoja nasi kwa muda mrefu zaidi kidogo.—R.M.P.”
Jambo moja kuu la mwaka huu wa utumishi kwa Brazili lilikuwa kutolewa kwa New World Translation Reference Bible Biblia moja yenye chapa kubwa katika Kireno. Nyusipepa kadhaa na magazeti yalikuwa na makala juu yayo. Veja, gazeti la habari linalojulikana sana katika São Paulo, lilichapisha makala moja yenye kichwa: “BIBLIA YA YEHOVA—Tafsiri iliyo kamili zaidi sana ya Maandiko yatolewa,” ikisema kwa sehemu:
“Juma lililopita, Mashahidi wa Yehova walitoa katika Brazili Biblia yenye maelezo ya pambizoni na maandiko-mlingano mengi zaidi ya nyingineyo yote iliyopata kutolewa. Kikiitwa The New World Translation of the Holy Scriptures, kitabu hicho kilitungiwa United States kwa msaada wa makompyuta na kikachapwa katika buku moja la kurasa 1,600. Katika Brazili, [hiyo Biblia mpya] ina chapa ya kwanza ya nakala 50,000, jambo ambalo ni zuri sana. Chapa iliyo nzuri ya kitaifa ina wastani wa nakala 5,000.”
Yale magazeti yanayochapishwa katika rangi nne yanazaa matokeo mazuri sana katika Brazili. Afisi ya tawi haijapata kamwe mbele ya hapo kupokea maandikisho mengi sana hivyo: 49,154 katika mwezi mmoja. Vicente, mhandisi wa reli, husafiri wakati mwingi sana na hivyo huduma yake ya mlango kwa mlango ni ya kiasi tu. Yeye alisoma katika Mnara wa Mlinzi kwamba dada mmoja alikuwa ameangusha maandikisho 59 kwa kuwatolea wafanya kazi wenzake. Kwa hiyo yeye akaamua kujaribu hilo. Yeye aliweka mradi wake kuwa maandikisho kumi kwa Aprili. “Mimi nilishtuka kikweli,” akaandika. “Mimi nilifikia mradi wangu katika siku mbili! Kwa hiyo mimi nikauinua kufika 20 lakini nikaufikia katika siku saba. Mradi wa tatu wa 30 ulifikiwa kufikia katikati ya mwezi. Kwa hiyo nikaweka mradi wangu kuangusha mengi kama alivyofanya yule dada ambaye ono lake nilikuwa nimesoma. Wazia shangwe yangu wakati nilipoweza kuripoti maandikisho 68 kwa mwezi ule!”
Ndugu mwingine, aliposikia wazee wakitia moyo utumishi wa painia msaidizi, aliuomba katika Machi. Yeye aliufurahia sana hivi kwamba aliendelea katika Aprili na akaangusha maandikisho 79 katika miezi hiyo miwili, mengi yayo kwenye mahali pake pa kazi.
Hata mtoto mwenye umri wa miaka minne alifanya sehemu yake. Rafiki mmoja alikuja kutembelea jamaa yao kwa siku chache. Siku moja yule mgeni alihisi kutaka kusoma naye akalalamika hivi, “Je! hakuna cho chote cha kusoma katika nyumba hii?” Yule Shahidi mchanga, mikono yake ikiwa viunoni mwake, akajibu kwa ukali hivi, “Kumbe hakuna cho chote cha kusoma katika nyumba hii? Ngoja dakika moja tu.” Msichana huyo akakimbia kwenye chumba cha mamake, akapanda juu ya kiti, akapata rundo la magazeti ya mamake, Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Akampelekea yule mgeni akasema “Sasa ona kama hakuna cho chote cha kusoma!” Yule mgeni aliyafurahia sana hivi kwamba mchanga yule akasema: “Ukitaka, unaweza kuyapokea nyumbani mwako kwa posta.” Tokeo likawa nini: maandikisho mawili.
Ekwedori ilikuwa na wawakilishi kutoka mataifa kumi na matatu tofauti wakifanya kazi kwenye mradi wao wa tawi mwaka huo wa utumishi uliopita. Jambo kuu kwa hao wafanya kazi wa ujenzi wa kujitolea lilikuwa wakati waliotumia katika utumishi wa shambani, kijapokuwa kizuizi cha lugha. Masoko ya jua-kali, vituo vya basi, na barabara za mji yalikuwa mahali palipowafaa kufanya kazi ya kutoa ushuhuda. Mara nyingi kuonyesha tu mojapo vitabu vyenye picha, kama vile Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia, au broshua yenye rangi kunatosha kuvuta idadi kubwa ya watu. Kikundi cha ndugu wanane kutoka kwa wafanya kazi wa ujenzi walihubiri katika soko asubuhi moja na kuangusha vitabu 73, broshua 51, na magazeti 30. Katika wakati mwingine, kikundi cha wanne kilitoa ushuhuda kwenye kituo cha mwisho cha basi na kuangusha broshua 133 na vitabu 13. Wangaliweza kuangusha vitabu zaidi, lakini akiba yao iliisha.
Tetemeko la dunia moja lilitikisa San Salvador mji mkuu wa El Salvador, mara tu mwaka wa utumishi ulipoanza. Angalau akina ndugu 14, pamoja na watu wenye kupendezwa, waliuawa. Majumba ya Ufalme mengi na makao ya watu binafsi yalibomoka. Tokeo lililo kubwa zaidi la tetemeko juu ya watu lilikuwa, si maumivu kutokana na hasara ya mali ya kimwili, bali ule mshtuko wa kimoyoni lililousababisha. Juu ya hilo, ile jeuri ya kisiasa yenye kuendelea ambayo huenea nchini inalemea watu. Pia, maji na nguvu za umeme hutolewa kwa kipimo kwa vipindi virefu vya wakati, huku infleshoni ikipunguza sana thamani ya pesa za watu.
Hata hivyo, katika mazingira haya yasiyo na tumaini, akina ndugu wana matazamio mazuri ya kiroho kwa sababu tawi limewaendeleza wakiwa na shughuli katika kazi za kitheokrasi. Msaada ulitayarishwa kwa ajili ya washiriki wa kundi waliopoteza makao yao katika lile tetemeko la dunia. Majumba ya Ufalme yalitengenezwa. Kisha Desemba ukatokeza kiinua hali cha kiroho kikubwa—“Amani ya Kimungu” Mikusanyiko ya Wilaya minne. Jumla ya hadhirina ilikuwa 30,003, na 521 wakabatizwa. Ukumbusho ulihudhuriwa na 58,933—hesabu iliyo kubwa zaidi karibu mara nne ya kilele chao cha wahubiri 16,041.
Amerika Kaskazini na Visiwa vya Karibea ‘Zatoa Ushuhuda’
Watu wawe matajiri au maskini, wadogo au wakubwa haifanyizi tofauti kwa watumishi wa kidunia wa Yehova; wao wataendelea ‘kutoa ushuhuda’ kwa watu wote. (Mdo. 26:22) Huenda wenye nyumba fulani wakataka kujua ni kwa sababu gani sisi huendelea kuwatembelea baada ya wao kutuambia hawapendezwi. Lakini kuna sababu nzuri sana kwa nini tunarudi. Fikiria kielelezo hiki kutoka Kanada:
Mwanamke mmoja aliyetembelewa na Mashahidi wawili aliwaambia wazi kabisa kwamba yeye hakutaka lo lote kuhusiana na dini yetu. Baadaye, alipokuwa akifanya kazi zake za nyumbani, yeye alianza kufikiria Mashahidi. Maswali juu ya itikadi zetu yakaja akilini mwake. Kwa hiyo aliingia katika gari lake na kuliendesha juu-chini katika barabara za mji ili akatafute wale Mashahidi wawili. Hawakupatikana po pote. Kisha aliendesha gari lake kwenda nyumbani kwa rafiki yake, akifikiri kwamba wao walikuwa wametembelea rafiki yake. Hapana, wao hawakuwa wametua huko, akaambiwa. Yule rafiki yake alisema kwamba alifanya kazi pamoja na Shahidi mmoja na akajitolea kuwakutanisha hawa wanawake wawili. Yule dada aliyeendewa anaeleza hivi:
“Katika ile ziara ya kwanza kabisa, kwa mshangao wangu, walikuwapo wanawake watano, walionishambulia kwa maswali kama vile, ‘Ni kwa sababu gani ninyi mnajiita wenyewe Mashahidi wa Yehova?’ ‘Ni kwa sababu gani ninyi mnaende nyumba kwa nyumba?’ na ‘Je! ninyi mnaitikadi katika Yesu?’ Mimi nilitumia saa tatu nikijibu maswali yao. Tangu ziara hiyo ya kwanza kabisa, mimi nimerudi kwa wastani mara tatu kwa mwezi na nimekutana na watu 5 hadi 15 kila wakati.”
Katika kipindi cha wakati wa miezi sita, dada yetu aliangusha magazeti 313, vijitabu 171, na vitabu 272 kwa kikundi hicho. Lakini sasa yule dada anasema: “Mimi natia kila jitihada kutia moyo kile kikundi kijifaidi na programu yetu ya funzo la Biblia la nyumbani wakiwa mmoja mmoja.” Itapendeza sana kuona yale yatakayotukia bado.
Shule ni ardhi yenye rutuba ya kupanda mbegu za Ufalme. Shahidi mmoja mchanga kutoka Kanada anasema hivi juu ya kile kitabu Life—How Did It Get Here? By Evolution or by Creation?: “Mimi niliamua kukiweka juu ya dawati yangu katika njia ya kwamba kingeonekana wazi na wanafunzi wengine. Watano walikuja na kukitazama. Mimi nilitaja sura zacho mbalimbali. Wanafunzi watatu waliniomba niwapatie nakala. Kisha, mimi nilimuuliza mtunza-maktaba ya shule kama yeye angependa kimoja. Yeye alikubali kukipokea kama mchango kwa maktaba. Kesho yake, aliniambia kwamba tayari kilikuwa kimeazimwa na akaomba apate kimoja kwa ajili yake mwenyewe na kingine kwa ajili ya rafiki mmoja. Mwishowe, mwalimu wangu wa sayansi alikubali nakala mbili. Mtunza-maktaba pia ameomba vingine viwili zaidi tangu hapo. Mimi nimepata kuona kwamba ikiwa wewe unatia jitihada, Yehova ataibariki. Yeye alibariki jitihada yangu kwa angusho la vitabu 11.”
Vijana katika Guadeloupe wanasihiwa pia wafanye shule yao kuwa eneo ambalo katika hilo wangetolea ushuhuda wanashule wenzao na walimu. Hata hivyo, mwenendo mzuri katika shule ni wa maana kabisa pia. Desemba uliopita, katika darasa moja wanafunzi walipewa mgawo wa kukariri somo moja juu ya Krismasi. Dada mmoja mchanga alikataa na akajitolea akariri somo moja juu ya habari nyingine. Yule mwalimu wa shule alishikwa na kiruu na akaongoza darasa katika kudhihaki dada yetu.
Lakini kufikia robo ya tatu ya mwaka wa shule, hali zilikuwa zimebadilika. Yule mwalimu alikiri kwa mama ya yule mhubiri wetu mchanga hivi: “Yehova yupo pamoja nanyi; yeye anamhami binti yako. Si kwamba tu mwenendo wake ni mzuri sana, bali yeye pia anafanya vizuri sana katika kazi ya shule, akipata wastani mzuri. Mimi nataka kukupongeza wewe. Wewe umeelimisha mtoto wako vizuri. Alasiri ii hii tu mimi nililiambia darasa zima kwamba Yehova, Mungu wa binti yako, ndiye Mungu wa kweli na ni mwenye nguvu zaidi ya miungu ya dini nyinginezo kwa sababu mwenendo wa binti yako sikuzote ni wa heshima, hali wanashule wenzake hufanyiza fujo na kufanya mambo mabaya.”
Netherlands Antilles ni eneo la wenye kusema lugha nyingi. Kiholanzi ndiyo lugha rasmi. Papiamento ndiyo lugha ya kienyeji, hali Kiingereza ndiyo lugha ya biashara. Watu wengi husema pia Kihispania kwa sababu Netherlands Antilles ni kikundi cha visiwa vilivyo karibu sana na pwani ya Kolombia na Venezuela. Hivyo, mtu wa kawaida husema na kusoma lugha kadhaa. “Kwa mshangao wetu,” yaandika afisi ya tawi, “kile kisiwa cha Kurasao, kikiwa na idadi ya watu 171,500, kina nyusipepa sita za kila siku, na zote huendelea katika biashara mwaka baada ya mwaka. Kwa kuwa watu hapa hupenda kusoma, wao wanasoma vitabu vyetu pia. Wao wanathamini kikweli magazeti yetu yenye kupendeza. Mojapo tukio kubwa la mwaka limekuwa kutokea kwa chapa ya Kipapiamento ya Mnara wa Mlinzi katika rangi ya kurasa nzima. Bila shaka hili limetusaidia kuongeza maangusho yetu ya magazeti wakati wa mwaka wa utumishi.”
Si ajabu kwamba Martinike ilikuwa na hadhirina ya Ukumbusho ambayo ni karibu mara tatu hesabu ya wahubiri. Watu katika kisiwa hicho hufanya maendeleo ya haraka katika kutumia ukweli. Mathalani, wiki moja baada ya dada mmoja painia na mumeye kuanza funzo la Biblia pamoja na mume na mke waliooana, wapya hao wenye kupendezwa walihudhuria funzo la kitabu na, upesi baada ya hapo, mikutano yote. Mwezi mmoja baadaye walikuwa sehemu ya wasikilizaji kwenye mkusanyiko wa wilaya. Kwa kuwa yule mwanamume alikuwa kiongozi wa chama cha wafanya kazi, mipango ya kitengenezo ya ule mkusanyiko ilimvutia. Lo! ulikuwa tofauti kama nini katika adabu na mikutano ya chama chake! Yule mwanamume alishirikiana pia na kikundi kilichojizoeza yoga. Lakini sasa alisema: ‘Biblia ni dawa nzuri zaidi kwa utulivu wa akili na moyo na ni yenye msaada mwingi zaidi katika kutatua matatizo ya kibinafsi kuliko zoea la yoga.’ Miezi minane baada ya funzo lake la kwanza, yeye alionyesha wakfu wake kwa Yehova kwa ubatizo wa maji, na mke wake na binti mkubwa zaidi sasa ni wahubiri.
Ulaya ‘Yatangaza Uhuru’
Huku tisho la vita ya nyukilia likining’inia kama wingu lenye kutisha juu ya Ulaya, Mashahidi wa Yehova wanatangaza uhuru ambao ni Yehova tu anayeweza kuleta. (Isa. 61:1) Habari njema hizi zinasikiwa hata na wale walio wagumu kufikia, kama jambo lifuatalo lililoonwa linavyoonyesha.
Austria ilifanya jitihada nyingi wakati wa mwaka wa utumishi uliopita kutumikia watu walio viziwi. Mwanamume mmoja kijana aliye kiziwi katika nchi hiyo alipata nakala moja ya Mnara wa Mlinzi katika chumba cha kungojea cha kituo cha reli. Alikuwa mwenye udadisi, akachukua lile gazeti, na kuanza kusoma. Lile neno “Yehova” lilimtatiza. Yeye alifikiri ‘ni jina la mmoja wa mitume wa Yesu,’ na akaendelea kusoma. Makala moja iligusa moyo wake, na kwa kuwa sikuzote ilikuwa tamaa yake kufundisha watu juu ya Mungu, yeye alizuru afisi ya tawi katika Vienna. Huko yeye alipokea anwani ya mahali viziwi huwa na mikutano yao. Yeye alihudhuria mkutano wa kwanza juma ilo hilo hata ingawa ilimaanisha kusafiri kilometa 90 za kwenda na za kurudi pia. Bidii yake tayari imezaa matunda. Mume na mke walio viziwi wanajifunza Biblia na wanahudhuria mikutano kwa ukawaida.
Katika Sweden Kanisa la Serikali la Kilutheri lina kazi ngumu. Zaidi ya asilimia 90 ya idadi ya watu ni wa kanisa lile, lakini ni kikundi cha wachache tu kinachohudhuria kanisa kwa ukawaida. Watu wanajiuzulu uanachama wao wa kanisa kwa maelfu kila mwaka. Viongozi wa kidini katika kusini mwa Sweden wanahangaika. Walipanga semina mbili kuzungumzia hali hiyo. Kwa kuwa Mashahidi wa Yehova wanajulikana kuwa kimojapo vikundi vya kidini vinavyokua kwa haraka zaidi katika Sweden, yule mpangaji wa semina alipiga simu kwenye afisi ya tawi na kuomba kama mmoja wa Mashahidi wa Yehova angeweza kuja na kuwataarifu juu ya itikadi, njia, na tengenezo letu. Mwangalizi wa wilaya mmoja alitumwa. Yeye alitoa hotuba na kujibu maswali yao.
Kwenye ile semina ya kwanza, iliyofanywa Februari 1986, makasisi na wawakilishi wengine wa kanisa wapatao 50 walikuwapo. Walisikiliza kwa makini, wakiwa na mwelekeo wa upole na heshima. Baada ya pindi hiyo, vitabu 5, broshua 25, na magazeti 30 viliangushwa.
Semina iliyofuata ilifanywa Februari 1987. Viongozi wa kidini wapatao 20, profesa wa sosholojia ya kidini, na profesa msaidizi wa theolojia kwenye Chuo Kikuu cha Lund walihudhuria. Akimjulisha mwangalizi wa wilaya kuwa msemaji, mwenyekiti, aliyekuwa vikari alisema: “Kwanza, mimi nataka kuwaambia ninyi kwamba mimi nina hakika hakuna ye yote wetu sisi makasisi [tulio] hapa angekubali kuhubiri katika hali zile zile kama mgeni wetu msemaji anavyofanya. Mimi najua kwamba yeye anafanya hivyo kwa wakati wote na bila mshahara. Tofauti na hilo, sisi makasisi tunalalamika juu ya mishahara yetu, tukitaka zaidi na zaidi nyakati zote.”
Wakati wa pindi hiyo, maswali mengi yalizushwa nao wasikilizaji walielekea kukubali maelezo yaliyotolewa. Baada ya pindi hiyo, walio wengi wao walipanga mstari mbele ya yule ndugu na kuomba vitabu. Broshua zipatazo 25 na magazeti 20 viliangushwa. Kijana mmoja kiongozi wa kidini alimwambia yule ndugu kwamba yeye anasifu sana tengenezo letu. “Inashangaza kuona jinsi ninyi mnavyoshikamana pamoja katika itikadi yenye umoja sana na udugu katika nchi zaidi ya 200 kuzunguka ulimwengu,” yeye akasema akipiga kite juu ya magumu yanayopata kanisa katika Sweden.
Kilometa zipatazo 80 kutoka Madrid, Hispania, yamejengwa magereza mawili yenye ulinzi wa hali ya juu ambamo wahalifu hatari na washambulizi hufungwa. Katika mojapo ya magereza haya, ambalo linatengenezwa upya, chumba kimoja kinatayarishwa kitumiwe kipekee kama “Jumba la Ufalme” na chumba cha funzo kwa wale wanaotaka kuzungumza juu ya Biblia pamoja na Mashahidi wa Yehova. Katika lile gereza jingine, wafungwa wapatao 50 wanakutana pamoja kwa kawaida kusikiliza mikutano iliyorekodiwa inayofanywa na kundi la mahali pale.
Wale wafungwa wanaohudhuria mikutano hii wanaonekana kuwa tofauti na wale wafungwa wengine. Wao wanajipamba na kuvalia kwa unadhifu, na hata wao wanafunga tai, jambo ambalo hakuna mmoja wa wale wafungwa wengine hufanya. Ishara inayosema “Hakuna Kuvuta Sigareti” imewekwa ionekane wazi kwenye mahali pa mkutano.
La maana zaidi, hao wafungwa wanatumia yale wanayojifunza. Mfungwa mmoja alikuwa amepanga kwa uangalifu sana wizi wa benki, ambao angefanya baada ya kuachiliwa kwake. Yeye alitupilia mbali mipango hiyo kwa sababu ya ukweli wa Biblia aliokuwa amejifunza. Mwingine ameamua kumwoa kisheria yule mwanamke aliyekuwa amekuwa akiishi naye kwa muda wa miaka tisa. Hata hivyo, mfungwa mwingine alikuja kwenye mkutano akiwa na jicho jeusi. Alipoulizwa kilichokuwa kimetukia, kwa uchangamfu yeye alieleza kwamba mfungwa mwenzake alikuwa amempiga ngumi, lakini yeye alikuwa na furaha sana kwa sababu alikuwa amefaulu kujizuia asirudishe ovu kwa ovu.
‘Mtukuze Yehova Katika Visiwa vya Bahari’
Kutoka visiwa vya bahari yaja sauti ambayo kweli kweli inalitukuza jina la Yehova. (Isa. 24:15) Kile kisiwa cha Réunion, kilichoko katika Bahari Kuu ya Hindi mashariki mwa Afrika katika eneo la tawi la Mauritius, ni mfano mmoja wa sauti hiyo. Alipokuwa katika shughuli ya kazi ya kuhubiri, ndugu mmoja kijana alimkuta mwanamuziki mmoja ambaye tayari alikuwa na baadhi ya vichapo vyetu vya Biblia. Yule mwanamuziki alikuwa wa bendi ya muziki wa roki ya watu watano, ambao walikuza na kuuza marijuana (bangi). Hata hivyo, yule ndugu alimwalika yule mwanamuziki kwenye mkusanyiko wa wilaya wa 1986. Watatu kutoka bendi ile walikuja ile siku ya kwanza ya mkusanyiko, na wote watano wakahudhuria siku ya mwisho. Funzo la Biblia lilianzishwa kwa wote. Washiriki wanne wa ile bendi walikuwa wa jamaa moja, na ujapokuwa upinzani kutoka kwa jamaa yao, wao waliharibu zao lao la marijuana. Halafu, wao walilitolea kundi kama msaada ile maikrofoni waliyotumia kwa muziki wao wa roki. Katika muda wa miezi mitatu, wote watano walibadili maisha zao kwa kadiri ya kwamba walistahili kuwa wahubiri.
Mashariki ya Australia utapata New Caledonia. Katika pindi ya mwaka wa utumishi uliopita, afisi hii ya tawi ilituma ndugu kadhaa kwenye visiwa Wallis na Futuna, ambako Kanisa Katoliki hutawala maisha za watu nalo linapinga kazi yetu vikali sana. Hesabu fulani ya akina ndugu kutoka visiwa hivi wanaishi katika New Caledonia. Katika pindi moja ya ziara ya hivi karibuni, akina ndugu walikutana na mwalimu wa koleji kutoka Kanisa Katoliki. Yeye aliwaambia kwamba, hivi karibuni, wao walikuwa na mazungumzo fulani darasani juu ya zile dini nyingine, na wanafunzi wote walitaka kuongea juu ya itikadi za Mashahidi wa Yehova. Baada ya kufanya uchunguzi fulani na kusikiliza hotuba zenye msingi wa vichapo vyetu, mwanafunzi mmoja alisema: “Inashangaza kuona kwamba wale wanaotoka kwenye kikundi chetu cha kikabila ambao wamekuwa Mashahidi wanaelekea kuwa na akili iliyo wazi zaidi, yenye kiasi zaidi, na wana maarifa mengi ya Biblia. Inaonekana kana kwamba harakati hii imefaulu katika kugeuza watu. Sisi hatuoni kani yenye kugeuza iyo hiyo katika kanisa letu.”
Kutoka afisi ya tawi ya kisiwa cha Pasifiki cha Hawaii sisi tunasikia ripoti za wachanga ambao wangali shuleni ambao pia huchukua msimamo ulio imara zaidi upande wa Yehova. “Kwa sababu mimi niliogopa kupata itikio lisilofaa kutoka kwa wanadarasa wenzangu, mimi naweza kukumbuka wakati nilizoea kuwapa sababu zilizo rahisi zaidi sana za mimi kujiepusha na mambo ya kilimwengu,” anakubali msichana mmoja Shahidi. “Basi, sifanyi hivyo tena! Mimi nimejifunza kuchukua kila mkazo mmoja mmoja na kuutumia kuwa nafasi ya kutoa ushuhuda zaidi. Hilo limeendeleza uhusiano wangu pamoja na Yehova na kujiheshimu mimi mwenyewe.”
Akiwa na jitihada hizo za unyofu, msichana huyo ameangusha vitabu vingi na kuongoza mafunzo ya Biblia tofauti tofauti yapatayo saba. Mwalimu wake wa sayansi alisema hivi kuhusu yeye: “Mimi nimeongea na wachache wa Mashahidi wa Yehova mbeleni wakati walipokuja kwenye mlango wangu, lakini imenichukua mpaka mwaka huu kupitia kwa mazungumzo tuliyoshiriki, vitabu ambavyo nimesoma, na uwezo wako wa kusema juu ya yale ambayo wewe unaitikadi kuwa yafaa kupanua hatimaye uelewevu wangu juu ya tengenezo la Mashahidi wa Yehova. Mimi nasifu sana jitihada na matimizo yako, na sasa ninaweza pia kuheshimu dini yako. Asante sana kwa kutonyamaza kimya na kwa kuchukua wakati kunieleza imani yako.”
Yule dada kijana anajumlisha mwelekeo wake juu ya kutoa ushuhuda shuleni kwa njia hii: “Jambo moja ambalo nimejifunza: Hata ingawa sisi tumetenganishwa na wale wahubiri na mapainia wengine na mikutano ya utumishi wa shambani, sisi hatujatenganishwa kamwe na eneo letu. Kwa saa 30 kila juma, sisi tuna eneo ambalo hakuna mwingineye yote anaweza kulifanyia kazi.”
Nchi Zilizo Chini ya Marufuku ‘Zaimba Juu ya Nguvu za Mungu’
Uvutano wa Yehova huvunja-vunja zile hila mbovu za wapinzani, hivyo kuwezesha watumishi wake wa kidunia ‘kuimba juu ya nguvu za Mungu.’ (Zab. 59:16) Ndugu zetu wanaoishi katika nchi ambako kazi ya Ufalme imepigwa marufuku hawawezi kunyamazishwa. Ueneza-evanjeli wao waendelea.
Siku moja katika Novemba 1986, katika mji mmoja wa kimkoa wa Afrika, kikundi kidogo cha akina ndugu kilichokuwa kimekusanyika katika nyumba ya faragha kwa Mkutano wa Utumishi kilitiwa mbaroni. Katika kikundi hiki alikuwamo yule painia wa pekee ambaye huchukua uongozi katika lile kundi. Yeye alipigwa vibaya sana na kupigwa mateke na mmoja wa wale mapolisi wawili waliokuwa wamewatia mbaroni. “Yeye ndiye anayeendeleza wengine katika kazi ya kuhubiri yajapokuwa marufuku! Ni kosa lake kwamba wengine wamo gerezani,” yeye akapaaza sauti.
Alipokuwa akipigwa, yule ndugu alililia Yehova kwa msaada na nguvu. Yule mlinzi wa gereza aliyekuwa akitazama alimwambia yule aliyekuwa akimpiga kwamba afadhali aache, akiongeza, “Inakupasa kujihadhari na kuwatenda vibaya watumishi wa Mungu!” Hilo lilikuwa na tokeo kwa sababu kesho yake yule polisi alikuja kwa ndugu akiomba msamaha kwa yale aliyokuwa amefanya. “Nililofanya lilikuwa baya sana,” yeye akasema kwa majuto. Yeye alikiri zaidi kwamba alijua Yehova ndiye Mungu wa kweli. Yule painia wa pekee na wale wengine waliachiliwa juma moja baadaye. Sasa wakati polisi wanaona ndugu zetu wakishiriki katika huduma, wanawaacha.
Katika nchi nyingine ya Kiafrika, kundi moja la wahubiri 35 tu walikuwa na wahubiri wengine wapya 19 wakibatizwa. “Mnara wa Mlinzi uliokoa maisha yangu!” akasema mmoja wao kabla ya ubatizo wake. Hivi ndivyo ilivyotukia:
Yeye alikuwa amekuwa afisa wa kile chama cha kisiasa chenye kutawala. Yule msimamizi wa kikundi cha washambulizi cha kwao na genge lake walimwinda mwanamume huyo. Walipowasili kwenye kao lake, wale washambulizi walimkuta akisoma gazeti la Mnara wa Mlinzi. Wao walimuuliza kama yeye ni mshiriki wa kanisa ambalo hutangaza gazeti hilo. Yeye alijibu kwamba yeye bado si mshiriki lakini alikuwa akijifunza na Mashahidi na alitumaini kuwa mmoja wao. Walimwambia kwamba wao walijua alikuwa afisa wa eneo wa kile chama chenye kutawala, lakini “kwa sababu ya lile gazeti” alilokuwa akisoma, hawatamuua. Wao walimwacha akiwa hai.
Kwa kusisimuka, mtu huyo mwenye kupendezwa alienda mbio kwenye mahali pa mkutano na kueleza akina ndugu kwamba yeye angalikuwa mfu kama si kwa sababu ya gazeti la Mnara wa Mlinzi. Sasa yeye alikuwa amepiga moyo konde awe mmoja wa Mashahidi wa Yehova.
Katika nchi ambako mateso ni mengi, Yehova anaweza kupofusha adui ili kuwapa himaya watumishi wake, kama jambo hili lililoonwa kutoka nchi moja ya Kiafrika linavyoonyesha. Tangazo la ziara ya mwangalizi wa mzunguko iliyokuwa ikija liliwasili kwenye kundi moja wakati ule ule ndugu mmoja alipotengwa na ushirika. Yule aliyetengwa na ushirika akawa mtaka kulipa kisasi naye akawaambia polisi kwamba alijua tarehe ya ziara ya mwangalizi wa mzunguko, naye angeweza kuwaongoza kwenye kao na kutambulisha huyu “samaki mkubwa,” mtu mashuhuri katika tengenezo letu.
Wenye mamlaka walionyesha kupendezwa kwingi nao wakangojea pindi hiyo kwa hamu. Ndipo, bila kutazamiwa, mwangalizi wa mzunguko alisogeza mbele tarehe ya ziara yake kwa kundi hili kwa majuma kadhaa. Wakati yule mwanamume aliyetengwa na ushirika alipoongoza polisi kwenye lile kao ambako yeye alidhani mwangalizi wa mzunguko angekuwa akizuru, kulikuwako kitamaushi kikubwa. Walipojifunza kwamba polisi walitazamia kumtia mbaroni mwangalizi wa mzunguko, akina ndugu waliwaambia polisi kwamba mhaini huyu hakuwa tena mmoja wa Mashahidi wa Yehova. Walipoulizwa ni kwa sababu gani, akina ndugu walijibu kwamba yeye hakuwa akiishi maisha ya Kikristo na kwa sababu hiyo alikuwa ametengwa na ushirika. Kwa kukasirishwa na matumaini ya bandia yaliyokuwa yamezushwa na wakiwa wametahayarishwa, wale polisi walisema: “Basi, ikiwa yeye hafai vya kutosha kwenu, yeye hafai vya kutosha kwetu pia,” nao walimburuta yule mtu aliyetengwa na ushirika na kumtupa gerezani.
Kutoka nchi moja ya Kiesia iliyo chini ya marufuku, mmoja wa mapainia alimkuta mwanamume kijana kwenye mlango ambaye alionyesha kupendezwa kwingi katika mazungumzo ya Biblia. Kwa kuwa yeye hakuwa amebeba vitabu vyo vyote, aliahidi kuzuru tena na kumpa kitu fulani cha kusoma. Wiki iliyofuata alirudi. Baada ya mazungumzo ya saa moja na nusu, yule kijana alichukua kile kitabu Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani. Alisema: “Wajua, mimi nimekuwa nikisali Mungu kwa wiki tatu atume mtu anisaidie kuelewa Biblia. Mimi naitikadi wewe ni jibu la sala yangu.” Yule dada na mumeye sasa wanaongoza funzo la Biblia na mtu huyu mwenye kupendezwa.
Katika nchi moja ya Mashariki ya Kati, ndugu mmoja aliteswa na jamaa yake; wao walimwona kuwa mwasi-imani. Wakati yeye alipomwambia mama yake kwamba ndoa yake ingefunganishwa na mhudumu wa Mashahidi wa Yehova, yeye alikataa kabisa mwaliko wake ahudhurie mwadhimisho wa ile arusi. Yeye aliiona ndoa ya mwanaye kuwa namna fulani ya uzinzi kwa sababu ingefanyiwa mkataba nje ya kanisa lake. Mwishowe, yule ndugu alimsadikisha mamaye ahudhurie arusi yake. Yeye alienda bila kutaka, lakini alipokuwa akisikiliza hotuba iliyotolewa na mzee, yeye akaanza kulia. Mwana mwingine wake, akiwa katika hadhirina pia, alishtuka. Yeye alimuuliza mamaye ni kwa sababu gani alikuwa na huzuni. Mama alisema kwamba yeye alikuwa amehudhuria miadhimisho mingi ya ndoa, lakini hii ndiyo iliyokuwa mara ya kwanza maishani mwake mwote kuelewa ndoa ni nini hasa, sababu yayo na maana yayo. Yeye alilia kwa sababu alikuwa na furaha. Sasa yule mama na wale washiriki wengine wa jamaa kwa ujumla wamo katika ukweli.
Kwa kupendeza, katika chapa ya Machi 15, 1987, ya The Sunday Gleaner kutoka Kingston, Jameika, mhariri mmoja, baada ya kusoma Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova 1987 na kutoa maelezo mazuri juu ya ukuzi wetu wa haraka, alimalizia tahariri yake kwa taarifa hii: “Ikiwa sisitizo lenye kuendelea la kuhubiri zaidi litafuatwa katika mwaka huu wa utumishi, kitabu cha mwaka 1988 chapaswa kiwe chenye kuvutia hata zaidi.” Ndiyo, baada ya kufikiria ripoti ya mwaka wetu wa utumishi uliopita, sisi tunaweza kukata maneno kwamba hicho ni “chenye kuvutia hata zaidi.” Hivyo, shukrani zimwendee Yehova, toka mwisho mmoja wa dunia kufika ule mwingine kazi ya kueneza evanjeli ya Mashahidi wa Yehova yaendelea.—Zab. 75:1.
[Sanduku katika ukurasa wa 27]
Wafanya-kazi wa Kimataifa wa Ujenzi wa Kujitolea
Katika pindi ya mwezi wa Novemba 1985, wenye kujitolea 11—wa umri mbalimbali kuanzia ndugu mseja mwenye umri wa miaka 26 kufika wazazi-mababu-na-nyanya wenye umri wa miaka 59—waliondoka United States kwenda Afrika. Utume wao ulikuwa nini? Kusaidia katika ujenzi wa kifaa kipya cha tawi katika nchi ambayo hutumikia Mashahidi wa Yehova zaidi ya 100,000. Tangu hapo, wenye kujitolea zaidi ya 800 walio stadi katika kazi za ujenzi nao wakiwakilisha matawi 12 wamekuwa wakisaidia kwenye miradi ya ujenzi wa matawi 13. Wafanya kazi fulani walijitolea kwa muda usiopungua mwaka mmoja, wengine walikaa kwa majuma mawili kufika miezi mitatu. Wenye kujitolea hawa na jamaa zao wanahisije juu ya mgawo kama huu? Hapa pana baadhi ya maelezo yao:
◻ “Kwa miaka mingi mimi nimefanya kazi ngumu, lakini katika ulimwengu. Sasa nishati zangu zote huliendea tengenezo la Yehova. Kutokuwa na lo lote la kufanya na ulimwengu ni kitulizo, na kujitumikisha mwenyewe kwa ajili ya Yehova ni shangwe kimwili, kimoyoni, na kiroho.”
◻ “Ni vigumu kueleza yale maurafiki yenye nguvu yaliyositawi katika ule muda mfupi nilipofanya kazi katika mradi huu.”
◻ “Sisi tukiwa jamaa tunataka kushukuru ninyi kwa pendeleo ambalo mume wangu amekuwa nalo akiwa mfanya kazi wa ujenzi wa kimataifa. Hata ingawa hakuna ye yote wetu aliyeweza kwenda pamoja naye, ujuzi wake umenufaisha jamaa kwa ujumla. Hiyo inaonyesha sisi jinsi tengenezo la Yehova lilivyo na umoja kila mahali. Pia, hilo lilisaidia yeye kuona jinsi sisi tunavyoweza kurahisisha maisha zetu ili kwamba sisi, tukiwa jamaa, tuweze kutumikia Yehova kwa ukamili zaidi.”
[Sanduku/Picha katika ukurasa wa 24, 25]
Mpanuo Katika Makao Makuu
Katika Januari 1983 Sosaiti ilinunua katika Brooklyn, New York, nusu moja ya eneo lenye nyumba mjini lenye meta 61 likiwa na jengo la kiwanda lenye orofa tisa. Jengo hili sasa limetengenezwa upya kabisa. Kisha katika Desemba 1986 Sosaiti ikanunua ile nusu nyingine ya eneo lile lile lenye nyumba likiwa na jengo jingine la kiwanda lenye orofa tisa. Majengo mawili haya sasa yanaunganishwa na daraja lenye urefu wa meta 49 na upana wa meta 4 kwenye jengo-la-majengo la kiwanda cha kwanza chenye majengo manne.
Tangu 1978 Sosaiti imeweka na kuendesha katika kiwanda chayo cha Brooklyn matbaa nane zenye mwendo wa juu, aina ya Harris, zinazochapa vikuto vya karatasi mfululizo kwa mtindo wa ofseti na zenye rangi nne. (Matbaa nne kama hizo zinatumiwa kiwandani kwenye Mashamba ya Mnara wa Mlinzi, umbali wa kilometa 160 kaskazini mwa Brooklyn.) Ili kwenda sambamba na mahitaji yenye kuongezeka ya kuchapa Biblia, wakati wa mwaka wa utumishi uliopita Sosaiti ilinunua matbaa zaidi mpya tatu za ofseti. Hizo ni matbaa Hantscho zenye mwendo wa juu, zenye rangi nne na sehemu tano, ambazo huchapa vikuto vya karatasi mfululizo kwa mtindo wa ofseti. Mbili za hizi ni matbaa-vikuto-mbili za kuchapia vitabu na magazeti. Ile nyingine ni matbaa-vikuto-nne yenye urefu wa meta 35 ya kuchapia kwa kutumia karatasi ya Biblia. Pamoja na matbaa mpya hii, kiwanda cha Brooklyn sasa kina matbaa tatu kwa ajili ya uchapaji wa kutumia karatasi ya Biblia.
Nyongeza ya mali kwa ajili ya makao ya jamaa ya Betheli ya Brooklyn ilipatikana katika Februari 1987. Jengo la orofa 11 liko kwenye 97 Columbia Heights na litakuwa na vyumba 127, pamoja na egesho la magari 30 la chini ya ardhi. Akidu (mjenzi wa kandarasi) aliyeajiriwa alimaliza kujenga ukuta wa nje wa mjengo, na wafanya kazi wa Sosaiti watamaliza ujenzi wa ndani kufikia karibu na Septemba 1988.
[Picha]
Majengo mawili ya kiwanda yenye orofa tisa yaliyonunuliwa juzijuzi yanayochukua eneo la nyumba za mjini
[Picha]
Jengo jipya la kao la Betheli lenye orofa 11, kwenye 97 Columbia Heights
[Chati katika ukurasa wa 34-41]
RIPOTI YA MWAKA WA UTUMISHI WA 1987 WA MASHAHIDI WA YEHOVA ULIMWENGUNI POTE
(Ona nakala iliyochapishwa)
[Picha katika ukurasa wa 7]
Ureno ilikuwa na vilele saba vya wahubiri, ikipita alama ya 32,000 kwa mara ya kwanza
[Picha katika ukurasa wa 15]
“Tumaini Katika Yehova” Mikusanyiko ya Wilaya ilivutia umati wa watu uliovunja rekodi
[Picha katika ukurasa wa 18]
Jumba la Ufalme lililojengwa karibuni, Kerala, India
[Picha katika ukurasa wa 26]
Matawi ambako wafanya kazi wa kimataifa wa ujenzi wa kujitolea walisaidia